TAIFA Stars timu ya soka ya Taifa ya Tanzania,imefanikiwa kulala ikiwa nyumbani baada ya kufungwa mabao 4-2 dhidi ya Ivory Coast na kuzima harakati za hapa na pale za kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014 huko Brazil.
Amini watanzania
wengi na wadau wa michezo nchini waliweka matumaini na kudhani Taifa Stars ingeweza kusonga mbele katika
harakati hizo za kufuzu kucheza Kombe la Dunia 2014, lakini sasa ukweli
kila kitu kipo wazi na ukweli umejionyesha.
Asilimia kubwa ya watanzania Sasa
wamekubaliana na uhalisia wa mambo kwamba Timu ya Taifa ifike tunako taka inahitaji muda kidogo kuona
Taifa Stars ikisonga mbele katika kuelekea kufuzu Kombe la Dunia na siyo rahisi
kama ilivyodhaniwa hapo kabla.
Ni
mambo mengi yaliyotokea katika mchezo dhidi ya Ivory Coast ambayo yaliigharimu
Taifa Stars licha ya uwanja kujaa idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa
wakiishangilia timu yao bila kuchoka.
Jambo
la msingi ni kwamba, Taifa Stars ikiwa katika harakati za kuhakikisha inafuzu
Kombe la Dunia wengi tulisahau kwamba kiukweli ilikuwa ngumu kwa Taifa
Stars kufuzu fainali hizo japokuwa kwa mapenzi tulidhani timu hii ingeweza
kufuzu kwa kuanza na vipigo kwa timu za Morocco na Ivory Coast.
Tukitazama
mchezo kati ya Taifa Stars na Ivory Coast kuna baadhi ya mambo yalionekana
kwamba bado tuna safari ndefu ya kufuzu Kombe la Dunia kama kweli tuna nia ya
kufanya hivyo.
Mambo
mengi mno yalijitokeza katika mchezo kati ya Taifa Stars dhidi ya Ivory Coast
na haya ni machache kati ya mengi yake.
1.Umakini wa safu ya ulinzi ulikuwa hafifu -katika kudhibiti kasi ya Salomon Kalou pamoja na Gevinho walikuwa mwiba katika safu ya ulinzi ya tanzania.

Hapa katika hali ya kawaida ilionekana upande wa mchezaji Erasto Nyoni unaweza kubeba lawama nzito lakini halikuwa kosa lake kwani alilazimika kwenda katikati kuongeza nguvu na kusawazisha makosa ya mabeki wa kati ambapo ilipelekea kusahau nafasi yake na majukumu aliyopewa.
Katika hali ya kawaida kiukweli ilionekana‘njia’ tangu dakika za mwanzo, beki Erasto Nyoni inaonekana
hakupata ushauri wa kutosha kuhusu kutulia na kucheza soka kwani hata makelele
ya mashabiki yalimfanya aonekane mtu asiyefa hatuweza kumlaumu.
2.Nguvu ndogo ya wachezaji wa Taifa Star-
2.Nguvu ndogo ya wachezaji wa Taifa Star-
Safu
ya kiungo- kwa upande wa Ivory Coast ikisimamiwa vilivyo na Yaya Toure licha ya mchezo wa jana kucheza safu ya ushambuliaji aliweza kutimiza majukumu aliyopewa na kocha wake kiukweli kiungo huyu wa Club ya Man city alionyesha uwezo wake na kuwazidi wachezaji wa Taifa Star Abubakar Sure boy ambaye ni mfupi na mwenye umbo dogo alionekana mchezaji wa kawaida mbele ya Yaya Toure ambapo pia Frank domayo pamoja na Mwinyi
Kazimoto licha ya kucheza vizuri lakini maumbo yao walionekana kutoweza kuhimili mikimikiya Traore Lucina na Jean Jacques ambao wote ni
watu wenye miili mikubwa pia hilo lilikuwa moja ya jambo lililoigharimu timu.
4.Umakini Mbovu wa Safu ya Ushambuliaji- Licha ya kuonyesha kiwango cha hali ya juu Mbwana Samata ,Tomas Ulimwengu pamoja na Amri Kiemba kwa kushirikiana kwa pamoja na kuweza kupata Mabao Mawili" Hapa wachezaji hawa walionekana kutopeana nafasi na kujipanga vizuri kuhakikisha wanajipatia nafasi nzuri za kutupia mabao wavuni.
5.Mbali ya yote'' Taifa star inastahili pongezi kwa kuweza kumiliki mpira na kuonyesha kandanda safi katika mchezo huo hivyo kubwa zaidi watanzania tuamini kabisa katika michuano ya CHAN inayo kuja lazima tutashiriki kutokana na ubora wa kocha wetu Kim Poulsen ambaye kiukweli ameweza kuitengeneza timu kucheza kwa kujiamini licha ya kupoteza mchezo ule" Hivyo kubwa zaidi ni kuipa Support Timu yetu ya Taifa. Ahsanteni.
3.Ubora wa wachezaji wa Ivory Coast-Kila mtu anafahamu Kabisa kuwa kikosi cha Timu ya hiyo kinawachezaji wengi wenye uzoefu wanaocheza katika ligi mbalimbali Barani ulaya wemeonekana kujiamini mbele ya wachezaji wa Taif Star na kujipa Matumaini kuwa wataibuka na ushindi katika mchezo ule. kwa ufupi tu kwa haraka haraka kila mdau wa michezo anafahamu uwezo wa Yaya Toure,Solomon Kalou,Gervinho na wengineo kina Bakari Kone nk.

5.Mbali ya yote'' Taifa star inastahili pongezi kwa kuweza kumiliki mpira na kuonyesha kandanda safi katika mchezo huo hivyo kubwa zaidi watanzania tuamini kabisa katika michuano ya CHAN inayo kuja lazima tutashiriki kutokana na ubora wa kocha wetu Kim Poulsen ambaye kiukweli ameweza kuitengeneza timu kucheza kwa kujiamini licha ya kupoteza mchezo ule" Hivyo kubwa zaidi ni kuipa Support Timu yetu ya Taifa. Ahsanteni.