Wednesday, July 3, 2013

USAJILI WAPAMBA MOTO BARANI ULAYA

Stoke City wamemsaini Beki wa Kimataifa wa Timu ya Spain U-21 Marc Muniesa anaecheza Barcelona kwa Uhamisho wa bure.
Muniesa, Miaka 21, ni mmoja wa Wachezaji wa Spain ambayo ilitwaa Ubingwa wa EURO 2013 kwa U-21 hivi karibuni na anajiunga na Stoke kwa Mkataba wa Miaka minne.
Huyu ni Mchezaji wa pili kuchukuliwa na Meneja mpya wa Stoke, Mark Hughes, baada ya Wiki iliyopita kumsaini Erik Pieters kutoka PSV Eindhoven.
SWANSEA YAKUBALIANA NA LIVERPOOL KUHUSU JONJO
Swansea City imeafikiana na Liverpool Ada ya Pauni Milioni 6 ya kumhamisha Kiungo Jonjo Shelvey na Mchezaji huyo sasa atakutana na Swansea ili kukamilisha makubaliano ya Maslahi yake binafsi.
Jonjo Shelvey, Miaka 21, alisainiwa na Liverpool kutoka Charlton Athletics kwa Dau la Pauni 1.7 Miaka mitatu iliyopita lakini akiwa Anfield kupata namba kwake kumekuwa nadra na Meneja Brendan Rodgers amemruhusu kutafuta Klabu nyingine.
Shelvey aliichezea England kwa mara ya kwanza Novemba Mwaka jana ilipofungwa na Sweden na pia amecheza Mechi 17 za Ligi huko Anfield Msimu uliopita.
Jana Swansea ilitangaza kuwasaini Wachezaji watatu wengine ambao ni Alejandro Pozuelo, Miaka 21, kutoka Real Betis ya Spain, Kipa wa Miaka 17, Gregor Zabret kutoka Klabu ya Slovenia NK Domzale na Alex Gogic, Kiungo wa Miaka 19 kutoka Klabu ya Greece, Olympiakos.
ARSENAL_NA_MCHEZA_RAGAARSENAL YAMCHUKUA MCHEZA RAGA!
Katika azma yao ya kukiimarisha Kikosi chao kuwa na nguvu na Misuli inayostahili kwa ajili ya Msimu mpya, Klabu ya Arsenal imemuajiri Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Ireland wa Mchezo wa Raga, Jerry Flannery, kuwa Kocha wao mpya wa kujenga nguvu, musili na stamina kwa Wachezaji wao.
Flannery, Miaka 34, alistaafu mapema kucheza Raga baada ya kuumia Misuli za Mguu.
MOURINHO AZUNGUMZA NA MARCO VAN GINKEL
Chelsea imefanya mazungumzo na Kiungo wa Vitesse Arnhem, Marco van Ginkel, ili ahamie Stamford Bridge.
Van Ginkel, Miaka 20, ameshakutana na Jose Mourinho na Alhamisi ataongea na Klabu yake ya Uholanzi ili apate baraka za Uhamisho.
Marco van Ginkel alijiunga na Vitesse Arnhem akiwa na Miaka 7 tu na kupanda kwenye Vyuo vya Klabu hiyo hadi Aprili 2010 alipocheza Timu ya Kwanza kwa mara ya kwanza.
Van Ginkel anathaminiwa kuwa na Dau la Pauni Milioni 8 na Mkataba wake na Klabu yake unamalizika Juni 2015.
Ikiwa Uhamisho huu utakamilika, huu utakuwa ni usajili wa pili kwa Jose Mourinho baada ya Wiki iliyopita kumnasa Mchezaji wa Kimataifa wa Germany, Andre Schurrle, kutoka Klabu ya Bundesliga, Bayer Leverkusen.

MESSI ASEMA BARCELONA ILIFANYA SAHIHI KUMNASA NEYMAR

Mshambuliaji nyota duniani wa kimataifa wa Argentina na klabu ya Barcelona, Lionel Messi anaamini kuwa klabu hiyo ilifanya jambo sahihi kumsajili Neymar katika kampeni yao ya kutetea taji La Liga na kufanya vyema katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao. Neymar mwenye umri wa miaka 21 alikamilisha usajili wake uliogharimu kiasi cha euro milioni 57 akitokea Santos Juni mwaka huu ingawa hatahivyo wakosoaji wanadai Barcelona ilifanya makosa kutumia fedha nyingi kumsajili nyota huyo ambaye hajawahi kucheza Ulaya. 
Lakini baada ya kufunga mabao manne katika michuano ya Kombe la Shirikisho ilikiwemo bao moja katika ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya mabingwa wa Dunia Hispania wakooaji hao watakuwa wameshapata majibu ya maswali yao na Messi anategemea nyota huyo kufanya makubwa zaidi atakapokuwa Barcelona. Messi amesema anategemea Neymar ataleta mchango mkubwa katika klabu hiyo kama akiendelea kucheza katika kiwango cha juu kama ilivyo kwa timu yake ya taifa na Santos. Barcelona ilifanikiwa kunyakuwa taji la La Liga msimu uliopita lakini walipata kipigo kikubwa kutoka Bayern Munich kwenye mechi za nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ambapo waling’olewa kwa kufungw ajumla ya mabao 7-0 katika mechi mbili walizocheza.

KUNANI HAPO?BOLOVIA MIAKA 17 IJAYO VIJANA KUITWA NEYMAR"

Katika taarifa za takwimu za ofisi ya msajili jijini La paz, Bolivia miaka 17 ijayo vijana wengi wa kiume wanaoishi katika mji huo watakuwa wakiitwa jina la mshambuliaji mpya wa fc barca Neymar. Katika taarifa iliyotolewa na gazeti moja nchini humo watoto 20 kati ya 100 wanaozaliwa katika mji mkuu huo wan chi hiyo wamepewa jina la nyota huyo mpya wa Barcelona ambaye amewateka mashabiki dunia nzima kutokana na kiwango cha hali ya juu alichokionyesha katika michuano ya Kombe la Shirikisho. Ofisa mmoja aliyetambulika kwa jina la Remigio Condori amesema wazazi wengi katika mji huo wanachagua jina la Neymar kwakuwa ndio liko katika fasheni ambapo miaka 17 ijayo vijana wengi wa kiume watakuwa wakiitwa jina hilo. Neymar ambaye amsajili na Barceona kwa ada ya euro milioni 57, alifunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 4-0 iliyopata Brazil dhidi ya Bolivia April mwaka huu.

ARSENAL KATIKA MVUTANO NA REAL MADRID-HIGUAIN"

Katika harakati za usajili mara baada ya kuinasa saini ya nyota wa klabu ya AJ Auxerre, Yaya Sanogo klabu ya Arsenal sasa inapambana kukamilisha kumsajili nyota wa klabu ya Real Madrid, Gonzalo Higuain. 
Klabu hizo mbili zimekuwa katika mvutano kuhusu ada ya uhamisho wa nyota huyo ambapo Arsenal wameonekana kuwa tayari kutoa kitita cha euro milioni 25, wakati Madrid wao wanataka ada iwe euro milioni 25.5. Kumekuwa na taarifa kuwa Arsenal wameshafikia makubaliano binafsi na mchezaji huyo ambapo ataanza na mshahara wa paundi 100,000 kwa wiki, mshahara ambao utamfanya kuwa mmoja wa wachezaji wanaolipwa zaidi kwenye klabu hiyo wakiwemo Theo Walcott na Thomas Vermaelen. Higuain ambaye nia raia wa Argentina inasenekana alikuwa akilipwa kiasi cha paundi 64,000 kwa wiki akiwa Madrid.

Tuesday, July 2, 2013

BRAZIL HAINA UBAVU DHIDI YA HISPAIN IJAPO KUWA IMESHINDA 3-0


NGULI wa soka Duniani Raia wa Argentina, Diego Maradona anaamini kuwa Hispania wasingepoteza mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Brazil kama wangecheza katika uwanja huru. Mabingwa hao wa Ulaya na Dunia walitandikwa mabao 3-0 katika Uwanja wa Maracana na Maradona mwenye umri wa miaka 52 anaamini kuwa mazingira yalikiathiri kikosi cha Hispania kinachonolewa na Vincente Del Bosque. Akihojiwa na waandishi wa habari katika ziara ya nchini Indonesia Maradona amesema Hispania hawakuwa na bahati kwakuwa walikuwa wakicheza nchini Brazil na anaamini kuwa nchi hiyo isingewafunga kama mchezo huo ungechezwa katika uwanja huru. Maradona pia hakusita kumsifia Lionel Messi na kudai kuwa bado ni mchezaji bora na mahasimu wake Cristiano Ronaldo na Neymar bado hawajafikia ubora wake.

NEYMAR NA ALBA KUFANYIWA UPASUAJI WA MAFINDIFINDO YA SHIGONI"TOSEZI"


Mkali mpya wa FC Barcelona, Neymar na beki Jordi Alba wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mafindofindo Ijumaa na wanatarajiwa kupona baada ya siku 10. Upasuaji huo ulipangwa kufanyika baada ya fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho iliyofanyika jijini Rio de Janeiro Jumapili iliyopita ambapo Brazil iliisambaratisha Hispania kwa mabao 3-0. Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo Neymar anatarajiwa kufanyiwa upasuaji huo huko Rio na baadhi ya madaktari wa Barcelona wanakuwepo kusaidia. Wakati Alba mwenye miaka 24 yeye atafanyiwa upasuaji wake siku hiyohiyo lakini katika kliniki iliyopo karibu na jiji la Barcelona na wote wanatarajiwa kupona ndani siku 10 baada ya upasuaji huo.

ARSENAL SASA YAJIWEKA KAMILI GADO KWA MSIMU MPYA WA BPL NCHINI UINGEREZA"

Wakiwa chini ya kocha Mfaransa, Aserne Wenger Timu ya soka ya Arseanal wamefanikiwa kuinasa saini ya nyota kinda wa kimataifa kutoka nchini Ufaransa, Yaya Sanogo kwa kumpa mkataba mrefu Emirates.
Kinda huyo kwa sasa yupo na timu ya taifa ya vijana ya Ufaransa chini ya umri wa miaka 20m katika fainali za Kombe la Dunia la vijana chini ya umri wa miaka 20 huku akiwa amefumania nyavu mara mbili kati ya matatu ya timu yake nchini Uturuki.
Akicheza ligi daraja la kwanza nchini Ufaransa, Sanogo  amefunga mabao tisa  katika mechi 13 huku akiandamwa na majeruhi ya mara kwa mara.
Target man: Sanogo has built an excellent reputation for himself in France 
Mtu mwenye dili kwa sasa: Sanogo amejijengee nafasi nzuri sana katika taifa la Ufaransa
More to come? Higuain (left) and Rooney (right) are also thought to be on Wenger's wishlist 
Nyota wengine wa kutua Emirates? Higuain (kushoto) na Rooney (kulia) pia wapo katika rada za Wenger ambaye anataka kupata nyota wakali wa kuimarisha kikosi chake msimu ujao
Gonzalo Higuain na Wayne Rooney wameripotiwa kuwa katika mipango ya Wenger msimu ujao, lakini kocha huyo raia wa Ufaransa amevutiwa na kinda Sanogo.
‘Sanogo ni mchezaji mzuri sana atakayesaini kwetu, ameonesha kiwango kikubwa katika klabu yake ya Auxerre na katika kikosi cha timu ya taifa chini ya umri wa miaka 20″. Alisema Wenger.