Club ya Bayern Munich na Borussia Dortmund
zinataraji kushuka dimba siku Jumamosi katika Mechi ya fungua pazi Msimu mpya kugombea
German Super Cup haya yakiwa kama Marudiano ya Fainali ya Mwezi Mei Uwanjani Wembley ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ambayo Bayern walishinda Bao 2-1 na kuweka historia ya kuwa Klabu ya kwanza Nchini Germany kutwaa Trebo, yaani Ubingwa wa Germany, Kombe la Germany na Ubingwa wa Ulaya.
German Super Cup haya yakiwa kama Marudiano ya Fainali ya Mwezi Mei Uwanjani Wembley ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ambayo Bayern walishinda Bao 2-1 na kuweka historia ya kuwa Klabu ya kwanza Nchini Germany kutwaa Trebo, yaani Ubingwa wa Germany, Kombe la Germany na Ubingwa wa Ulaya.
Hata hivyo, Dortmund wamesema wao
hawasaki kisasi pale Beki wao anaechezea Germany, Mats Hummels,
aliposema: “Hii si kisasi cha Wembley! Ni mtihani mzuri kuonyesha Msimu
huu tukoje!”
Kawaida German Super Cup hugombewa na
Bingwa na yule Mshindi wa Kombe la Germany lakini kwa vile vyote
vilichukuliwa na Bayern Msimu uliopita, Mshindi wa Pili wa Bundesliga,
ambae ni Borussia Dortmund aliemaliza Pointi 25 nyuma, ndie atacheza na
Bayern Munich.
Sura Mpya
Kila Timu, Bayern Munich na Borussia
Dortmund, zitaingia kwenye Mechi hii na sura mpya huku Bayern ikiwa na
Kocha mpya Pep Guardiola aliembadili Jupp Heynckes, Thiago Alcantara wa
Spain akiwa Bayern kutoka Barcelona na Mario Gotze akiwa pia Bayern
kutoka Dortmund.
Dortmund pia wanao wapya ambao ni Viungo
Pierre-Emerick Aubameyeng toka St Etienne na Henrikh Mkhitaryan kutoka
Shakhtar Donetsk lakini wote hawa wapya huenda wasicheze kutokana na
kuwa na maumivu.
Tayari Tiketi zote, 80,654 za
Westfalenstadion, kama ilivyo maarufu Signal Iduna Park, zimeshauzwa na
Mechi hii itatangazwa Nchi 195 Duniani.