Monday, April 14, 2014

KATIBU MKUU FIFA JEROME VALCKE KUFUNGUA SEMINA DAR

KATIBU MKUU WA FIFA KUFUNGUA SEMINA DAR

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Jerome Valcke atawasili nchini Mei 1 mwaka huu ambapo atafungua semina ya mawasiliano itakayoshirikisha viongozi wa vyama wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Akizungumza Dar es Salaam leo (Aprili 14 mwaka huu), Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema Valcke ambaye hii ni mara yake ya kwanza kuja Tanzania atafuatana na maofisa wengine wa saba wa FIFA.
Amesema semina hiyo iliyoandaliwa na FIFA itafanyika kwa siku mbili (Mei 1 na 2 mwaka huu) ambapo vilevile Valcke atapata fursa ya kuzungumza na waandishi wa habari wa ndani na wa kimataifa.
TFF_LOGO12Rais Malinzi amesema washiriki wa semina hiyo ni marais, makatibu wakuu na wakuu wa mawasiliano wa wanachama 12 wa CECAFA ambao ni Burundi, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Somali, Sudan, Sudan Kusini, Tanzania na Uganda.
Naye Mwenyekiti wa CECAFA, Leodegar Tenga ambaye alifuatana na Katibu Mkuu wake Nicholas Musonye amemshukuru Rais wa TFF kwa kukubali kuwa mwenyeji wa semina hiyo kwani itasaidia katika maendeleo ya mpira wa miguu katika ukanda huu.
RAMBIRAMBI MSIBA WA JOSEPHAT MAGAZI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Mwenyekiti wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu (FRAT) Mkoa wa Singida, Josephat Magazi kilichotokea jana mkoani Kilimanjaro.
Magazi ambaye pia aliwahi kuwa mwamuzi na kamishna wa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) alikuwa amelazwa katika Hospitali ya KCMC. Mazishi yatafanyika kesho (Aprili 15 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwao Ushirombo mkoani Shinyanga.
Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Magazi alishirikiana na TFF na wadau wengine wa mpira wa miguu katika masuala ya uamuzi na uongozi, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Magazi, FRAT na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Singida (SHIREFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Sunday, April 13, 2014

VPL: AZAM FC YATWAA UBINGWA, YAVUNJA MWIKO WA TANGU 2000

AZAM FC wakiWA katika dimba la Uwanja wa Sokoine, Mbeya, wamefanikiwa kutangaza ubingwa wakiwa na mechi moja mkononi baada kuichalaza mbeya city bao 2-1 na  kuvunja rekodi ya muda mrefu kwa timu zinazoshiriki VPL kutotwaa Ubingwa kwa Klabu nyingine mbali ya Yanga na Simba wa tangu Mwaka 2000.
Azam FC imefuta USIMBA NA UYANGA ambapo Yanga na Simba tangu Mwaka 2001 ambapo, baada ya Mtibwa kuutwaa Mwaka 2000 na kuutetea Mwaka 2001, Yanga na Simba zimekuwa zikipishana kwa kuubeba.
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
GF
PTS
1
Azam FC
25
17
8
0
35
50
59
2
Yanga SC
25
16
7
2
42
60
55
3
Mbeya City
25
12
10
3
12
31
46
4
Simba SC
25
9
10
6
14
40
37
Katika Mechi nyingine zilizochezwa Leo, Yanga waliichapa JKT Oljoro Bao 2-1 hukO Arusha na Jijini Dar es Salaam, Simba ilitunguliwa Bao 1-0 na Ashanti United.
VPL itakamilika Wikiendi ijayo Aprili 19 kwa Timu zote 14 kuwa Dimbani.
RATIBA/MATOKEO:
Jumapili Aprili 13
Simba 0 Ashanti United 1 (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam)
Mbeya City 1 Azam 2 (Sokoine, Mbeya)
JKT Oljoro 1 Yanga 2 (Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).
Mgambo Shooting 1 vs  1 Kagera Sugar (Mkwakwani, Tanga),
MABINGWA WALIOPITA:
1965 Sunderland (Sasa ni Simba SC)
1966 Sunderland
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans
2006 Young Africans
2007 Simba SC
2007/08 Young Africans
2008/09 Young Africans
2009/2010 Simba SC
2010/2011 Young Africans
2011/2012 Simba SC
2012/2013 Young Africans

Friday, April 11, 2014

UCL UEFA: SI MCHEZO NUSU FAINALI REAL VS BAYERN, ATLETI VS CHELSEA.

UEFA CHAMPIONZ LIGI Droo ya Mashindano makubwa ya Barani Ulaya imefanyika Leo huko Nyon, Uswisi, na Timu za Spain, Real Madrid na Atletico Madrid zimetenganishwa.
Mabingwa Watetezi Bayern Munich wataivaa Real Madrid na Vinara wa La Liga, Atletico Madrid, watapambana na Chelsea.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
NUSU FAINALI:
-Real Madrid v Bayern Munich
-Atletico Madrid v Chelsea
Mechi ya Kwanza: 22 & 23 Aprili
Mechi ya Pili: 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
EUROPA LIGI:
Kwenye Droo ya Nusu Fainali ya EUROPA LIGI, Klabu za Spain, Sevilla na Valencia zimekutanishwa na Mechi nyingine ni kati ya Benfica ya Ureno na Mabingwa wa Italy, Juventus.
EUROPA LIGI:
NUSU FAINALI:
-Sevilla v Valencia
-Benfica v Juventus
Mechi ya Kwanza: Aprili 24
Mechi ya Pili: Mei 1
FAINALI: Jumatano Mei 14, Juventus Stadium, Turin, Italy

VPL: MOTO KUWAKA KESHOSIMBA, ASHANTI UTD KUVAANA TAIFA

CHACHA KUCHEZESHA MICHUANO YA AYG
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua mwamuzi msaidizi wa Tanzania anayetambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Ferdinand Chacha ameteuliwa kuchezesha michezo ya Vijana ya Afrika (AYG- African Youth Games).

Michezo hiyo ya kwanza ya Afrika itachezesha jijini Gaborone, Botswana kuanzia Mei 22-31 mwaka huu. Tanzania pia itashiriki katika mashindano hayo ya vijana wenye umri chini ya miaka 15.

SIMBA, ASHANTI UTD KUVAANA TAIFA
Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho(Aprili 12 mwaka huu)  katika raundi ya 25 ambapo Simba na Ashanti United zitapambana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.

Mechi nyingine zitakuwa kati ya Tanzania Prisons na Rhino Rangers (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya) wakati Coastal Union itakuwa mwenyeji wa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Keshokutwa (Aprili 13 mwaka huu) kutakuwa na mechi nyingine nne za kukamilisha raundi hiyo. Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya wenyeji Oljoro JKT na Yanga.

Mtibwa Sugar itacheza na Ruvu Shooting (Uwanja wa Manungu, Morogoro), Mgambo Shooting na Kagera Sugar zitaoneshana kazi kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga huku Mbeya City ikiumana na Azam kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

TIMU YA WATOTO WA MITAANI YATAMBULISHWA BUNGENI
Timu ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania iliyotwaa ubingwa wa Dunia wa Watoto wa Mitaani nchini Brazil baada ya kuifunga Burundi mabao 3-1 kwenye fainali imetambulishwa leo (Aprili 11 mwaka huu) katika Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma.

Baadaye timu hiyo leo itapata chakula cha mchana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda. Saa 10 jioni itatembeza kombe hilo katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Dodoma katika gari za wazi.

Jioni imeandaliwa hafla maalumu ya chakula pamoja na burudani hapo hapo mjini Dodoma ambapo mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara.

MWENYEKITI WA CECAFA KUZUNGUMZA NA WAANDISHI
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Leodegar Tenga atakuwa na mkutano na waandishi wa habari Jumatatu (Aprili 14 mwaka huu).

Mkutano huo utafanyika kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) zilizopo Ghorofa ya 3, Jengo la PPF Tower mtaa wa Ohio/Garden Avenue kuanzia saa 5 kamili asubuhi.

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Thursday, April 10, 2014

FIFA LISTI UBORA DUNIANI: SPAIN1, TANZANIA YA 122

Droo ya Listi ya ubora ya fifa  iliyotolewa Leo imeonyesha Mabingwa wa Dunia Spain bado wapo Nambari Wani wakifuatiwa na Germany, ambao wamebakia Namba 2, huku Tanzania ikiporomoka Nafasi 5 na kushika Nafasi ya 122 wakati Nafasi ya Juu kabisa kwa Nchi ya Afrika inakamatwa na Ivory Coast ambao wako Nafasi ya 21wakiwa wamepanda Nafasi 3.
FIFA_LOGOWenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia Mwaka huu, Brazil, wamepanda Nafasi 3 na sasa wapo Namba 6 pamoja na Argentina walioporomoka Nafasi 3.
Listi nyingine ya Ubora Duniani itatolewa tena na FIFA hapo Tarehe 8 Mei.
20 BORA DUNIANI:
1        Spain
2        Germany
3        Portugal       [Wamepanda Nafasi 1]
4        Colombia      [Wamepanda Nafasi 1]
5        Uruguay        [Wamepanda Nafasi 1]
6        Argentina     [Wameshuka Nafasi 3]
6        Brazil            [Wamepanda Nafasi 3]
8        Switzerland   [Wameshuka Nafasi 1]
9        Italy             [Wameshuka Nafasi 1]
10      Greece          [Wamepanda Nafasi 3]
11      England        [Wamepanda Nafasi 1]
12      Belgium        [Wameshuka Nafasi 2]
13      USA              [Wamepanda Nafasi 1]
14      Chile             [Wamepanda Nafasi 1]
15      Netherlands  [Wameshuka Nafasi 4]
16      France           [Wamepanda Nafasi 1]
17      Ukraine        [Wamepanda Nafasi 1]
18      Russia           [Wamepanda Nafasi 1]
19      Mexico          [Wamepanda Nafasi 1]
20      Croatia         [Wameshuka Nafasi 4]

UCL: BAYERN YAIPIGA MAN UNITED 3-1,BARCA NJE.

ROBO FAINALI
Marudiano
Jumatano Aprili 9
{Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili}
Bayern Munich 3 Manchester United 1 [4-2]
Atletico Madrid 1 Barcelona 0 [2-1]
Mabingwa Watetezi wa UCL, UEFA Championz Bayern Munich, jana Usiku wamefanikiwa kutinga Nusu Fainali ya Mashindano hayo baada ya kuitandika Manchester United goli 3-1 katika Mechi ya Marudiano ya Robo Fainali.
Katika Mtange wa Kwanza huko Old Trafford Wiki iliyopita, Timu hizi zilitoka Sare ya Bao 1-1.
Kwenye Mechi hii, Man United walitangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 57 la Patrice Evra lakini Bayern walijibu haraka na kusawazisha Dakika 2 baadae kwa Bao la Mario Mandzukic na kuongeza Bao mbili kupitia Thomas Muller, Dakika ya 68 na Arjen Robben, Dakika ya 76.
Bayern sasa wanaungana kwenye Nusu Fainali ya UCL pamoja na Chelsea, Atletico Madrid na Real Madrid.
Droo ya kupanga Mechi za Nusu Fainali itafanyika Ijumaa Aprili 11.
VIKOSI:
BAYERN MUNICH: Neuer, Dante, Ribery, Mandzukic, Robben, Boateng, Gotze, Lahm, Muller, Alaba, Kroos.
Akiba: Raeder, Van Buyten, Rafinha, Pizarro, Weiser, Hojbjerg, Weihrauch.
MAN UNITED: De Gea; Jones, Smalling, Vidic, Evra; Fletcher, Carrick; Valencia, Rooney, Kagawa; Welbeck.
Akiba: Lindegaard, Büttner, Ferdinand, Giggs, Januzaj, Young, Hernandez.
REFA: Jonas Eriksson [Sweden]
Goli la Dakika ya 5 la Koke limewapa ushindi Atletico Madrid wa Bao 1-0 dhidi ya Barcelona walipocheza Uwanjani kwao Estadio Vicente Calderon katika Mechi ya Marudiano ya Robo Fainali wa ligi ya mabingwa UCL,
katika mtanange wa awali timu hizi zilitoka Sare ya Bao 1-1 huko Nou Camp Wiki iliyopita.
Katika Mechi hiyo, Atletico walianza kwa kishindo na mbali ya kufunga Bao hilo mapema pia walipiga Posti mara 3 ndani ya Dakika 20 za kwanza.
Hii ni mara ya kwanza kwa Atletico kuingia Nusu Fainali ya Mashindano haya tangu Mwaka 1974 na ni mara ya kwanza kwa Barca kushindwa kuingia Nusu Fainali tangu 2007.
Msimu huu, Timu hizi zimekutana mara 4 na kutoka Sare.
Atletico sasa wanaungana kwenye Nusu Fainali ya UCL pamoja na Chelsea, Bayern Munich na Real Madrid.
Droo ya kupanga Mechi za Nusu Fainali itafanyika Ijumaa Aprili 11. 
VIKOSI:
Atletico Madrid: Courtois, Godin, Filipe Luis, Juanfran, Miranda, Tiago, Koke, Raul Garcia, Gabi, Adrian, Villa
Akiba: Aranzubia, Mario Suarez, Rodriguez, Alderweireld, Insua, Sosa, Diego.
Barcelona: Pinto, Mascherano, Bartra, Jordi Alba, Dani Alves, Fabregas, Xavi, Iniesta, Busquets, Messi, Neymar
Akiba: Oier, Montoya, Pedro, Alexis, Song, Adriano, Sergi Roberto.
REFA: Howard Webb [England]
UEFA CHAMPIONZ LIGI
ROBO FAINALI
Marudiano
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Jumanne Aprili 8
Chelsea 2 Paris Saint-Germain 0 {3-3}, Chelsea wamesonga kwa Bao la Ugenini}
Borussia Dortmund 2 Real Madrid 0 {2-3}
DONDOO MUHIMU:
-DROO YA NUSU FAINALI: 11 Aprili
-Mechi kuchezwa 22 & 23 Aprili na Marudiano 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
WASHINDI [Miaka ya karibu]:
MSIMU MSHINDI NCHI MSHINDI WA PILI NCHI GOLI
2012-13 Bayern Munich Germany Borussia Dortmund Germany 2-1
2011-12 Chelsea England Bayern Munich Germany 1-1 (4–3)
2010-11 Barcelona Spain Manchester United England 3-1
2009-10 Internazionale Italy Bayern Munich Germany 2-0
2008-09 Barcelona Spain Manchester United England 2-0
2007-08 Man United England Chelsea England 1-1 (6–5)

Wednesday, April 9, 2014

RUVU SHOOTING VS AZAM YAAHIRISHWA! YANGA YAPIGA 2-1 KAGERA KWA TABU.

VPL: LIGI KUU VODACOM
MATOKEO:
Jumatano Aprili 9
R/Shooting v Azam FC {Mechi imeahirishwa hadi alhamis aprili 10 mwaka huu}
Yanga 2 Kagera Sugar 1
MABINGWA Watetezi wa VPL, Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara, Wanajangwani Yanga sc, wakishuka katika dimba la Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam imefanikiwa kuibuka na ushindi ya kuinyuka Kagera Sugar Bao 2-1 na kujiwekea uimara katika mbio za kuwania ubingwa baada ya kujizatiti katika Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 1 nyuma ya Vinara Azam FC ambao Leo walishindwa kucheza Mechi yao kutokana na Mvua.
Hii Leo, Azam FC walikuwa wacheze huko Mabatini, Mlandizi dhidi ya Ruvu Shooting lakini Mechi hiyo ililazimika kuahirishwa kutokana na Mvua kubwa kufanya Uwanja ufurike maji.
Huku Timu zote zikiwepo Uwanjani, Waamuzi waliukagua Uwanja wa Mabatini na kujiridhisha kuwa haufai kuchezwa na ndipo wakaamua kuahirisha Mechi hiyo.
Habari za awali zimesema kuwa Mechi hii itachezwa kesho.
Huko Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga waliifunga Kagera Sugar Bao 2-1 kwa Bao za Kipindi cha Kwanza zikifungwa na Hamisi Kiiza, Dakika ya 3, na Didier Kavumbagu, Dakika ya 34 wakati Kagera Sugar walifunga Bao lao Dakika ya 63 kupitia Daud Jumanne.
Yanga, ambao wako Pointi 1 nyuma ya Vinara Azam FC, sasa wamebakisha Mechi mbili dhidi ya JKT Oljoro, huko Arusha, na Simba wakati Azam FC wana Mechi 3 dhidi Ruvu Shooting, Mbeya City huko Mbeya na JKT Ruvu.
RATIBA:
Jumamosi Aprili 12
Mtibwa Sugar vs Ruvu Shooting (Manungu, Morogoro),
Coastal Union vs JKT Ruvu (Mkwakwani, Tanga),
Tanzania Prisons vs Rhino Rangers (Sokoine, Mbeya).
Jumapili Aprili 13
Mgambo Shooting vs Kagera Sugar (Mkwakwani, Tanga),
Simba vs Ashanti United (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam)
Mbeya City vs Azam (Sokoine, Mbeya)
JKT Oljoro vs Yanga (Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
GF
PTS
1
Azam FC
23
15
8
0
31
45
53
2
Yanga SC
24
15
7
2
41
58
52
3
Mbeya City
24
12
10
2
13
30
46
4
Simba SC
24
9
10
5
15
40
37
5
Kagera Sugar
24
8
10
6
2
22
34
6
Ruvu Shooting
22
9
7
6
0
27
34
7
Mtibwa Sugar
25
7
10
8
0
28
31
8
Coastal Union
24
6
11
7
-2
16
29
9
JKT Ruvu
23
8
1
14
-19
19
25
10
Mgambo Shooting
23
6
6
11
-16
16
24
11
Ashanti UTD
23
4
7
12
-20
17
19
12
JKT Oljoro
24
3
9
12
-17
17
18
13
Prisons FC
22
3
9
10
-11
17
18
14
Rhino Rangers
23
3
7
13
-17
15
16