Katika
mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars)
na Burundi (Intamba Mu Rugamba) itakayochezwa Aprili 26 mwaka huu Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam kiingilio cha chini ni sh. 5,000.Mechi hiyo itakuwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kiingilio hicho ni kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa wa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000.
Taifa Stars inayodhaminiwa na
Kilimanjaro Premium Lager tayari ipo kambini kwenye hoteli ya Kunduchi Beach
kujiandaa kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka nchini
Kenya.
Burundi inatarajia kuwasili nchini keshokutwa (Aprili 22 mwaka huu) tayari kwa ajili ya mechi hiyo inayotajiwa kuwa ya kusisimua. Mechi hiyo imepangwa kuanza saa 10 jioni.
Burundi inatarajia kuwasili nchini keshokutwa (Aprili 22 mwaka huu) tayari kwa ajili ya mechi hiyo inayotajiwa kuwa ya kusisimua. Mechi hiyo imepangwa kuanza saa 10 jioni.
Wachezaji wa Taifa Stars waliopo
kambini ni Deogratias Munishi, Mwadili Ali, Aidan Michael, Aggrey Morris,
Erasto Nyoni, Hassan Mwasapili, Kelvin Yondani, Said Moradi, Amri Kiemba, Frank
Domayo, Himid Mao, Jonas Mkude, Athanas Mdamu, Haruna Chanongo, Juma Liuzio,
Khamis Mcha, Mrisho Ngasa, Ramadhan Singano na Simon Msuva.Wengine ni Benedicto Mlekwa, Emma Simwanda, Joram Mgeveje, Omari Kindamba, Edward M
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)




