Tuesday, April 22, 2014

JUMAMOSI TAIFA STARS NA BURUNDI KIINGILIO BUKU TANO

DSC_0178Katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na Burundi (Intamba Mu Rugamba) itakayochezwa Aprili 26 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kiingilio cha chini ni sh. 5,000.
Mechi hiyo itakuwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kiingilio hicho ni kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa wa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari ipo kambini kwenye hoteli ya Kunduchi Beach kujiandaa kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka nchini Kenya.
Burundi inatarajia kuwasili nchini keshokutwa (Aprili 22 mwaka huu) tayari kwa ajili ya mechi hiyo inayotajiwa kuwa ya kusisimua. Mechi hiyo imepangwa kuanza saa 10 jioni.

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/04/tff_LOGO12.jpg Wachezaji wa Taifa Stars waliopo kambini ni Deogratias Munishi, Mwadili Ali, Aidan Michael, Aggrey Morris, Erasto Nyoni, Hassan Mwasapili, Kelvin Yondani, Said Moradi, Amri Kiemba, Frank Domayo, Himid Mao, Jonas Mkude, Athanas Mdamu, Haruna Chanongo, Juma Liuzio, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa, Ramadhan Singano na Simon Msuva.
Wengine ni Benedicto Mlekwa, Emma Simwanda, Joram Mgeveje, Omari Kindamba, Edward M
ayunga, Shiraz Sozigwa, Yusuf Mlipili, Said Ally, Abubakar Mohamed, Hashim Magona, Omari Nyenje, Chunga Zito, Mohammed Saidi, Ayoub Lipati, Abdurahman Ally na Paul Bundara
 BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Monday, April 21, 2014

VPL YAMALIZIKA IKIWA NA CHANGAMOTO ZAKE AZAM IKITWAA UBINGWA HUO.



MSIMU wa VPL Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara umefikia tamatu jumamosi ya aprili 19 mwaka huu kwa Azam FC kutawazwa kuwa mabingwa wapya baada ya kumaliza na pointi 62 dhidi ya 56 za waliokuwa mabingwa watetezi, Yanga SC baada ya mechi zote 26.
 
Licha ya kuwa timu ya kwanza kuifunga Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine Aprili 13, mwaka huu,


Azam FC pia inakuwa timu ya kwanza nje ya Simba na Yanga kutwaa ubingwa wa Bara tangu mwaka 2000 Mtibwa Sugar ilipofanya hivyo
Azam inakuwa timu ya saba nje ya Si


mba SC kutwaa taji la Ligi Kuu, baada ya Cosmo mwaka 1967, Mseto mwaka 1975, Pan Africans mwaka 1982, Tukuyu Stars mwaka 1986, Coastal Union 1988 na Mtibwa Sugar mara mbili mfululizo 1999 na 2000.

Ashanti United ya Ilala, Dar es Salaam inayomaliza ligi na pointi 25, inaungana na JKT Oljoro ya Arusha iliyomaliza na pointi 19 na Rhino Rangers ya Tabora pointi 16 kuipa mkono wa kwaheri Ligi Kuu msimu wa 2013/2014 na nafasi zao kuchukuliwa na Ndanda FC ya Mtwara, Polisi ya Morogoro na Stand United ya Shinyanga zilizopanda kwa ajili ya msimu ujao. 

Mbali na Azam kumaliza kileleni na pointi 62, Yanga SC pointi 56 nafasi ya pili, Mbeya City ya Mbeya imemaliza nafasi ya tatu kwa pointi zake 49, Simba SC ya nne pointi 38, Kagera Sugar ya tano pointi 38 pia, Ruvu Shooting ya sita pointi 38, Mtibwa Sugar ya saba pointi 31, JKT Ruvu ya nane pointi 31 Coastal Union ya tisa pointi 29, Prisons ya 10 pointi  28 na JKT Mgambo ya 11 pointi 26. 
Huku tunahitimisha pazia la Ligi Kuu pamoja na kufurahia kufika salama, lakini ukweli ni kwamba kuna mapungufu mengi yaliyojitokeza ndani ya msimu huu ambayo yangeweza hata kusababisha athari kubwa.

Miongoni mwa hayo ni suala la uchezeshaji wa marefa, mfumo na muundo mzima wa ligi yetu ikiwa ni pamoja na kanuni kutozingatiwa, au kuwa na kanuni ambazo hazikidhi vigezo vya kimataifa.

Kanuni ya tano ya Ligi Kuu inasema kifungu cha (1) Uwanja wa nyumbani ni ule ul
iochaguliwa na timu husika na Uwanja wa ugenini ni ule ambao timu pinzani imekaribishwa kucheza.
Kifungu cha (2) Kutokana sababu za kiusalama au Uwanja, kutofikika au sababu nyingine yeyote ya msingi, TFF kwa kushauriana na timu husika, endapo timu yoyote haina Uwanja wa nyumbani unaofaa kwa mashindano ya Ligi, timu husika inaweza kuchagua kwa idhini ya TFF, Uwanja mwingine wowote, hata nje ya mji huo au Mkoa ili mradi Uwanja huo uwe jirani na mkoa wa timu husika ndani ya Tanzania Bara na uwe na sifa zinazokubalika,”.


Kuna tatizo katika kanuni hii, ukipitia kanuni nyingine nyingi duniani, zinaweka wazi kwamba timu itakuwa na Uwanja mmoja tu wa nyumbani, lakini kanuni hii ya ligi yetu imefumbwa na matokeo yake timu kama Ruvu Shooting, Mtibwa Sugar Azam FC na Prisons msimu huu zimetumia Uwanja zaidi ya mmoja wa nyumbani.
Ruvu, Mtibwa na Azam zimeruhusiwa kutumia viwanja vyao kwa mechi zote za Ligi Kuu isipokuwa zile zinazohusu Simba na Yanga, kwa sababu timu zote za Kariakoo, Dar es Salaam zina mashabiki wengi.   

WANACHAMA WA CLUB YA COASTAL UNION WATOA NENO KUHUSU UONGOZI WAO.


Coastal union  ambayo imemaliza Ligi Kuu Bara ikishika nafasi ya tisa na alama 29 ambapo ilikuwa sio matarajio ya wanachama wa club hiyo nao wametoa neno.
Wanachama ambao wa club hiyo kutoka jiji la Tanga walitoa ujumbe kwa uongozi wao wakionyesha kupinga mambo kadhaa yanayoonekana kutokwenda sawa.
Lakini kilichoonyesha kweli mambo hayo hayako vizuri ni wachezaji kwenda kuwaunga mkono wanachama hao mara baada ya mechi hiyo kwisha.
Uongozi wa Coastal Union, umekuwa ukishutumiwa kukataa kutoa kadi mpya za wachama, huku Kassim El Siagi ambaye ni katibu mkuu akielezwa kuwa chanzo.
Siagi amekuwa akisisitiza kwamba lazima kabla ya kuwakubali wanachama wapya, basi wawahakiki kwanza kwa kuwajadili.
Lakini katiba ya Coastal Union haina kipengele hicho.

Saturday, April 19, 2014

ASHANT,JKT OLJORO, RHINO RANGERS MKONO WA KWAHERI ZASHUKA DARAJA



Ligi kuu Vodacom Tanzania bara leo imefikia tamati baada ya timu zote kusha dimbani katika viwanja saba hapa nchini ambapo Azam FC imekabidhiwa Kombe lao huko Azam Complex, Chamazi mara baada ya Mechi yao ya kukamilisha Ratiba ambayo waliifunga JKT Ruvu Bao 1-0.
Kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam, Watani wa Jadi, Yanga na Simba nao walikutana kwenye Dabi ya Kariakoo, isiyokuwa na maan
a yeyote mbali ya kukamilisha Ratiba, na kutoka Sare ya Bao 1-1.
Kwenye Mechi hiyo, iliyohudhuriwa na Watazamaji wachache tofauti na desturi, Simba walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 76 Mfungaji akiwa Haruna Chanongo na Yanga kusawazisha kwa Bao la Dakika ya 86 la Simon Msuva.
Mechi pekee iliyokuwa na umuhimu mkubwa ni ile iliyochezwa Uwanja wa Jamhri huko Morogoro kati ya Tanzania Prisons na Ashanti United na Prisons kuifunga Ashanti Bao 1-0 na wao kupona na kuishusha Daraja Ashanti ambao wa
naungana na JKT Oljoro na Rhino Rangers kuporomoka Daraja.
VPL, LIGI KUU VODACOM
Mechi za mwisho za Ligi
Ratiba/Matokeo:
Jumamosi Aprili 19
Rhino Rangers v Ruvu Shooting [Ali Hassan Mwinyi, Tabora]
Mbeya City 1 Mgambo JKT 0 [Sokoine, Mbeya]
Tanzania Prisons 1 Ashanti United 0 [Jamhuri, Morogoro]
JKT Ruvu 0 Azam FC [Azam 1 Complex, Chamazi]
JKT Oljoro 1 Mtibwa Sugar 1 [Sheikh Amri Abeid, Arusha]
Coastal Union 0 Kagera Sugar 1 [Mkwakwani, Tanga]
Yanga 1 Simba 1 [National Stadium, Dar es Salaam]
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Azam FC
26
18
8
0
51
15
36
62
2
Young Africans
26
16
8
2
61
19
42
56
3
Mbeya City
26
13
10
3
33
20
13
49
4
Simba SC
26
9
11
6
41
27
14
38
5
Kagera Sugar
26
9
11
6
23
20
3
38
6
Ruvu Shooting
25
9
8
8
26
32
-6
35
7
Mtibwa Sugar
26
7
10
9
30
31
-1
31
8
JKT Ruvu
26
10
1
15
23
40
-17
31
9
Coastal Union
26
6
11
9
17
20
-3
29
10
Mgambo JKT
26
6
8
12
18
35
-17
26
11
Tanzania Prisons
26
6
10
10
26
33
-7
28
12
Ashanti United
26
6
7
13
20
39
-19
25
13
JKT Oljoro
26
3
10
13
19
37
-18
19
14
Rhino Rangers
25
3
7
15
18
37
-19
16