Saturday, June 22, 2013

ACCELOTT MTAZAMA ROONEY KWA JICHO LA TATU ZAIDI"

Carlo Ancelott ambaye kwa sasa ni kocha mpya wa Real Madrid, katika moja ya harakati zak ni kumsajili Wayne Rooney majira haya ya joto kama mshambuliaji huyo asiye na furaha atashindwa kumaliza tofauti zake na Manchester United.
Katika hali ya kawaida tunafahamu kabisa Rooney anapenda zaidi kuungana na Jose Mourinho ndani ya Chelsea ikiwa atamaliza miaka yake tisa ya kuishi United, lakini Madrid itakuwa na nafasi kubwa ya kumsajili mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ikiwa ataondoka.
Klabu zote  hizi mbili zina uwezo sana tu wa kulipa Pauni Milioni 30 za ada ya uhamisho wake na kumlipa mchezaji mwenyewe mshahara wa Pauni 250,000 kwa wiki.

Kocha wa zamani wa Chelsea, Ancelotti anatarajiwa kuthibitishwa kuwa mrithi wa Mourinho Jumatatu na atakabidhiwa orodha ya wachezaji wanaotakiwa, wakiwemo Rooney, Gareth Bale, Edinson Cavani na Luis Suarez.
Rooney, ambaye amebakiza miaka miwili katika Mkataba wake, atakuwa na mazungumzo na kocha mpya wa United, David Moyes baada ya wote kurejea baada ya wote kurejea kutoka mapumzikoni siku chache zijazo, lakini inaonekana kama atabadilisha mawazo yake juu ya kwenda kuanza maisha mapya. 
Wakati huo huo, kocha wa zamani wa Ufaransa, Laurent Blanc anajiandaa kurithi mikoba ya Ancelotti ya ukocha wa Paris Saint-Germain.

Baada ya mpango wa mabingwa hao wa Ufaransa kumchukua kocha wa zamani wa England, Fabio Capello kukwama, sasa beki wa zamani wa Manchester United, Blanc, mwenye umri wa miaka 47 atapewa mikoba

Makubaliano Kati ya Laurent Blanc na Paris St Germain  yamefikiwa leo yeye kuwa kocha mpya wa klabu ya Jiji  hapa ni kwa mujibu wa ripoti zilizotolewa.
Makubaliano baina ya kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa na PSG yamekubaliwa kwa miaka miwili. Ilipangwa kwamba, atasaini Mkataba wiki ijayo,