Friday, June 7, 2013

JOSE MOURINHO AJA NA KASI MPYA NA NGUVU MPYA KATIKA USAJILI".

Baada ya kukabidhiwa bikoba kwa mara ya pili ndani ya Chelsea jose mourinho amekuja kasi mapya ya kutafuta  washambuliaji kikosini hapo baada ya jana usiku kuanza mazungumzo na mchezaji mwenye thamani ya Pauni Milioni 50, Edinson Cavani wa Napoli, saa kadhaa baada ya kutoa ofa ya Pauni ya Milioni 34.9 kumnasa mshambuliaji wa Zenit St Petersburg, Hulk.
Kocha Mourinho ameorodhesha wachezaji wanne anaowataka wakiwemo kutoka Fiorentina, Stevan Jovetic na Manchester City, Edin Dzeko katika orodha hiyo.
Interest: Napoli have opened talks with Chelsea over Uruguay striker Edinson Cavani (left)
Napoli imeanza mazungumzo na Chelsea kuhusu mshambuliaji wa Uruguay, Edinson Cavani (kushoto)
Mourinho ameweka wzi na kuamini kuwa atamsajili mchezaji wa Pauni Milioni 25, Jovetic na kuwapiku Juventus, lakini anakabiliwa na ushindani kutoka klabu yake ya zamani, Real Madrid katika kuwania saini ya Cavani wakati Dzeko anaonekana kuwa mboni mbadala. Napoli haijakataa mpango wa kubadilishana Cavani na Dzeko na Manchester City, lakini mpango unaonekana kusinzia.
Rais wa Napoli, Aurelio de Laurentiis alisema jana usiku: "Kuna dhamira kutoka Chelsea kwa Cavani, watanipigia mimi saa chache zijazo. Nitafurahi akibaki, lakini ikiwa ataondoka atampata mbadala wake,".
Mshambuliaji wa Brazil, Hulk pia amethibitisha Mourinho anamtaka Stamford Bridge.
Target: Chelsea have made a £35m offer for Zenit St Petersburg's Brazilian forward Hulk
Chelsea imetoa ofa ya Pauni Milioni 35 kwa Zenit St Petersburg juu ya Mbrazil, Hulk.