Friday, August 16, 2013

SUAREZ ARUDI NYUMBANI ANFIELD BAADA YA MISUKOSUKO YA HAPA NA PALE YA KUTAKA KUONDOKA"

Mshambuliaji nyota Luis Suárez leo amerudi kikosini huko Anfield na kuanza Mazoezi tena pamoja na Kikosi cha Kwanza cha Timu ya Liverpool baada ya kuzuiwa kufanya hivyo na Meneja Brendan Rodgers kwa kuishambulia Klabu kwa madai ya kuvunja ahadi ya kumruhusu ahame ikiwa haitafuzu kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu huu.
Jumanne iliyopita Suarez alilazimishwa kufanya Mazoezi peke yake na kutakiwa kuiomba Klabu radhi kwa kauli zake na inaaminika Mchezaji huyo ametii amri hiyo na ndio maana amerudishwa tena Mazoezini kwenye Kikosi cha Kwanza.
Suarez amekuwa akisinikiza kuihama Liverpool na Arsenal ilishatoa Ofa ya Pauni 40,000,001 kumnunua lakini Liverpool imekataa na kusisitiza Mchezaji huyo hauzwi.
Msimamo huo ulisisitizwa zaidi na Mmiliki mkuu wa Liverpool kutoka Marekani, John W Henry, ambae Wiki iliyopita alitamka Suarez hatauzwa kwa Arsenal au kwa Klabu yeyote Ulaya.
Kwa sasa Suarez yupo kwenye Kifungo cha Mechi 10 alichopewa mwishoni mwa Msimu uliokwisha Mwezi Mei kwa kumng’ata meno Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic kwenye Mechi na tayari ameshatumuikia Mechi 4 na bado 6.
Wakati huo huo, Liverpool imefanikiwa kukubaliana na Klabu ya Spain, Valencia, ili kumchukua Beki wao wa kushoto Aly Cissokho kwa Mkopo wa Msimu mmoja.
Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers alikuwa akisaka Mchezaji wa pozisheni hiyo ili kuleta ushindani kwa Beki wake José Enrique na waliwahi kuwawania Lorenzo Melgarejo wa Benfica na Guilherme Siqueira wa Granada ili kujaza Nafasi hiyo.