TIMU ya Kandanda ya wilaya ya Korogwe leo imetawadhwa kuwa mabingwa wapya wa Mashindano ya Vijana ya Copa Coca Cola ngazi ya mkoa baada ya kufanikiwa kuitandika Muheza mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa uwanja wa Mkwakwani mjini hapa.
Mchezo
huo ambao ulianza majira ya saa nane mchana ulikuwa mkali na wenye
upinzani wa hali ya juu kutokana na timu zote kushambuliana kwa zamu na
kuonyesha kandanda nzuri na la kuvutia ambapo hadi timu zote zinakwenda
mapumziko,Korogwe walikuwa wakiongoza bao 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo timu zote ziliingia uwanjani hapo zikiwa na hari ya mchezo baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake.
Mabao ya Korogwe yalifungwa na Erick Msagati ambaye alipachika mabao yote kwenye mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo timu zote ziliingia uwanjani hapo zikiwa na hari ya mchezo baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake.
Mabao ya Korogwe yalifungwa na Erick Msagati ambaye alipachika mabao yote kwenye mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake.