Saturday, February 15, 2014

FA CUP: LEO JUMAMOSI NI MAN CITY v CHELSEA!!

FA_CUP_2013-2014FA CUP
Raundi ya Tano
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumamosi Februari 15
15:45 Sunderland v Southampton
18:00 Cardiff v Wigan
18:00 Sheff Wed v Charlton
20:15 Man City v Chelsea
Jumapili Februari 16
16:30 Everton v Swansea
18:00 Sheff Utd v Nottm Forest
19:00 Arsenal v Liverpool
Jumatatu Februari 17
22:45 Brighton v Hull City

MANCHESTER CITY v CHELSEA
Kuelekea Mechi ya leo Tunakumbuka Wiki ziliyopita, kwenye Mechi ya Ligi iliyochezwa Etihad, Chelsea waliifunga Man City Bao 1-0 na kwenye FA CUP wameshakutana mara 4 na City kufungwa mara ya kwanza, Mwaka 1915, lakini wameshinda mara zote 3 zilizobakia ikiwemo mara ya mwisho Msimu uliopita walipoifunga Chelsea 2-1 kwenye Nusu Fainali.
Man City hawajashinda katika Mechi zao mbili zilizopita, wakifungwa moja na Sare moja, lakini Chelsea hawajafungwa katika Mechi zao 12 zilizopita wakishinda 9 na Sare 3.

ARSENAL VS LIVERPOOL KESHO FEB16
Hapa kazi ipo itakuwa  FA CUP yenye upinzani kutokana Arsenal watataka kulipa kisasi cha Jumamosi iliyopita kunyukwa Bao 5-1 huko Anfield kwenye Mechi ya Ligi.
Kwenye FA CUP, Timu hizi zimekuwa zikukutana kila Msimu katika Misimu 12 iliyopita na Arsenal kushinda mara 7, zikiwemo Fainali 2, na Liverpool  kushinda Fainali 1 na kusonga mara 4 mbele ya Arsenal.
Katika Mechi za FA CUP 8 zilizopita , Arsenal wamefungwa moja tu na Liverpool na hiyo ilikuwa kwenye Fainali ya 2001.
Katika Mechi 12 zilizopita wakicheza kwao Emirates, Arsenal hawajafungwa hata Bao moja kati Mechi 11.
Liverpool hawajafungwa katika Mechi 9 zilizopita wakishinda 7 na Sare 2.