Saturday, February 15, 2014

YANGA KUTUPA KARATA LEO VS KOMOROZINE.


YANGA SC Mabingwa wa Tanzania Bara, jioni ya leo wanashuka dimbani kucheza mechi yao ya mwisho ya Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji Komorozine mjini Moroni.
Katika me

chi ya kwanza Yanga SC walishinda mabao 7-0 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Wacomoro Dar es Salaam Jumapili na leo wanatakiwa kumalizia vyema kazi yao dhidi ya timu hiyo dhaifu.
Endapo Yanga SC itafanikiwa kukamilisha vyema matokeo ya Randi ya Awali, basi itakutana na mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misiri katika Raundi ya Kwanza.