Wednesday, February 5, 2014

OKWI ATINGA KAMBINI BAGAMOYO

Mshambuliajih hatari Emmanuel Okwi amejiunga na kambi ya Yanga mjini Bagamoyo.
Okwi ambaye usajili wake umesimamishwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ameanza mazoezi na wenzake.

Akizungumza na mkali wa dimba Okwi amesema ameanza mazoezi na wenzake baada ya kufanya pekee kwa zaidi ya wiki.

TFF imesimamisha usajili wake kwa madai kwamba kuna kesi tatu za msingi ambazo ni Simba kuishitaki Etoile du Sahel ikitaka kulipwa dola 300,000, Okwi kuishitaki timu hiyo na yenye pia imemshitaki Fifa.
Okwi alikuwa jukwaani akiishuhudia Yanga ikivunja mwisho wa msimu kwa kuifunga Mbeya City bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.