Sunday, February 2, 2014

AZAM YAITANDIKA KAGERA, YAKAA KILELENI!

Ligi kuu Vodacom Tanzania bara imeendelea leo Jijini Dar es Salaama ambapo Mechi mbili zimepigwa zikihusisha Timu 3 za juu na Azam FC kubaki kileleni baada kuinyuka Kagera Sugara Bao 4-0 huko Azam Complez, Chamazi na Yanga kuipa kipigo cha kwanza kwenye Ligi Mbeya City na kubaki Nafasi ya Pili.
YANGA 1 MBEYA CITY 0
Goli la Dakika ya 16 la Supastraika, Mrisho Ngassa, liliwashushia Mbeya City kipigo cha kwanza kwenye Ligi na kuifanya Yanga izidi kujichimbia Nafasi ya Pili ikiwa Pointi 1 nyuma ya Azam FC.
Mbeya City, ambao walipigana kiume, walipata pigo mara tu baada Kipindi cha Pili kuanza baada ya Mchezaji wao Steven Mazanda kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
AZAM FC 4 KAGERA SUGAR 0
Huko Azam Complex, Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salamm, Wenyeji na Vinara wa VPL, Azam FC, waliendelea kukaa kileleni baada kuinyuka Kager Sugar Bao 4-0.
Bao za Azam FC zilifungwa na Brian Umony, Bao mbili, na nyingine kupitia Jabir Aziz Stima na Kevin Friday.
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano  Februari 5
Tanzania Prisons vs Coastal Union (Uwanja wa Sokoine, Mbeya)
Mgambo Shooting vs Ruvu Shooting (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga)
Rhino Rangers vs Oljoro JKT (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora)
JKT Ruvu vs Ashanti United (Uwanja wa Azam Complex, Chamazi)


MSIMAMO:
NO
TEAMS
P
W
D
L
GF
GA
GD
PTS
1
Azam FC
16
10
6
0
29
10
19
36
2
Young Africans
16
10
5
1
34
12
22
35
3
Mbeya City
16
8
7
1
22
13
9
31
4
Simba SC
15
8
6
1
31
13
18
30
5
Mtibwa Sugar
15
5
6
4
19
18
1
21
6
Kagera Sugar
16
5
6
5
15
15
0
21
7
Coastal Union
15
3
9
3
11
8
3
18
8
Ruvu Shootings
14
4
6
4
16
16
0
18
9
JKT Ruvu
14
6
0
8
13
18
-5
18
10
Rhino Rangers
15
2
5
8
9
18
-9
11
11
JKT Oljoro
15
2
5
8
10
15
-5
11
12
Ashanti United
15
2
4
9
13
28
-15
10
13
Tanzania Prisons
13
1
6
6
6
16
-10
9
14
Mgambo JKT
15
2
3
10
7
26
-19
9