Timu
ya Taifa ya Malawi (Flames) inatarajiwa kuwasili nchini Mei 1 mwaka huu
kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Mei 4
mwaka huu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ikiwa chini ya Kocha
mpya, Mart Nooij tayari ipo jijini Mbeya kujiwinda kwa mechi hiyo ikiwa
ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mashindano dhidi ya Zimbabwe
itakayochezwa jijini Dar es Salaam kati ya Mei 16 na 18 mwaka huu.