Tuesday, April 29, 2014

KAVUMBAGU ATUA AZAM KWA MKATABA WA MWAKA MMOJA.

Mshambuliaji Didier Kavumbagu mchana wa leo amesaini mkataba wa mwaka mmoja na mabingwa wapya wa ligi kuu soka Tanzania bara, klabu ya Azam fc.
Mtandao wa Mkali wa dimba tz umafanikiwa kuthibitisha Taarifa hii kwa afisa habari wa  Azam fc, wana Lambalamba, Jafari iddi maganga 
Maganga amesema Kavumbagu tumem
alizana nae na amesaini rasmi mkataba wa mwaka mmoja, hivyo basi tutakuwa nae msimu ujao kwenye kampeni ya kutetea ubingwa wetu pamoja na michuano ya klabu bingwa ya Afrika.
Kavumbagu ambae ni Mshambuliaji mahiri na nahodha wa timu ya Taifa ya Burundi ameamua kumwaga wino Azam baada ya Uongozi wa Yanga kusuasua kumpa mkataba mwingine baada ya ule wa miaka miwili kumalizika.
Maganga amesema kuwa lengo la kuanza usaji mapema ni kuweka mipango mathubuti katika kuhakikisha azam fc inakuwa timu bora na kuweza kukiweka imara kikosi hicho katika msimu ujao pamoja na ligi ya mabingwa barani africa