Kamati ya uchaguzi ya Simba
imepanga uchaguzi mkuu wa klabu hiyo kufanyika juni 29 mwaka huu baada
ya msajili wa vyama vya michezo na klabu kuipitisha katiba yao
iliyofanyiwa marekebisho.

“Kamati yangu ina watu makini na wenye uadilifu mkubwa. Pia wana mawazo ya kuijenga klabu ya Simba”.
“Jana tulikutana na kupanga
ratiba ya uchaguzi. Hatutakuwa na huruma na watu watakaoenda kinyume na
kanuni za uchaguzi”. Alisema Ndumbaro.
Ndumbaro
alisema kuanzia mei 9 mwaka huu mchakato wa kuanza kutoa fomu kwa watu
wenye nia ya kuwania nafasi za uongozi utaanza rasmi, na siku ya
kurudisha fomu ni mei 14 mwaka huu.