Saturday, June 7, 2014

MASHABIKI WA YANGA MBEYA WAUTAKA UONGOZI WA YANGA KUMUELEZA MAXIMO KUZIBA PENGO LA KAVUMBAGU

Mashabiki na wadau wa soka mkoani mbeya wameutaka Uongozi wa Yanga sc kuhusu wameutaka uongozi huo kupendekeza kumweleza kocha mpya anayetarajiwa kuja kuinoa yanga kocha Marcio Maximo kumpata mshambuliaji mahiri wa kuziba nafasi ya Didier Kavumbagu, kabla ya kuanza kukinoa kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi ya Tanzania Bara.

Wakizungumza na mtandano wa mkali wa dimba kupitia sayari ya michezo wames
ema kuwa kutokana habari zilizo tolewa katika Mkutano Mkuu wa marekebisho ya baadhi ya vipengele kwenye Katiba ya Yanga umefanyika na kumalizika salama na furaha kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi -Oysterbay huku wanachama wakipitisha kipengele cha kuundwa kwa kamati ya maadili.
katika kikao cha wanachama wa club ya yanga kilicho fanyika Juni 1 mwaka huu uongozi wa yanga Ulimtangaza kuwa Maximo kama kocha anayetarajiwa kuinoa Yanga.

Wamesema kuwa Maximo anatakiwa kutazama mchezaji sahihi atakae ziba pengo la mshambuliaji Didier Kavumbagu kwa ajili ya kuunda upya timu hiyo licha ya kuwa na Wachezaji wengi katika safu ya Ushambuliaji.
 Kwa mujibu wa chanzo cha karibu kutoka ndani ya yanga Taarifa zinasema mazungumzo na Kocha Maximo yamefikia sehemu nzuri kwa ajili ya kuja Tanzania kuinoa Yanga SC.