Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) limepokea kwa masikiti
ko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Simba na
Taifa Stars, Gebo Peter kilichotokea usiku wa kuamkia leo (Juni 6 mwaka huu)
katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa katika familia ya
mpira wa miguu nchini kwani, Gebo enzi za uhai wake alitoa mchango mkubwa akiwa
mchezaji na baadaye kiongozi katika timu ya Manyema ya jijini Dar es Salaam.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu
Gebo Peter, klabu ya Manyema na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam
(DRFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha
msiba huo mzito.
Msiba upo nyumbani kwao Vingunguti
karibu na Kanisa Katoliki ambapo taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na
familia.
Marehemu ambaye ameacha mjane na watoto
watatu anatarajiwa kuzikwa kesho (Juni 7 mwaka huu) nyumbani kwao Kigurunyembe,
mjini Morogoro.
Bwana
alitoa, na Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe. Amina