Wednesday, July 16, 2014

CHELSEA YAMNASA MBADALA WA COLE KUTOKA ATLETICO.

KLABU ya Atletico Madrid imetangaza kuwa imefikia makubaliano na Chelsea kuhusu uhamisho wa Filipe Luis. Chelsea kwa kipindi kirefu amekuwa wakihusishwa na kutaka kumsajili nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 huku mwezi Juni wakiipa taarifa Atletico kuwa wako tayari kutoa paundi milioni 20 zilizowekwa katika mkataba wake. Atletico wamethibitisha rasmi kuwa wameshakubaliano juu ya uhamisho huo na kilichobakia ni mchezaji huyo kufanyiwa vipimo vya afya na Chelsea. Luis anatarajiwa kuziba nafasi ya Ashley Cole aliyeruhusiwa kuondoka kwenda Roma kama mchezaji huru kufuatia kumalizika kwa mkataba wake. Beki huyo wa kushoto atajiunga na mchezaji mwenzake Diego Costa ambaye naye alikamilisha usajili wake kutoka Atletico uliogharimu kiasi cha paundi milioni 35 mapema wiki hii. Luis anakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Chelsea katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi baada ya kusajiliwa kwa Costa, Cesc Fabregas na kiungo chipukizi Mario Pasalic.