Wednesday, July 16, 2014

NBA: DENG AENDA KUZIBA PENGO LA LEBRON JAMES.

MCHEZAJI nyota wa mpira wa kikapu kutoka nchini Uingereza, Luol Deng amejiunga na timu ya Miami Heat kama mchezaji huru. Deng ambaye amezichezea timu za Cleveland Cavaliers na Chicago Bulls msimu
uliopita anatarajiwa kuchukua nafasi ya LeBron James ambaye amehamia Cavaliers wiki iliyopita. Rais wa Heat, Pat Riley amesema Deng ni mmoja ya mchezaji muhimu waliomsajili katika historia ya timu hiyo. Deng ambaye ni mzaliwa wa Sudan aliiwakilisha Bulls kutoka mwaka 2004 mpaka 2014 na mara mbili amefanikiwa kuchaguliwa katika kikosi cha wachezaji nyota wa mchezo huo nchini Marekani, aliuzwa Cavaliers Januari mwaka huu. Heat wamefanikiwa kutinga fainali nne zilizopita za Ligi Kuu ya Mpira wa Kikapu nchini Marekani-NBA ambapo walishinda mwaka 2012 na 2013 lakini walichapwa na San Antonio Spurs msimu uliopita.