Mabingwa wa tanzania bara 2013-2014
azam fc imekamilisha hayau ya makundi imemaliza katika klabu Bingwa Afrika
Mashariki na Kati, Kombe la Kagame baada ya kuichalaza mabao 4-1 Adama City ya
Ethiopia Uwanja wa Nyamirambo mjini hapa.
Kwa matokeo hayo Azam FC ya Tanzania Bara, imekwea kileleni mwa Kundi A kwa kufikisha pointi nane baada ya mechi nne, ikishinda mbili na sare mbili na hatimaye kutinga hatua ya bRobo Fainali.
Dakika 45 za kwanza zilimalizika
timu hizo zikiwa zimefungana bao 1-1, Azam wakitangulia kupitia kwa Nahodha
John Bocco ‘Adebayor’ akiunganisha krosi ya Khamis Mcha ‘Vialli’ kabla ya
Desaleny Debesh kuisawazishia Adama dakika ya 39.
Refa Mohamed Hassan kutoka Somalia alikataa bao la Kipre Herman Tchetche dakika ya 42, akidai kipa alibughudhiwa na kipindi cha pili Azam iliingia na moto mkali na kufanikiwa kuongeza mabao matatu.
Kocha Mcameroon Joseph Marous Omog alifurahia matokeo hayo na akasema sasa anajipanga kwa Robo Fainali.
Kikosi cha Azam FC; Mwadini Ali, Erasto Nyoni, Gardiel Michael/Said Mourad dk51, David Mwantika, Aggrey Morris, Kipre Balou, Khamis Mcha ‘Vialli’/Farid Mussa dk61, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Mudathir Yahya dk72, John Bocco ‘Adebayor’, Didier Kavumbangu na Kipre Tchetche.