Saturday, August 16, 2014

MAXIMO ATOA NENO KWA PATRIC PHIRI KUHUSU VPL SEPT 20

Mbrazil Marcio Maximo Kocha Mkuu wa klabu Yanga ametoa ya moyoni kwa kumkaribisha nchini kocha wa Simba Timu pinzani wa jadi, Mzambia, Patrik Phiri aliyetua hivi karibuni na kuanza kazi ya kukinoa kikosi cha Wanamsimbazi.
Maximo alichukua nafasi ya Mholanzi, Hans van Der Pluijm huku Phiri akiwa amesaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumikia Simba baada ya kuchukua mikoba iliyoachwa na  Mcroatia, Zdravko Logarusic aliyetimuliwa Jumapili iliyopita.
Katikamkutano na waandishi wa habari, Maximo amesema kuwa amemkaribisha kocha huyo ambaye anafahamu kuwa ni mzuri lakini amemtaka kutambua ushindani uliopo wa ligi ya Tanzania.
Maximo amesema napenda kumwambia kocha mpya wa Simba (Patrick Phiri),  karibu Tanzania lakini ajue kuwa ligi ina ushindani wa hali ya juu japo natambua kuwa yeye ni kocha mzuri na anayeifahamu ligi ya hapa”, alisema Maximo.
Phiri ametua nchini siku chache zilizopita na kusaini mkataba wa mwaka
mmoja kuinoa Simba, hii ikiwa ni mara ya tatu tofauti kuionoa timu hiyo.
Kwa upande mwingine, Maximo alisema kuwa kikosi chake kinaendelea vizuri na mazoezi ambapo kinamchanganyiko wa vijana na wakongwe ambao wengine walikuwa kwenye timu zao za Taifa.
Maximo aliongeza kuwa beki aliyesajiliwa na timu hiyo, Edward Charles ni mchezaji mzuri anayeamini ataisaidia Yanga kwa muda mrefu kutokana na umri  wake kuwa mdogo.
Maximo anatarajia kutaja majina ya wachezaji ataokwenda nao kwenye kambi kisiwani Pemba na watakaa huko kwa takribani siku kumi na baadae kurudi Dar tayari kwa kuanza msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.