Wekundu wa Msimbazi Simba Sc imekamilisha mechi zake za kirafiki za kujipima nguvu katika kambi yake ya Afrika kwa kufungwa mabao 2-0 na Jomo Cosmos mjini Johannesburg jioni hii.
Pamoja na kufungwa na timu hiyo ya Daraja la Kwanza, inayomilikiwa na kufundishwa na gwiji wa soka Afrika Kusini, Jomo ‘Black Prince’ Sono, Simba SC ilicheza soka ya kuvutia.

Katika mchezo wake wa kwanza, Simba SC ililazimishwa sare ya bila kufungana na Orlando Pirates kabla ya kufungwa mabao 4-2 na Bidvest Wits, au Wits University.
Simba SC itaendelea na mazoezi kesho na inatarajiwa kurejea Dar es Salaam Ijumaa tayari kwa mchezo wa Jumamosi, unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini.