Wednesday, November 26, 2014

ASKARI POLISI WILAYA CHUNYA ATIWA NGUVUNI KWA TUHUMA ZA MAUAJI.

ASKARI polisi wa kitengo cha usalama barabarani Wilayani Chunya Mkoani Mbeya, PC  Zeferin Didas Focas mwenye umri wa miaka (34) amefukuzwa kazi kwa tuhuma za kuhusika na mauji ya raia Abisai Wadi mwenye miaka 22.
Kamanda wa polisi Mkoani Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kufukwa kazi kwa askari huyo baada ya husika na mauji ya raia huyo yaliyotokea  katika Kata ya Igalula barabara ya Itindi Mkwajuni  Wilayani Chunya Mkoani Mbeya.
Amesema,  askari huyo akiwa na mwezie aliisimamisha pikipiki iliyokuwa imempakia abiria nyuma ambapo dereva huyo alikaidi, ndipo askari huyo alichukua jiwe na kuitupia pikipiki hiyo iliyokuwa katika mwendo kasi  na kumpata abiria huyo.
Amesema, jiwe hilo linasemekana lilimkuta abiria aliyepakizwa kwenye poikipiki hiyo lakini haikuwekwa wazi kwamba jiwe hilo lilimpata katika sehemu ipi ya mwili wa marehemu huyo.

Amesema, askari huyo ambaye kwa sasa anatambulika kwa namba ya X6710 anatarajiwa kufikishwa mahakamani  ili kujibu tuhuma za mauji zinazomkabili mbele yake.