JUMLA ya shilingi
bilioni tano zimetolewa na serikali
kama kianzio cha ujenzi wa jengo la upasuaji ujenzi wa maabara pamoja na kununua dawa
katika hospitali teule ya rufaa ya Tumbi
mkoani Pwani.
Kauli hiyo ya serikali
imetolewa na naibu waziri ofisi ya waziri mkuu Aggrey Mwanri mjini Dodoma
katika kipindi cha maswali na majibu ambapo amekiri kuwa miundombinu ya
hospitali hiyo haiendani na mahitaji yaliyopo.
Amesema kuwa ili kukabiliana
na hali hiyo serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya
upanuzi wa hospitali hiyo, ambapo inakadiriwa shilingi bilioni 30 zilitumika
kwa ajili ya shughuli za ujenzi huo kwa mwaka 2010.