Thursday, November 6, 2014

JESHI LA POLISI MBEYA LAMSHIKILIA MTU MMOJA KWA KUUZA NYAMA YA MBWA

KATIKA tukio la kushangaza mwanaume mmoja amekamatwa na polisi wilaya ya Kyela mkoa wa Mbeya kwa tuhuma za kuuza nyama ya Mbwa.
Mtuhumiwa huyo amefahamika kwa jina la Ahad Jesikaka mwenye umri wa miaka 20, mkazi wa kijiji cha Ngyekye, kata ya Matema, wilayani humo.
Akithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi amesema kuwa amewauzia kitoweo hicho watu wawili.
Amewataja walionunua nyama hiyo ni Enock Nsemwa mwenye miaka 25, na Anyandile Mbwilo mwenye umri wa miaka 29, wote wakazi wa Ngyekye.
Hata hivyo anatoa wito kwa jamii kuwa makini hususuni wanaponunua vyakula ili kujiepusha na madhara ya kiafya.