Thursday, November 6, 2014

MESSI AFIKIA REKODI YA RAUL BAO 71 AMBWAGA RONALDO UEFA

Mshambuliaji Mahiri wa Argetina na Barcelona Lionel Messi amefanikiwa kuifikia rekodi ya nyota wa zamani wa Real Madrid katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Raul Gonzalenz alikuwa akishikilia rekodi ya kufunga mabao 71 na kuwa mfungaji mwenye mabao mengi zaidi kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Cristiano Ronaldo alionekana ndiye atakuwa wa kwanza kumfikia Raul,lakini mabao mawili aliyofunga Messi wakati Barcelona ikiichalaza Ajax magoli 2-0 kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, yamekwamisha ndoto za Ronaldo.
Wafungaji Bora: wa Kihistoria Uefa.
Lionel Messi: Magoli 71 Mechi 90-Barcelona.
Raul: Magoli 71 Mechi 142-Real Madrid na Shalke 04.
C'Ronaldo: Magoli 70 Mechi 107-Man united na R'Madrid
Ruud van Nistelrooy: Magoli 56 Mechi 73-Psv Eindhoven,Man U na R'Madrid.
Thierry Henry: Magoli 50 Mechi 112-Arsenal,Barca,Los angel marekani.