Monday, November 3, 2014

SUMATRA MKOA WA MBRYA YASEMA HATAVUMILIA TABIA ZA MADERA KUJAZA MAFUTA WAKATI WA KUBEBA ABIRIA.

MAMLAKA ya usafiri na udhibiti wa nchi kavu na majini (Sumatra) mkoa wa Mbeya imesema kuwa haitavumilia tabia ya baadhi ya watumiaji wa vyombo vya usafiri  kujaza mafuta  wakati vikiwa vimebeba abiria.
Aidha mamlaka hiyo imesisitiza kuwa ikiwa watumiaji hao watabainika kutenda kosa hilo watatozwa faini ya shilingi laki mbili na nusu.
Akizungumza na Highlands fm, Afisa mfawidhi wa Sumatra, Denis Daud amesema vitendo hivyo vinahatarisha usalama wa abiria na kwamba  mamlaka hiyo imekuwa ikitoa elimu kwa watumiaji hao.

Katika hatua nyingine Daud, amewataka watumiaji hao kujaza mafuta ya kutosha kwenye magari yao ili kuondoa usumbufu kwa abiria pindi magari hayo yanapokata mafuta barabarani.