Timu ya Mbeya City wagonganyundo wa jiji la mbeya ikiwa katika dimba la mkwakwani imepokea kipondo kingine baada ya kuchapwa mabao 2-1 na Mgambo JKT.
Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, washindi walipata mabao yote katika kipindi cha kwanza.
Mbeya City wakajitahidi kupata bao katika kipindi cha pili na kuzaa matokeo ya mabao 2-1 katika dakika 90.