Friday, May 3, 2013

25 WARIPOTI KAMBINI YOUNG TAIFA STARS

Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inakutana Mei 9 mwaka huu jijini Dar es Salaam kupokea na kupanga utekelezaji wa maagizo ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kuhusu uchaguzi wa shirikisho.

Kikao hicho cha dharura chini ya Uenyekiti wa Rais wa TFF, Leodegar Tenga kitakuwa na ajenda hiyo moja tu katika kuhakikisha utekelezaji wa maelekezo ya FIFA unafanyika haraka ili uchaguzi ufanyike ndani ya muda uliopangwa.

FIFA katika maelekezo yake imetaka kwanza ziundwe Kamati ya Maadili na Kamati ya Rufani ya Maadili kabla ya kuingia kwenye mchakato wa uchaguzi wa Kamati mpya ya Utendaji ya TFF. FIFA imeagiza uchaguzi uwe umefanyika kabla ya Oktoba 30 mwaka huu.

KILA LA KHERI AZAM KOMBE LA SHIRIKISHO
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaitakia kila la kheri timu ya Azam katika mechi yake ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika itakayochezwa Morocco kesho (Mei 4 mwaka huu).

Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya pili ya michuano hiyo itachezwa jijini Rabat kuanzia saa 11 jioni kwa saa za Morocco. Timu hizo zilitoka suluhu katika mechi ya kwanza iliyochezwa jijini Dar es Salaam wiki mbili zilizopita.

Azam iko nchini Morocco kwa karibu wiki nzima sasa ikijiandaa kwa mechi hiyo chini ya Kocha wake Stewart John Hall. Msafara wa Azam nchini humo unaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Eliud Mvella.

25 WARIPOTI KAMBINI YOUNG TAIFA STARS
Wachezaji 25 kati ya 30 walioitwa na Kocha Kim Poulsen kwenye kikosi cha pili cha Taifa Stars (Young Taifa Stars) wameripoti kambini ambapo mazoezi yalianza tangu jana jioni (Mei 2 mwaka huu).
Kocha Kim amewaitaka wachezaji katika kambi hiyo ya siku tano ili kuangalia uwezo wao katika maeneo kadhaa kwa lengo la kupata baadhi ambao anaweza kuwajumuisha kwenye kikosi cha Taifa Stars siku za usoni.

Wachezaji watano walioshindwa kujiunga katika kambi ya timu hiyo iliyoko hoteli ya Sapphire jijini Dar es Salaam ni Aishi Manula, David Mwantika, Himid Mao, Samih Nuhu na Seif Abdallah ambao wako Morocco na timu yao ya Azam.

KAMATI YA MASHINDANO KUPITIA MAANDALIZI RCL
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inakutana Jumapili (Mei 5 mwaka huu) kupitia maandalizi ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) iliyopangwa kuanza Mei 12 mwaka huu.

Tayari mikoa 18 kati ya 27 kimpira imeshapata mabingwa wao kwa ajili ya RCL itakayotoa timu tatu zitakazopanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao (2013/2014).

Kamati hiyo chini ya Uenyekiti wa Blassy Kiondo ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF itapokea taarifa ya maandalizi ya ligi hiyo kutoka Idara ya Mashindano ya TFF na kufanya uamuzi juu ya mikoa ambayo haijawasilisha mabingwa wao.

Ligi hiyo itachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini, na ratiba (draw) itapangwa wakati wowote. Ada ya kushiriki ligi hiyo kwa kila klabu ni sh. 100,000 na usajili utakaotumika na ule ule wa ligi ngazi ya mkoa. Hakutakuwa na usajili mpya wa wachezaji.

LALA SALAMA VPL KUENDELEA JUMAPILI
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea Jumapili (Mei 5 mwaka huu) kwa mechi moja kati ya Ruvu Shooting na Simba itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.15 jioni.

Hiyo itakuwa mechi ya raundi ya 24 kwa timu hizo ambapo Simba iko nafasi ya nne ikiwa na pointi 39 nyuma ya mabingwa Yanga wenye pointi 57, Azam yenye pointi 48 na Kagera Sugar ambayo ina pointi 40. Ruvu Shooting iko katika nafasi ya saba ikiwa na pointi 31.

Hadi sasa mabao 348 yameshafungwa katika ligi hiyo huku Yanga ikiongoza kwa kufunga 45. Polisi Morogoro yenye pointi 22 katika nafasi ya 12 ndiyo iliyofunga mabao machache ikiwa nayo 13 tu.

African Lyon yenye pointi 19 katika nafasi ya mwisho ndiyo inayoongoza kwa kuwa na kadi nyingi. Timu hiyo inayofundishwa na Charles Otieno ina kadi 44 ambapo kati ya hizo nne ni nyekundu. Mtibwa Sugar ya Manungu, Turiani mkoani Morogoro yenyewe inaongoza kwa kuwa na kadi nyingi nyekundu ambapo hadi sasa inazo saba.

YANGA, COASTAL UNION ZAINGIZA MIL 66
Mechi namba 172 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Coastal Union iliyochezwa juzi (Mei 1 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa timu hizo kutoka sare ya bao 1-1 imeingiza sh. 66,022,000.

Watazamaji 11,478 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 15,378,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 10,071,152.54.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 10,230 na kuingiza sh. 51,150,000 wakati idadi ndogo ya washabiki ilikuwa ya kiingilio cha sh. 20,000 kilichovutia washabiki 69 na kuingiza sh. 1,380,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,819,793.62, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 4,691,876.17, Kamati ya Ligi sh. 4,691,876.17, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,345,938.09 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,824,618.51.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Thursday, May 2, 2013

KUTOKUWEPO KWA MESSI NI BAHATI KWETU-JUPP


Bosi wa THE BAVARIANI klabu ya Bayern Munich, Jupp Heynckes anaamini kuwa kikosi chake kilipata bahati kwakuwa mshambuliaji nyota wa Barcelona Lionel Messi hakuwemo katika kikosi hicho kitendo ambacho kilipelekea timu hiyo kushinda kwa mabao 3-0 kwenye mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Camp Nou. Mshambuliaji huyo wa kimataifa alikuwa katika benchi akitizama mabao ya Arjen Robben, bao la kujifungala Gerard Pique na Thomas Muller yakiididimiza timu hiyo kwa jumla ya mabao 7-0 katika mechi mbili za nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya walizokutana. Wakati Heynckes akisifu umakini wa kikosi chake katika mechi hiyo ya marudiano lakini amekiri kuwa wapinzani wao walikuwa tofauti bila ya kuwepo nyota wao Messi. Kocha huyo amesema hakuna mtu aliyetegemea kuwa kikosi chake kingeibuka na ushindi wa mabao 7-0 katika mechi mbili walizokutana lakini pamoja na hivyo huwezi kusema zama za Barcelona zimekwisha kwasababu waliwakosa nyota wao wengi ambao ni majeruhi.
na kwa upande wake meneja wa klabu ya FC Barcelona, Tito Vilanova ametanabaisha kwamba majeruhi sio sababu ya kukosekana kwa mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Lionel Messi katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina aliwashangaza mashabiki wa timu hiyo baada ya kuondolewa katika kikosi kilichoanza dhidi ya Bayern huku wengi wakidhani majeruhi ya msuli wa paja ndio chanzo kikubwa cha kukosekana kwake. Hata hivyo kwa mujibu wa Vilanova majeruhi halikuwa tatizo la kumuacha Messi na kudai kuwa angeweza kumpa nafasi nyota huyo kuingia katika kipindi cha pili kama angedhani kikosi chake kilikuwa na nafasi ya kufika fainali. Vilanova amesema Messi hakuwa mgonjwa kama watu wanavyofikiri lakini alikuwa hajisikii vyema hivyo alifikiri kwamba kwa hali aliyokuwa nayo asingeweza kuisaidia timu hiyo kwa muda ule.

BIN KHALIFA AMETEULIWA KUWA MJUMBE WA FIFA
SHIRIKISHO la Soka barani Asia limemchagua Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Duniani-FIFA katika uchaguzi uliofanyika Malaysia. Al Khalifa ambaye ni raia wa Bahrain alifanikiwa kupata kura 28 katika kura 46 zilizopigwa ambapo alimshinda Hassan Al Thawadi wa Qatar aliyepata kura 18. Al Khalifa amewahi kuikosa nafasi hiyo ya juu kabisa ya maamuzi ya FIFA kwa kura chache baada ya kuzidiwa na aliyekuwa rais wa AFC Mohamed Bin Hammam kwa kura 23 kwa 21 mwaka 2009. AFC pia imemteua Al Khalifa kugombea nafasi ya urais wa shirikisho kwa kipindi kingine cha miaka miwili.

BALE ATEULIWA MCHEZAJI BORA NA WANAHABARI WA MICHEZO


Baada  Juzi kufanikiwa kutwaa Tuzo mbili za PFA, Professional Footballers' Association, za Mchezaji Bora wa Mwaka pamoja na Mchezaji Bora Kijana wa Mwaka Gareth Bale tena ameteuliwa kuwa Mchezaji Bora wa Mwaka na FWA, Football Writers' Association, na

Katika Msimu huu, Bale ameifungia Tottenham Mabao 19 katika mechi zake 29 za Ligi.
WASHINDI WALIOPITA WA FWA:
-2003: Thierry Henry
-2004: Thierry Henry
-2005: Frank Lampard
-2006: Thierry Henry
-2007: Cristiano Ronaldo
-2008: Cristiano Ronaldo
-2009: Steven Gerrard
-2010: Wayne Rooney
-2011: Scott Parker
-2012: Robin van Persie
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>


WASHINDI WALIOPITA WA TUZO MBILI PFA/
FWA KWA MPIGO:
-1980: Terry McDermott
-1983: Kenny Dalglish
-1984: Ian Rush
-1986: Gary Lineker
-1987: Clive Allen
-1988: John Barnes
-1998: Dennis Bergkamp
-1999: David Ginola
-2000: Roy Keane
-2001: Teddy Sheringham
-2003: Thierry Henry
-2004: Thierry Henry
-2007: Cristiano Ronaldo
-2008: Cristiano Ronaldo
-2010: Wayne Rooney
-2011: Robin van Persie
Kikosi cha Mwaka cha Ligi Kuu ya Uingereza ni hiki:
David de Gea (Manchester United), Pablo Zabaleta (Manchester City), 
Jan Vertonghen (Tottenham Hotspur), Rio Ferdinand (Manchester United),
 Leighton Baines (Everton), Michael Carrick (Manchester United), 
Juan Mata (Chelsea), Gareth Bale (Tottenham Hotspur),
 Luis Suarez (Liverpool), Eden Hazard (Chelsea),
 Robin van Persie (Manchester United).d), 
Juan Mata (Chelsea), Gareth Bale (Tottenham Hotspur),
 Luis Suarez (Liverpool), Eden Hazard (Chelsea), 
Robin van Persie (Manchester United).

RONALDINHO KATIKA ULIMWENGU WA SOKA

Ronaldinho
Taarifa kuhusu yeye
Full name
Ronaldo de Assis Moreira
Date of birth
21 March 1980 (age 33)
Place of birth
Height
1.83 m (6 ft 0 in)[1]
Playing position
Timu ya sasa
Current club
Number
10
Timu ya ujana
1987–1998
Timu ya wakubwa 
Years
Team
Mechi
(Goli
1998–2001
52
(21)
2001–2003
55
(17)
2003–2008
145
(70)
2008–2010
76
(20)
2011–2012
33
(15)
2012–
32
(9)
Timu ya taifa
1996
6
(2)
1999
5
(3)
2000–2008
27
(18)
1999–
96
(33)

CLUB MATAJI
Grêmio
·         South Cup (1): 1999
·         Rio Grande do Sul State Championship (1): 1999
Paris Saint-Germain
·         UEFA Intertoto Cup (1): 2001
Barcelona
·         La Liga (2): 2004–05, 2005–06
·         Supercopa de España (2): 2005, 2006
·         UEFA Champions League (1): 2005–06
AC Milan
·         Serie A (1): 2010–11
Flamengo
·         Taça Guanabara (1): 2011
·         Taça Rio (1): 2011
·         Campeonato Carioca (1): 2011


TIMU YA TAIFA Brazil

·         Copa América (1): 1999
·         FIFA World Cup (1): 2002
·         FIFA Confederations Cup (1): 2005
·         Superclásico de las Américas (1): 2011
Brazil U23
·         CONMEBOL Men Pre-Olympic Tournament (1): 1999
·         Olympic Bronze Medal (1): 2008
Brazil U17
·         FIFA U-17 World Championship (1): 1997
TUZO BINAFSI
1.Kombe la Shirikisho Golden boy : 1999
2. Kombe la Shirikisho la Golden ball: 1999
3.Rio Grande do Sul Hali michuano ya mfungaji bora: 1999
4. CONMEBOL Wanaume Kabla ya Olimpiki mashindano mfungaji bora: 2000
5. Kombe la Dunia All-Star Team: 2002
6.FIFA miaka 100
7. Balon di’o tuzo (2): 2003-04, 2005-06
8.La Liga Ibero-American Mchezaji wa Mwaka (1): 2004
9. FIFA World Mchezaji wa Mwaka (2): 2004, 2005
10.Ballon d'Or (1): 2005
11. FIFPro World Mchezaji wa Mwaka (2): 2005, 2006
12. UEFA mfungaji bora wa club (1): 2004-05
13. UEFA Club Mchezaji wa Mwaka (1): 2005-06
14.UEFA Timu ya Mwaka (3): 2003-04, 2004-05, 2005-06
15.FIFPro World XI (3): 2004-05, 2005-06, 2006-07
16 Golden mfungaji bora (1): 2009

EUROPA LIGI-NUSU FAINALI: JE LEO CHELSEA KUTINGA FAINALI

[Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 5 Usiku, Bongo Taimu]

MARUDIANO
Alhamisi Mei 2
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Benfica v Fenerbahce [0-1]
Chelsea v FC Basel [1-2]
FAINALI
AMSTERDAM ARENA
MEI 15
Benfica/Fenerbahce v Chelsea/FC Basel 
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
FAINALI WATOTO WA BABA MMOJA
RATIBA/MATOKEO:
MARUDIANO
Jumanne Aprili 30
[Kwenye Mabano Jumla Magoli Mechi 2]
Real Madrid 2 Borussia Dortmund 0 [3-4]
Jumatano Mei 1
Barcelona 0 Bayern Munich 3 [0-7]
MAGOLI:
Barcelona 0
Bayern Munich 3
-Arjen Robben Dakika ya 32
-Pique 72 [Kajifunga Mwenyewe]
-Thomas Mueller 76
FAINALI
25 Mei 2013
UWANJA wa WEMBLEY, London.
Borrussia Dortmund v Bayern Munich