MATOKEO BPL LEO England - Premier League (Table) | |||
18:18 | May 19 | ||
FT | Chelsea | 2 - 1 | Everton |
FT | Liverpool | 1 - 0 | Queens Park R. |
FT | Manchester C. | 2 - 3 | Norwich C. |
FT | Newcastle U. | 0 - 1 | Arsenal |
FT | Southampton | 1 - 1 | Stoke C. |
FT | Swansea C. | 0 - 3 | Fulham |
FT | Tottenham H. | 1 - 0 | Sunderland |
FT | West Bromwich A. | 5 - 5 | Manchester U. |
FT | West Ham U. | 4 - 2 | Reading |
FT | Wigan Athletic | 2 - 2 | Aston Villa |
Sunday, May 19, 2013
BPL YAFIKIA TAMATI MAN U, MAN CITY, CHELSEA, ARSENAL KUCHEZA UEFA.
BABA WA NEYMAE ASISITIZA MWANAE KUBAKI BRAZIL MAPAKA 2014
BABA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Brazil na klabu ya Santos, Neymar kwa mara nyingine amesisitiza kuwa mwanae atabakia nchini Brazil mpaka kipindi cha majira ya kiangazi 2014. Kumekuwa na tetesi nyingi kuhusu nyota huyo kutimkia klabu ya Barcelona katika kipindi cha miezi michache ijayo huku kocha wake Tito Vilanova akithibitisha kuwa mazungumzo baina ya pande hizo mbili yamefanyika. Hata hivyo baba yake Neymar amesisitiza kuwa mwanae amepanga kumaliza mkataba wake na Santos akidai kuwa kama Barcelona na Real Madrid zina mpango ya kumsajili nyota huyo basi hawana budi kusogeza mipango yao mwakani. Mzee huyo amesema mipango iliyopo ni kuona mwanae anamaliza mkataba na Santos na kama klabu hiyo ikiamua kumuuza kabla ya mkataba wake kumaliza basi wanapaswa kutoa taarifa kabla ili aweze kuzungumza na mwanae kama yuko tayari kwenda Ulaya.
ROY AKERWA NA CHELSEA, MAN CITY VS TOTTENHAM KWENA MAREKANI.

Klabu
hizi 3 zitasafiri n kuelekea Marekani kuumana zenyewe kwa wenyewe katika
Mechimbili za kirafiki huku Tottenham wakitua Visiwa vya Bahamas kucheza na
Jamaica.
ZIARA:
Mei 23: Man
City v Chelsea [St Louis]
Mei 25: Chelsea
v Man City [New York]
Mei 23: Tottenham
v Jamaica [Thomas A. Robinson National Stadium, Nassau Paradise Island,
Bahamas]
England
nayo inatarajiwa kucheza na Republic of Ireland, Uwanjani Wembley hapo Mei 29
na kisha kuruka kwenda Brazil kucheza Uwanja wa Maracana Jijini Rio De Janeiro na
Brazil hapo Juni 2.
Kikosi
cha Hodgson alichokiteua kuiwakilisha England katika Mechi hizo mbili kina
Wachezaji wanane toka Timu hizo tatu.
Chelsea
inasemekana imekubali kuwaruhusu Frank Lampard, Ashley Cole na Gary Cahill
kuondoka baada ya Mechi yao ya kwanza ya Tarehe 23 na Man City ili kurudi
London kujiunga na England.
Lakini
Hodgson amesema wao walipanga Mechi zao za Kimataifa kwa makusudi ili kuwapa
Wachezaji wote mapumziko ya Wiki moja baada ya Msimu wa Klabu zao kumalizika
kisha kuwachukua wao kwa Wiki moja na baada ya hapo kuwaachia kwenda Vakesheni
zao kabla kurudi Klabuni kwao kwa matayarisho ya Msimu mpya wa 2013/14.
Hogson
amesema Ziara hizo za Klabu zitawafanya wasafiri safari ndefu kuvuka Bahari ya
Atlantic na kurudi tena na hilo halitasaidia matayarisho yao.
Akimalizia
Hodgson alisema: “Hii ndio hali ambayo tumejikuta tunayo na hatuwezi
kulazimisha Klabu nini wafanye.”
KIKOSI
KAMILI:
MAKIPA: Ben
Foster, Joe Hart, Alex McCarthy.
MABEKI: Leighton
Baines, Gary Cahill, Ashley Cole, Phil Jagielka, Glen Johnson, Phil Jones,
Joleon Lescott, Kyle Walker.
VIUNGO: Michael
Carrick, Tom Cleverley, Frank Lampard, James Milner, Alex Oxlade-Chamberlain,
Theo Walcott.
MAFOWADI: Andy
Carroll, Jermain Defoe, Wayne Rooney, Daniel Sturridge, Danny Welbeck.
PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-
Pambalo la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.
Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Saturday, May 18, 2013
YANGA YAITANDIKA SIMBA BAO 2-0 NAKUPELEKA SHANGWE JANGWANI.
Katika mechi wa kukata na shoka wapinzani
wa jadi katika soka la Tanzania ambapo kwa ujumla leo ndio ilikuwa tamati ya ligi kuu Vodacom Tanzania bara
yanga leo imesheherekea ubingwa wake kwa furaha kubwa baada ya kuibamiza simba
Bao 2-0 katika Mechi iliyopigwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam
Yanga ambao walijinyakulia
Ubingwa mapema wakiwa na baadhi ya michezo mkononi, wameanza mechi hii kwa kasi
zaidi ambapo kunako dakika ya 4 ya mchezo mchezaji wa kimataifa kutoka Burundi Didier
Kavumbagu aliweza kutupia bao la kuongoza na kuleta furaha kwa mashabiki wa
yanga kote Tanzania.
Lakini katika Dakika ya 28 simba
walipata nafasi safi ya kusawazisha Bao hilo walipopata Penati kufuatia Nadir
Haroub 'Cannavaro' kumuangusha Mrisho Ngassa katika eneo la hatari lakini Mussa
Mudde alikosa Penati hiyo baada kipa alli Mustapha barthez kuicheza penati hiyo..
dakika 45 za kipindi cha kwanza Yanga 1
Simba 0 katika Kipindi cha Pili, Dakika ya 63, Hamis Kiiza alifungia Yanga Bao la Pili.
Kwenye Dakika ya 89 Mechi
hii iliingia balaa baada ya masoud Cholo wa Simba na DidierKavumbagu kuvaana na Refa Martin Saanya alipoingilia
kati na kuanguka chini na alipoamka
refa huyo alionekana kutokwa damu lakini Mechi iliendelea.
VIKOSI
VYA LEO:

Akiba: Said Mohamed, Juma
Abdul, Oscar Joshua, Nurdin Bakar, Nizar Khalfan, Said Bahanuz, Jerry Tegete
Simba: Juma
Kaseja, Nassor Masoud 'Chollo', Haruna Shamte, Shomari Kapombe, Mussa Mudde,
William Lucian, Mwinyi Kazimoto, Abdallah Seseme, Mrisho Ngassa, Amri Kiemba,
Haruna Chanongo
Akiba: Abel Dhaira, Miraji Adam, Ramadhan Singano 'Messi', Felix
Sunzu, Christopher Edward, Jonas Mkude, Hassan Mkude
REFA: Martin Saanya [Morogoro]
RATIBA/MATOKEO:
Jumamosi
Mei 18
Simba SC 0 Yanga 2
Toto Africans 2 Vs 0 Ruvu
Shooting
Mgambo JKT 1 Vs African Lyon 0
JKT Ruvu 1 Vs 0 Mtibwa
Sugar
TZ Prisons 0 Vs 1 Kagera
Sugar
JKT Oljoro 0 Vs 1 Azam FC
Polisi Moro 1 Vs 0 Coastal
Union
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Timu tano za juu hucheza michuano ya BANK ABC huku Yanga pia mwakani ikiwakilisha Taifa katika Club Bingwa afrika bila kusahau Azam fc kurejea tena katika michuano ya kombe la shirikisho barani afrika kwa mara ya pili baada ya mwaka ya mwaka huu kutolewa na timu ya Far Rabat kwa jumla ya bao 2-1.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Timu tano za juu hucheza michuano ya BANK ABC huku Yanga pia mwakani ikiwakilisha Taifa katika Club Bingwa afrika bila kusahau Azam fc kurejea tena katika michuano ya kombe la shirikisho barani afrika kwa mara ya pili baada ya mwaka ya mwaka huu kutolewa na timu ya Far Rabat kwa jumla ya bao 2-1.
Timu 3 zimeshuka daraja african lyon,Polisi morogoro,Toto african kuzipisha Mbeya city kutoka mbeya tanzania, Ashanti united ya Dar es saalam bila kusahau Rhino Rangers ya Tabora kucheza VPL Msimu ujao.
MSIMAMO:
MSIMAMO:
*YANGA =BINGWA
NA
|
TIMU
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
1
|
yanga
|
26
|
18
|
6
|
2
|
47
|
14
|
33
|
60
|
2
|
azam fc
|
26
|
15
|
6
|
4
|
45
|
20
|
25
|
54
|
3
|
simba sc
|
26
|
12
|
9
|
5
|
38
|
25
|
13
|
45
|
4
|
kagera sugar
|
26
|
11
|
8
|
6
|
26
|
19
|
8
|
44
|
5
|
mtibwa sugar
|
26
|
10
|
9
|
6
|
29
|
25
|
5
|
39
|
6
|
coastal union
|
26
|
8
|
11
|
6
|
25
|
24
|
2
|
35
|
7
|
ruvu shooting
|
26
|
8
|
8
|
9
|
22
|
26
|
-2
|
32
|
8
|
jkt oljoro
|
26
|
7
|
8
|
10
|
21
|
26
|
-5
|
29
|
9
|
tanzania prisons
|
26
|
7
|
8
|
10
|
16
|
23
|
-6
|
29
|
10
|
jkt ruvu
|
26
|
7
|
5
|
13
|
21
|
38
|
-18
|
29
|
11
|
mgambo shooting
|
26
|
7
|
4
|
14
|
16
|
27
|
-11
|
28
|
12
|
polisi morogoro
|
26
|
4
|
10
|
11
|
13
|
23
|
-11
|
25
|
13
|
toto african
|
26
|
4
|
10
|
11
|
21
|
33
|
-13
|
25
|
14
|
african lyon
|
26
|
5
|
4
|
16
|
16
|
38
|
-22
|
19
|
Subscribe to:
Posts (Atom)