Timu ya taifa ya Cameroon imefanikiwa kupata kocha mpya Volker
Finke kuwa kocha mkuu wa timu hiyo huku kibarua chake cha kwanza Mjerumani huyo ni kuhakikisha timu hiyo inafuzu michuano ya
Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil. Finke
anachukua nafasi ya kocha wa muda wa timu hiyo Jean-Paul Akono ambaye
aliwekwa hapo kuziba nafasi ya Denis Lavagne Septemba mwaka jana baada
ya Mfaransa huyo kushindwa kuisaidia timu hiyo kufuzu michuano ya
Mataifa ya Afrika 2012 na 2013. Kocha
huyo mwenye umri wa miaka 65 aliwahi kuifundisha klabu ya SC Freiburg
kuanzia mwak 1991 mpaka 2007 na atakuwa anafundisha kikosi cha timu ya
taifa kwa mara ya kwanza baada ya kutemwa na timu ya Urawa Red Diamonds
ya Japan na timu ya Cologne ya nchini kwake. Katika
mechi za kufuzu Kombe la Dunia, Cameroon wako kileleni mwa kundi I
wakiwa na alama sita katika mechi tatu walizocheza wakifuatiwa na Libya
wenye alama tano, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo-DRC alama nne na Togo
alama moja. Kazi
yake ya kwanza Finke itakuwa ni kukiongoza kikosi cha timu ya taifa ya
nchi hiyo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Ukraine utakaochezwa jijini
Kiev Juni 2 mwaka huu kabla ya kuhamishia nguvu zao katika mechi za
kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Togo Juni 9, DRC Juni 16 na Libya
Septemba 6 mwaka huu
Thursday, May 23, 2013
CLUB YA SANTOS YAKATAA OFA YA PILI YA BARCA

FA CHADAI KUWA CARROL AJITOA TIMU YA TAIFA KUTOKANA NA MAJERUHI.

KOCHA WA LIVERPOOL RODGERS HANA MPANGO WA KUMUUZA SUAREZ.
BOSI wa majogoo wa jiji la londo Liverpool Brendan Rodgers amesema hana mpango wa kumuuza mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Luis Suarez. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay alikosa mechi nne za Liverpool mwishoni mwa msimu huu baada ya kufungiwa mechi 10 kwa kumng’ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic lakini alimaliza katika nafasi ya tatu katika orodha ya wafungaji wa Ligi Kuu nchini Uingereza akiwa na mabao 23. Liverpool haijafuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya toka mwaka 2009 lakini pamoja na vilabu vikubwa kummezea mate Suarez, kocha huyo ana imani kwamba ataweza kumbakisha mchezaji huyo kwa msimu ujao. Rodgers amesema kwasasa wanajipanga kutengeneza kikosi chao kwa ajili ya msimu ujao na Suarez ni sehemu ya kikosi hicho ingawa amekiri kwamba zipo baadhi ya klabu kubwa zinazomtaka.
GARCIA AMUOMBA RADHI MCHEZAJI NAMBA MOJA TIGER WOODS
MCHEZAJI machachali wa mchezo wa gofu, Sergio Garcia ameomba radhi kwa kauli yake ambayo inaweza kuonekana kama ya kibaguzi kwenda kwa nyota wa mchezo huo anayeshika namba moja kwa ubora Tiger Woods. Garcia mwenye umri wa miaka 33 aliulizwa kama ataweza kula chakula cha jioni na Woods ili kuzungumzia tofauti zao za hivi karibuni na mchezaji huyo kutania kuwa atamuandalia kuku wa kukaanga nyota huyo. Kuku wa kukaanga ni chakula kinachohusishwa na watu weusi huko Marekani haswa wale wanaotoka kusini mwa nchi hiyo. Garcia aliomba radhi kwa kauli hiyo kama imeeleweka vibaya akidai kuwa hakumaanisha chochote kuhusu ubaguzi wa rangi kwa nyota huyo ambao ambaye asili yake ni mweusi.
MURRAY AJITOA MICHUANO YA WAZI UFARANSA:
MCHEZAJI nyota maarufu wa tenisi kutoka Uingereza Andy Murray amejitoa katika michuano ya wazi ya Ufaransa kutokana na maumivu ya mgongo yaliyopelekea kushindwa kuendelea kucheza katika michuano ya wazi ya Italia. Murray ambaye anashika namba mbili katika orodha za ubora Duniani kwa upande wa wanaume amejitoa katika michuano hiyo baada ya kushauriwa na madaktari wake na anatarajia kurejea tena uwanjani katika michuano ya Wimbledon katikati ya mwezi ujao. Nyota huyo ambaye ni bingwa wa michuano ya wazi ya Marekani amesema umekuwa ni uamuzi mgumu kufanya kwani huwa anapenda kucheza jijini Paris lakini imekuwa nje ya uwezo wake kwasababu ya ushauri wa kiafya aliopewa. Murray aliwaomba radhi waandaaji wa michuano hiyo na kuwashukuru mashabiki wake kwa kumtumia ujumbe wa kumuunga mkono na sasa kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kuhakikisha anapona na kurejea haraka uwanjani.
Wednesday, May 22, 2013
MWAMUZI WA AFRIKA KUSINI KUICHEZESHA STARS MOROCCO.

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.
Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.
Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.
Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;
Mei 22 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 23 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 23 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 25 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 26 Saa 3 asubuhi Uwanja wa Karume
MSIMAMO WA KUNDI C:
P W D L GF GA Pts
Ivory Coast 3 2 1 0 7 2 7
Tanzania 3 2 0 1 5 4 6
Morocco 3 0 2 1 4 6 2
Gambia 3 0 1 2 2 6 1
REKODI YA KIM POULSEN STARS
Mei 26, 2012
Tanzania 0 – 0 Malawi (Kirafiki)
Juni 2, 2012
Ivory Coast 2 – 0 Tanzania (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 10, 2012
Tanzania 2 – 1 Gambia (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 17, 2012
Msumbiji 1 – 1 Tanzania (Tanzania ilitolewa
kwa penalti kufuzu Mataifa ya Afrika)
Agosti 15, 2012
Botswana 3 – 3 Tanzania (Kirafiki)
Novemba 14, 2012
Tanzania 1-0 Kenya (Kirafiki)
Desemba 22, 2012
Tanzania 1-0 Zambia (Kirafiki)
Januari 11, 2013
Tanzania 1-2 Ethiopia (Kirafiki)
Februari 6, 2013
Tanzania 1-0 Cameroon (Kirafiki)
Machi 22, 2013
Tanzania 3-1 Morocco (Kufuzu Kombe la Dunia)
MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga atakuwa na mkutano na waandishi wa habari. Mkutano huo utafanyika kesho (Mei 23 mwaka huu) saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Subscribe to:
Posts (Atom)