Friday, June 7, 2013

TAIFA STARS SASA INAJITOSHELEZA- TENGA


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeishukuru Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kwa kuiwezesha timu ya taifa, Taifa Stars kuondokana na matatizo na kuwaomba Watanzania kuiombea timu ili ifanye vizuri katika mechi yake ya kesho (Juni 8 mwaka huu) dhidi ya Morocco mjini Marrakech.
Stars, ambayo inashika nafasi ya pili kwenye kundi lake la mashindano ya awali ya Kombe la Dunia ikiwa nyuma ya Ivory Coast kwa tofauti ya pointi moja, inacheza na Morocco katika mechi ya nne itakayofanyika Marrakech baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 katika mechi ya kwanza iliyofanyika Dar es Salaam mwezi Machi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Rais wa TFF, Leodegar Tenga alisema kuwa tangu kuanza kwa udhamini, TFF haijawahi kupata udhamini mkubwa kama wa Kilimanjaro Premium Lager ambayo imeingia mkataba wa miaka mitano wa kuidhamini Stars wenye thamani ya dola milioni 10 za Marekani.

“Katika kipindi chote hiki hatujawahi kupata udhamini ambao umekidhi mahitaji yote ya timu kama huu wa TBL,” alisema Tenga kwenye mkutano na waandishi uliofanyika kwenye ofisi za TFF.

“Lakini katika mwaka mmoja uliopita (tangu TBL ianze kudhamini) hatujawahi kushindwa kuisafirisha timu; kushindwa kulipa posho za wachezaji; kutanguliza watu wetu kwenda nje kuiandalia timu sehemu nzuri; kuzilipia tiketi za ndege timu tunazocheza nazo mechi za kirafiki na hata kuzilipia ada ya kucheza mechi (appearance fee).

“Posho za wachezaji zimepanda kwa karibu mara mbili na ndio maana leo wachezaji wanaijali timu yao. Yote haya ni kutokana na udhamini huu. Watu wanasema usione vinaelea….”

Tenga alisema kuwa udhamini huo ndio sasa umeanza kuzaa matunda na timu inafanya vizuri ikiwa ni pamoja na kuwa na maandalizi ya muda mrefu.

“Sasa tunawaomba Watanzania waiombee timu na tunawashukuru wale waliokwenda Morocco kuishangilia kwa kuwa vijana wetu wanapata nguvu pale wanapoona kuna watu wako nyuma yao,” alisema Tenga.

Rais huyo wa TFF pia alisifu kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kuiita timu Ikulu na kuongea na kula na wachezaji, akisema kitendo hicho kitasaidia kuongeza hamasa kwenye timu.

Naye Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema kampuni yake itaendelea kuwa bega kwa bega na TFF na kwamba uhusiano baina ya pande hizo mbili umeimarika na utaendelea kuimarika.

Katika mkutano huo, Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) lilikabidhi fulana maalum kwa ajili ya mashabiki ambao wamekwenda Morocco kuishangilia timu.

Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu alisema tayari fulana 250 zimegawiwa kwa mashabiki walioko Morocco na nyingine zilitarajiwa kusafirishwa jana.

USHIRIKI DARFUR MIKONONI MWA SERIKALI- TENGA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema kuwa ushiriki wa klabu za Tanzania kwenye mashindano ya Kombe la Kagame yaliyopangwa kufanyika kwenye miji ya Darfur Kaskazini na Gordofan Kusini nchini Sudan unategemea tamko la Serikali ambayo kwa sasa inafanya tathmini ya hali ya usalama.

Tenga, ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za TFF, alisema tayari TFF na Serikali zimeshafanya mazungumzo, na Serikali imepewa taarifa zote muhimu kuhusu mashindano kwa ujumla, malazi ya klabu za Tanzania, uhakika wa usalama, usafiri wa ndani na mambo mengine muhimu hivyo kwa sasa Serikali inatathmini taarifa hizo kabla ya kutoa tamko.

“Masuala ya usalama yako nje ya uwezo wa CECAFA. Kwa hiyo, kama Serikali itabaini kuwa hali usalama ya huko si nzuri, hatutaziruhusu na kama ikiona hali ni nzuri, itaruhusu,” alisema Tenga.

“Jukumu la CECAFA (Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu vya Nchi za Afrika Mashariki na Kati) ni kuandaa mashindano na kupata uhakika wa usalama kutoka nchi mwenyeji.
“Kama tukipata uhakika huo wa usalama, mashindano yanafanyika. Lakini nchi moja moja zinayo haki ya kuhoji usalama kwa kuwa ni wajibu wa Serikali hizo kujali maisha ya wananchi wake.”

Tenga alisema kuwa mashindano hayo yalikuwa yafanyike Ethiopia, lakini katika dakika za mwisho nchi hiyo iliomba isiandae mashindano hayo hadi mwakani na ndipo Sudan ilipojitokeza kuokoa mashindano hayo.

Alisema wakati wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu (FIFA) uliofanyika Mauritius, CECAFA iliitisha mkutano mkuu wa dharura na kupewa taarifa ya maandalizi ya mashindano hayo kutoka uongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Sudan na wanachama wakaridhia baada ya kuhakikishiwa usalama.

“Hivyo nchi wanachama wa CECAFA zimeridhia kushiriki baada ya kuhakikishiwa usalama, lakini kwa kuwa Waziri wetu ameonyesha wasiwasi kuhusu usalama wa Darfur, hatuna la kufanya zaidi ya kumsikiliza. Ni kauli ya kiongozi anayeonekana kuwajibika na ni lazima tusubiri tamko la Serikali,” alisema Tenga.

“Lakini napenda kuishukuru Serikali ya Sudan kwa uamuzi huo kwa sababu kuandaa mashindano hayo si kitu kidogo. Tayari Katibu Mkuu wa CECAFA (Nicholas Musonye) ameshakwenda kwenye maeneo hayo na kukaa wiki nzima akikagua viwanja na hoteli zitakazotumika na kuridhika nazo,” alisema.

Alisema watu wasipotoshe tamko la Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alilolitoa Bungeni kuhusu ushiriki wa timu zetu Darfur.

“Mhe. Membe alisema Serikali itafanya uchunguzi ijihakikishie kuwa hali ya usalama ni nzuri… alisema Serikali haitakubali kuruhusu raia wake kwenda Darfur wakati hali ya usalama si nzuri,” alisema Tenga.

“Kwa maana hiyo, na baada ya TFF kuipa Serikali taarifa zote muhimu kuhusu hali itakavyokuwa wakati wa mashindano, sasa tunasubiri tamko la Serikali. Na hii ni kawaida kabisa kwa kuwa hata hapa tunapoaandaa mashindano, ni lazima kwanza tupata uhakika wa usalama kutoka serikalini ndipo tuziite timu.”

Alifafanua kuwa si jukumu la CECAFA kuamua mashindano yafanyike mji gani na kwamba chama cha nchi mwenyeji ndicho kinachoamua mashindano yafanyike mji gani.

“Sasa kwa suala la Sudan, magavana wa majimbo hayo mawili ya Darfur Kaskazini na Gordofan Kusini waliomba kwa chama chao mashindano hayo yafanyike kwenye miji hiyo na Serikali ya Sudan ikaihakikishia CECAFA usalama,” alisema.



“Sasa ikitokea Serikali yetu ikasema hali si nzuri, hatutaziruhusu timu zetu ziende kwa sababu masuala ya usalama yako nje ya CECAFA.”

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

TAIFA STARS YAIKABILI MOROCCO UGENINI KESHO DIMBANI.

Taifa Stars inatupa karata yake ya pili ugenini kwenye mechi za mchujo za Kombe la Dunia kwa kesho (Juni 8 mwaka huu) kuikabili Morocco (Lions of the Atlas) kwenye Uwanja wa Grand Stade hapa Marrakech, Morocco.

Ilipoteza ya kwanza ugenini dhidi ya Ivory Coast mwaka jana, na kushinda mbili mfululizo nyumbani dhidi ya Gambia na Morocco. Mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za Morocco ni ya pili kwa Stars katika uwanja huo ambapo mwaka juzi ilifungwa mabao 3-1.

Washabiki wa Morocco wanaonekana kuikatia tama timu yao yenye pointi mbili tu nyuma ya Ivory Coast inayoongoza kundi hilo la C ikiwa na pointi saba ikifuatiwa na Tanzania yenye sita. Huo ni mtazamo wa washabiki, lakini kwa upande wa timu inaonekana imepania kujichomoa katika nafasi za chini.

Kwa upande wa Kocha wa Stars, Kim Poulsen amesema timu yake imepania mechi hiyo, lengo likiwa ni kuona inapata matokeo mazuri baada ya dakika 90 za mechi hiyo itakayokuwa chini ya refa Daniel Frazier Bennett wa Afrika Kusini.

Amesema timu yake itacheza kwa umakini na uangalifu kwa vile wanajua wapinzani wao wakicheza mbele ya washabiki wao watakuwa katika shinikizo za kushinda, jambo ambalo wamejiandaa kukabiliana nalo.

Kwa upande wa maandalizi, Kim amesema Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na wadhamini wa timu hiyo Kilimanjaro Premium Lager wameiandaa vizuri kwani iko kambini kwa wiki tatu sasa na kupata mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan iliyochezwa wiki iliyopita nchini Ethiopia.

Stars iliifunga Morocco mabao 3-1 zilipokutana Machi 24 mwaka huu jijini Dar es Salaa. Lakini zilipokutana hapa Marrakech mara ya mwisho mwaka 2011, Morocco iliibuka na ushindi wa mabao 3-1.

Kim amesisitiza kuwa kikosi chake kimepania kufanya vizuri katika michuano hii ya mchujo ya Kombe la Dunia, ha hiyo inathibitishwa na matokeo ya timu kadri inavyoendelea kucheza mechi za mashindano.

“Moja ya mipango yetu katika mechi hizi za Kombe la Dunia ni kushinda nyumbani, hilo hadi sasa tumelifanya kwa asilimia 100. Lakini ili tukae vizuri zaidi tumekuja hapa Morocco kwa lengo la kupata matokeo mazuri, ingawa tunajua mechi itakuwa ngumi,” amesema kocha huyo raia wa Denmark.

Kwa hapa Marrakech mechi hiyo imekuwa haizungumzwi mara kwa mara, na kubwa ni kuwa Wamorocco wengi wanaamini kuwa timu yao ambayo hadi sasa ina pointi mbili haina nafasi ya kusonga mbele katika hatua inayofuata ya michuano hiyo.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Marrakech, Morocco
+212 610120619

GAZIDIS ATHIBITISHA KUWA ARSENAL WENGER ATAONGEZA MKATABA MPYA.

MTENDAJI Mkuu wa The Gunners club ya Arsanal Ivan Gazidis ametanabaisha kuwa kocha wa timu hiyo Arsene Wenger anataka aongeze Mkataba wake mwishoni mwa msimu ujao na kuiongoza klabu hiyo kufanya vizuri katika soka ya Ulaya.
Mkataba wa Wenger unaisha mwakani na tayari amepata ofa kibao kuanzia nyumbani kwao Ufaransa, ambako Paris Saint-Germain na klabu yake ya zamani, Monaco zinamtaka.
Sign him up! Gazidis wants the French boss to extend his deal with Arsenal beyond next summer
Gazidis (chini kushoto) anataka Mfaransa aongeze Mkataba mwishoni mwa msimu ujao
Sign him up! Gazidis wants the French boss to extend his deal with Arsenal beyond next summer
Matokeo mabaya ya miaka ya karibuni yalitarajiwa kumuweka katika wakati mgumu kocha huyo mwenye umri wa miaka 63, lakini Gazidis anatarajia atabaki na kuunda kikosi cha nguvu.
Pato la mwaka la Arsenal linatarajiwa kuongezeka kwa Pauni Milioni 70, na kuwasogeza kwa wanaopata Pauni Milioni 300, Real Madrid, Barcelona, Manchester United na mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich.
Hiyo itawapa fursa ya kushindana na klabu hizo kununua wachezaji wa kuanzia Pauni Milioni 25 na kutaka mishahara ya kuanzia Pauni 200,000 kwa wiki kama Wayne Rooney, mmoja kati ya wachezaji inayowataka hivi sasa.
Klabu tatu za juu katika msimamo wa Ligi Kuu ya England, Manchester United, City na Chelsea zote zimebadilisha makocha wao, lakini Arsenal bado na imani na Wenger.

JOSE MOURINHO AJA NA KASI MPYA NA NGUVU MPYA KATIKA USAJILI".

Baada ya kukabidhiwa bikoba kwa mara ya pili ndani ya Chelsea jose mourinho amekuja kasi mapya ya kutafuta  washambuliaji kikosini hapo baada ya jana usiku kuanza mazungumzo na mchezaji mwenye thamani ya Pauni Milioni 50, Edinson Cavani wa Napoli, saa kadhaa baada ya kutoa ofa ya Pauni ya Milioni 34.9 kumnasa mshambuliaji wa Zenit St Petersburg, Hulk.
Kocha Mourinho ameorodhesha wachezaji wanne anaowataka wakiwemo kutoka Fiorentina, Stevan Jovetic na Manchester City, Edin Dzeko katika orodha hiyo.
Interest: Napoli have opened talks with Chelsea over Uruguay striker Edinson Cavani (left)
Napoli imeanza mazungumzo na Chelsea kuhusu mshambuliaji wa Uruguay, Edinson Cavani (kushoto)
Mourinho ameweka wzi na kuamini kuwa atamsajili mchezaji wa Pauni Milioni 25, Jovetic na kuwapiku Juventus, lakini anakabiliwa na ushindani kutoka klabu yake ya zamani, Real Madrid katika kuwania saini ya Cavani wakati Dzeko anaonekana kuwa mboni mbadala. Napoli haijakataa mpango wa kubadilishana Cavani na Dzeko na Manchester City, lakini mpango unaonekana kusinzia.
Rais wa Napoli, Aurelio de Laurentiis alisema jana usiku: "Kuna dhamira kutoka Chelsea kwa Cavani, watanipigia mimi saa chache zijazo. Nitafurahi akibaki, lakini ikiwa ataondoka atampata mbadala wake,".
Mshambuliaji wa Brazil, Hulk pia amethibitisha Mourinho anamtaka Stamford Bridge.
Target: Chelsea have made a £35m offer for Zenit St Petersburg's Brazilian forward Hulk
Chelsea imetoa ofa ya Pauni Milioni 35 kwa Zenit St Petersburg juu ya Mbrazil, Hulk.

MAN CITY YATANGAZA RASMI KUMTWAA KIUNGO WA KIBRAZILI FERNADINHO.

Mabingwa wa ligi kuu nchini uingereza msimu wa 2011-2012 klabu ya Manchester City imetangaza rasmi kumsajili kiungo wa kimataifa wa Brazil Fernadinho kutoka klabu ya Shakhtar Donetski ya Ukraine. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28 amekuwa katika rada za City kwa karibu msimu mzima na anajulikana nchini Uingereza kwa kuifungia klabu yake bao katika ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Chelsea katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi msimu uliopita. City ambao mpaka sasa hawajapa mbadala wa kocha Roberto Mancini aliyeondoka, hawakutoa taarifa zozote za kiasi cha fedha walizomnunulia mchezaji huyo lakini kumekuwa na tetesi katika vyombo vya habari nchini Uingereza kuwa amewagharimu kiasi cha paundi milioni 30. Akihojiwa Fernadinho amesema kuwa hayo ni mabadiliko, changamoto na nafasi aliyokuwa akiisubiria kwa kipindi kirefu na kuichezea City ni kama ndoto zake zimekuwa kweli. 

FALCAO AWEKA WAZI KUWA NIA KUBWA NI KUIPA MAFANIKIO MONACO.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao amesema nia yake kubwa ni kuisadia klabu ya Monaco ya Ufaransa kuwa moja ya klabu bora barani Ulaya kwa mara nyingine tena. Akihojiwa baada ya mazoezi na timu yake ya taifa jana Alhamisi Falcao amesema anajisikia fahari kubwa kuwapo Monaco hivyo kutokana na kuvutiwa na mipango waliyokuwa nayo katika kipindi kijacho hivyo mategemeo yao nikuifikisha timu hiyo katika anga za mafanikio. Akiwa Monaco nyota huyo wa zamani wa klabu ya Atletico Madrid ataungana na winga James Rodriguez ambaye pia ni raia wa Colombia baada ya kukubali uhamisho akitokea klabu ya FC Porto. Falcao amesema ana mahusiano mazuri na winga huyo na sio katika soka pekee bali wamekuwa marafiki wa karibu hata nje ya uwanja, na kummwagia sifa kwamba ni mchezaji bora ndio maana Monaco wametumia fedha nyingi kumsajili. 

BOLT MKALI WA MBIO FUPI DUNIANI KUKABIDHI ZAWADI NCHINI UFARANSA.

SHIRIKISHO la Tenisi nchini Ufaransa limetangza kuwa mshindi wa michuano ya wazi ya Ufaransa kwa upande wa wanaume atakabidhiwa zawadi na mkimbiaji nyota wa mbio fupi duniani raia wa Jamaica Usain Bolt.

Bolt bingwa mara sita wa michuano ya Olimpiki ambaye jana alishindwa kutamba katika mashindano ya Diamond League yaliyofanyika jijini Rome itali baada ya kushindwa na Justin Gatlin wa Marekani, atakuwa mwanariadha wa kwanza kupata heshima hiyo kwenye michuano mikubwa ya tenisi. 

Nusu fainali kwa upande wanaume inatarajiwa kufanyika leo ambapo bingwa mtetezi wa michuano hiyo Rafael Nadal anatarajia kuchuana na Novak Djokovic ukifuatiwa na mchezo mwingine wa nusu fainali kati ya Jo-Wilfried Tsonga dhidi ya David Ferrer. Kwa upande wa wanawake ambapo fainali itafanyika Jumamosi kati ya Serena Williams na maria Sharapova, tuzo yao itakabidhiwa na bingwa mara tatu wa zamani wa michuano hiyo ambaye pia amewahi kuongoza katika orodha za ubora kwa wanawake Arantxa Sanchez Vicario wa Hispania.