Wednesday, July 3, 2013

KUNANI HAPO?BOLOVIA MIAKA 17 IJAYO VIJANA KUITWA NEYMAR"

Katika taarifa za takwimu za ofisi ya msajili jijini La paz, Bolivia miaka 17 ijayo vijana wengi wa kiume wanaoishi katika mji huo watakuwa wakiitwa jina la mshambuliaji mpya wa fc barca Neymar. Katika taarifa iliyotolewa na gazeti moja nchini humo watoto 20 kati ya 100 wanaozaliwa katika mji mkuu huo wan chi hiyo wamepewa jina la nyota huyo mpya wa Barcelona ambaye amewateka mashabiki dunia nzima kutokana na kiwango cha hali ya juu alichokionyesha katika michuano ya Kombe la Shirikisho. Ofisa mmoja aliyetambulika kwa jina la Remigio Condori amesema wazazi wengi katika mji huo wanachagua jina la Neymar kwakuwa ndio liko katika fasheni ambapo miaka 17 ijayo vijana wengi wa kiume watakuwa wakiitwa jina hilo. Neymar ambaye amsajili na Barceona kwa ada ya euro milioni 57, alifunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 4-0 iliyopata Brazil dhidi ya Bolivia April mwaka huu.

ARSENAL KATIKA MVUTANO NA REAL MADRID-HIGUAIN"

Katika harakati za usajili mara baada ya kuinasa saini ya nyota wa klabu ya AJ Auxerre, Yaya Sanogo klabu ya Arsenal sasa inapambana kukamilisha kumsajili nyota wa klabu ya Real Madrid, Gonzalo Higuain. 
Klabu hizo mbili zimekuwa katika mvutano kuhusu ada ya uhamisho wa nyota huyo ambapo Arsenal wameonekana kuwa tayari kutoa kitita cha euro milioni 25, wakati Madrid wao wanataka ada iwe euro milioni 25.5. Kumekuwa na taarifa kuwa Arsenal wameshafikia makubaliano binafsi na mchezaji huyo ambapo ataanza na mshahara wa paundi 100,000 kwa wiki, mshahara ambao utamfanya kuwa mmoja wa wachezaji wanaolipwa zaidi kwenye klabu hiyo wakiwemo Theo Walcott na Thomas Vermaelen. Higuain ambaye nia raia wa Argentina inasenekana alikuwa akilipwa kiasi cha paundi 64,000 kwa wiki akiwa Madrid.

Tuesday, July 2, 2013

BRAZIL HAINA UBAVU DHIDI YA HISPAIN IJAPO KUWA IMESHINDA 3-0


NGULI wa soka Duniani Raia wa Argentina, Diego Maradona anaamini kuwa Hispania wasingepoteza mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Brazil kama wangecheza katika uwanja huru. Mabingwa hao wa Ulaya na Dunia walitandikwa mabao 3-0 katika Uwanja wa Maracana na Maradona mwenye umri wa miaka 52 anaamini kuwa mazingira yalikiathiri kikosi cha Hispania kinachonolewa na Vincente Del Bosque. Akihojiwa na waandishi wa habari katika ziara ya nchini Indonesia Maradona amesema Hispania hawakuwa na bahati kwakuwa walikuwa wakicheza nchini Brazil na anaamini kuwa nchi hiyo isingewafunga kama mchezo huo ungechezwa katika uwanja huru. Maradona pia hakusita kumsifia Lionel Messi na kudai kuwa bado ni mchezaji bora na mahasimu wake Cristiano Ronaldo na Neymar bado hawajafikia ubora wake.

NEYMAR NA ALBA KUFANYIWA UPASUAJI WA MAFINDIFINDO YA SHIGONI"TOSEZI"


Mkali mpya wa FC Barcelona, Neymar na beki Jordi Alba wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mafindofindo Ijumaa na wanatarajiwa kupona baada ya siku 10. Upasuaji huo ulipangwa kufanyika baada ya fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho iliyofanyika jijini Rio de Janeiro Jumapili iliyopita ambapo Brazil iliisambaratisha Hispania kwa mabao 3-0. Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo Neymar anatarajiwa kufanyiwa upasuaji huo huko Rio na baadhi ya madaktari wa Barcelona wanakuwepo kusaidia. Wakati Alba mwenye miaka 24 yeye atafanyiwa upasuaji wake siku hiyohiyo lakini katika kliniki iliyopo karibu na jiji la Barcelona na wote wanatarajiwa kupona ndani siku 10 baada ya upasuaji huo.

ARSENAL SASA YAJIWEKA KAMILI GADO KWA MSIMU MPYA WA BPL NCHINI UINGEREZA"

Wakiwa chini ya kocha Mfaransa, Aserne Wenger Timu ya soka ya Arseanal wamefanikiwa kuinasa saini ya nyota kinda wa kimataifa kutoka nchini Ufaransa, Yaya Sanogo kwa kumpa mkataba mrefu Emirates.
Kinda huyo kwa sasa yupo na timu ya taifa ya vijana ya Ufaransa chini ya umri wa miaka 20m katika fainali za Kombe la Dunia la vijana chini ya umri wa miaka 20 huku akiwa amefumania nyavu mara mbili kati ya matatu ya timu yake nchini Uturuki.
Akicheza ligi daraja la kwanza nchini Ufaransa, Sanogo  amefunga mabao tisa  katika mechi 13 huku akiandamwa na majeruhi ya mara kwa mara.
Target man: Sanogo has built an excellent reputation for himself in France 
Mtu mwenye dili kwa sasa: Sanogo amejijengee nafasi nzuri sana katika taifa la Ufaransa
More to come? Higuain (left) and Rooney (right) are also thought to be on Wenger's wishlist 
Nyota wengine wa kutua Emirates? Higuain (kushoto) na Rooney (kulia) pia wapo katika rada za Wenger ambaye anataka kupata nyota wakali wa kuimarisha kikosi chake msimu ujao
Gonzalo Higuain na Wayne Rooney wameripotiwa kuwa katika mipango ya Wenger msimu ujao, lakini kocha huyo raia wa Ufaransa amevutiwa na kinda Sanogo.
‘Sanogo ni mchezaji mzuri sana atakayesaini kwetu, ameonesha kiwango kikubwa katika klabu yake ya Auxerre na katika kikosi cha timu ya taifa chini ya umri wa miaka 20″. Alisema Wenger.

MTIBWA SUGAR YAJIPANGA KUJIWEKA SAWA NA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI KUU TZ BARA"

Kikosi cha mtibwa sukari
Timu ya Mtibwa Sugar ya manungu turiani ya mkoani morogoro inayonolewa na kocha mzawa Mecky Mexime wanatarajia kujiweka sawa katikati ya mwezi huu wa saba ili kujiandaa na mshikemshike wa msimu mpya waligi kuu soka Tanzania bara unaotarajiwa kuanza Agosti 24.
Mwenyekiti mwenye dhamana ya kuiongoza timu hiyo kubwa nchini Tanzania yenye historia ya kuzisumbua Simba na Yanga na kutwaa taji miaka ya nyuma, Jamal Baiser amesema kwa sasa wanafanya mipango ya kusajili wachezaji wa kuziba nafasi zilizoachwa wazi  kufuatia baadhi ya wachezaji kutimka klabuni hapo.
“Mpaka sasa hatujasajili wachezaji, lakini mipango yetu ni kusajili wachezaji wapatao watano, na baada ya kukamilisha taratibu zote, tutawajulisha mashabiki wetu. Kikubwa ni kwamba, tunahitaji kuwa na timu nzuri zaidi kuliko misimu mitatu iliyopita”. Alisema Baiser.
Baiser alisema kwa muda mrefu sasa,  Mtibwa sugar haifanyi vizuri sana wala vibaya sana, lakini kwa msimu ujao wanajiandaa kuwa timu bora zaidi,  huku wakichanganya damu changa na kongwe katika kikosi chao.
Mwenyekiti huyo alisema timu yao amepoteza baadhi ya wachezaji akiwemo Issa Rashid “Baba Ubaya” aliyejiunga na wekundu wa Msimbazi Simba pamoja na Hussein Javu anayesemekana kusaini yanga, lakini wana wachezaji wengine wa kuziba nafasi zao na wengine watawasajili.
“Walikuwa wachezaji muhimu sana, lakini hatuna jinsi, soka ni ajira yao, hatuna uwezo wa kuwabania nafasi ya kucheza klabu  nyingine, ila kiuhakika tunao wachezaji wengi sana wa kuziba nafasi zao nab ado tunatafuta nyota wengine wa kuwasainisha”. Alisema Baiser.
Akizungumzia suala la Javu kusaini Yanga, Baiser alisema Mtibwa Sugar  ilikuwa na mkataba naye, lakini Yanga waliomba ruhusa ya kuzungumza naye na wao wakakubali.
“Walituomba kuongea na Javu, tuliwaruhusu. Kama wamekubaliana na kumpa mkataba sisi bado hatuna taarifa ofisini, Yanga bado hawajaja kufanya taratibu za uhamishoi, kwahiyo hatujui kama wameshamalizana naye, hivyo sitaki kulizungumzia sana kwa sasa, wakati utafika nitazungumza”. Alisema Baiser.
Baiser alisema Javu alikuwa mchezaji muhimu sana, lakini wanajipanga kutafuta mbadala wake.

WEBB ASEMA WAAMUZI WANAIMANI KUBWA NA MFUMO MPYA WA TEKNOLOGIA YA MSTARI WA GOLI

Howard Webb Mwamuzi wa Uingereza amedai kuwa waamuzi wana imani kubwa na mfumo mpya wa teknologia ya kompyuta katika mstari wa goli ambao utatumika katika michuano ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil. Hakuna bao lolote kati ya mabao 68 yaliyofungwa katika michuano ya Kombe la Shirikisho lililohitaji teknologia hiyo ambayo ndio ilikuwa imeanza kutumika kwa mara ya kwanza kwenye michuano hiyo. Lakini Webb aliwaambia waandishi wa habari jijini Rio de Janeiro kwamba uhakika wa mfumo huo unawapa faida kubwa na waamuzi wana imani kwa kiasi kikubwa na mfumo huo ambao umefungwa na kampuni ya Kijerumani iliyoshinda zabuni hiyo ya GoalControl. Webb amesema hawana shaka na uthabiti wa mfumo huo na umeonekana kufanya kazi vyema hivyo anadhani utaendelea kufanya kazi hata katika michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Webb ambaye alichezesha mchezo wa fainali kati ya Kombe la Dunia mwaka 2010 kati ya Hispania na Uholanzi nchini Afrika Kusini ni mmoja katika orodha ya waamuzi 52 ambao watachujwa kwa ajili ya michuano hiyo mwakani.