Sunday, February 16, 2014

LA LIGA: BARCA YAITANDIKA 6-0 RAYO VALLECANO

FC Barcelona Mabingwa Watetezi wa La Liga huko SPAIN,Jana Usiku wakiwa katiak dimba la Nou Camp, waliichalaza Rayo Vallecano Bao 6-0 na kuendelea kukaa kileleni mwa Ligi hiyo wakifungana kwa Pointi na Atletico Madrid lakini wao wako juu kwa ubora wa Magoli.
Goli za Barca kwenye Mtanange huo yamewekwa kimiani na Neymar, Lionel Messi, Bao 2, Pedro, Sanchez na Adriano.
Nao, Atletico Madrid, mapema hiyo Jana waliichapa Real Valladolid Bao 3-0 kwa Bao za Raul Garcia Escudero
, Diego Costa na Diego Godin.
Leo hii Real Madrid, ambao wako Ugenini kucheza na Getafe, wana nafasi ya kuzikamata Barca na Atletico ikiwa watashinda lakini watamkosa Supastaa wao Cristiano Ronaldo ambae atakuwa akitumikia Mechi ya Pili ya Kifungo chake cha Mechi 3.
RATIBA/MATOKEO:
[Saa za Bongo]
Ijumaa Februari 14
Elche CF 0 Osasuna 0
Jumamosi Februari 15
Atletico de Madrid 3 Real Valladolid 0
Levante 1 UD Almeria 0
FC Barcelona 6 Rayo Vallecano 0
Villarreal CF 0 Celta de Vigo 2
Jumapili Februari 16
1400 Granada CF v Real Betis
1900 Getafe CF v Real Madrid CF
2100 Athletic de Bilbao v RCD Espanyol
2300 Sevilla FC v Valencia
Jumatatu Februari 17
2400 Malaga CF v Real Sociedad
MSIMAMO-Timu za Juu:

NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 FC Barcelona 24 19 3 2 69 17 52 60
3 Atletico Madrid 24 19 3 2 59 16 43 60
2 Real Madrid CF 23 18 3 2 65 24 41 57
4 Athletic Bilbao 23 13 5 5 42 28 14 44
5 Villarreal CF 24 12 4 8 44 29 15 40
6 Real Sociedad 23 10 7 6 42 34 8 37
7 Sevilla FC 23 8 7 8 42 41 1 31
8 Valencia 23 9 4 10 36 35 1 31

JK AWAPA RUNGU CCM, AWATAKA KUACHA UNYONGE DHIDI YA CHADEMA".

MWENYEKITI wa CCM, Rais Jakaya Kikwete amewapa rungu wana-CCM akiwataka  kuacha kujifanya wanyonge dhidi ya vitendo vya fujo ambavyo hufanyiwa na  Chadema hasa nyakati za uchaguzi.




Rais Kikwete amesema hayo leo, wakati akiongoza kikao maalum cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM mjini Dodoma.

“Uchaguzi wa Kalenga ndiyo huo upo mbele yetu, hadi sasa hakuna tatizo lililojitokeza kama Arumeru mambo yapo shwari kabisa, lakini tujue tu kwamba pale tunaenda kushindana na watu (Chadema) ambao wao silaha yao ya kwanza ni vujo.. ninaagiza sasa lazima wana CCM kukabiliana na fujo zao. Unyonge basi.”, alisema Rais Kikwete na kuongfeza;

“CCM kuendelea kujifanya wanyonge kila mara sasa basi. Haiwezekazi watu wanafanya vujo hadi kuwatoboa watu macho ninyi nmanyongea tu, hili haliwezekani. Tazama pale Ingunga  mtu wenu alimwagiwa tindikali hadi leo ana  ulemavu wa kudumu kisa uchaguzi tu, aah haiwezekani kabisa”, alisema Rais Kikwete.

Mapema Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete alipongeza wana CCM na viongozi wao katika Kata zote zilizofanya uchaguzi mdogo wa Udiwani na hatimaye CCM kuibuka na ushindi wa Kata 23, Chadema ikiambulia tatu na NCCR Mageuzi kimoja.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-brGp3ubKcaSU7smoXfjTAApUg9f-YwbT3atmCqVx6i5JXWg8q23PhU_rOCHS91U3LbUya0oXNUJ93VIe3GyKWlXoqePApyka_4M8sqa37GHHhi73ftK2h3rYFcUf6wh4kx3U6iR6777q/s1600/13.jpg
Hata hivyo Rais Kikwete alisema, licha ya CCM kuzoa kata nyingi kwenye uchaguzi huo, viti vinne kwenda kwa upinzani bado ni doa hivyo lazima CCM Kihakikishe inazikomboaata hizo nyakati za chaguzi zijazo.

“Ni kweli tumezoa kata nyingi, lakini kwa kuwa lengo letu CCM kila wakati ni kushinda tu, hatua hiyo ya kuzikosa kata nne bado ni doa lazima kuzikomboa kata hizo chaguzi zijazo”, alisema, Rais Kikwete.

Pia alipongeza CCM, kwa ushindi iliopata kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Kimbesamaki na kwamba CCM inaona fahari kulirejesha jimbo hilo mikononi mwake, kwa kuwa ilikuwa imelazimika kumfuza mwakilishi wake wa awali kwenye jimbo hilo kwa kuwa alikuwa msaliti aiyefaa kuendelea kuwemo ndani ya Chama

Saturday, February 15, 2014

VPL: MBEYA CITY YATOKA SARE 1-1 VS SIMBA DIMBANI SOKOINE

VPL_2013-2014-FPLigi Kuu Vodacom tanzania Bara  imeendelea leo katika Viwanja mbalimbali lakini mchakamchaka ulikuwa katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya ambapo Wagonga Nyondo Mbeya City waliumana uso kwa uso na Simba na matokeo kuwa Sare ya Bao 1-1.
Mbeya City ndio walikuwa wa kwanza kutikisa Nyavu  katika Dakika ya 14 kwa Penati ya Deogratius Julius na Amisi Tambwe kuisawazishia Simba katika Dakika ya 50.
Simba na Mbeya City sasa zimecheza Mechi mbili zaidi ya Vinara Azam FC, wenye Pointi 36, na Timu ya Pili Yanga, wenye Pointi 35.
RATIBA/MATOKEO:
Jumamosi Februari 15
Rhino Rangers 1 Mgambo JKT 1
Ashanti United 0 Kagera Sugar 0
Mtibwa Sugar 0 Tanzania Prisons 1
JKT Oljoro 0 JKT Ruvu 0
Mbeya City 1 Simba 1
Ruvu Shooting 1 Coastal Union 0
­­MSIMAMO  VPL:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Azam FC
16
10
6
0
19
36
2
Yanga SC
16
10
5
1
22
35
3
Mbeya City
18
9
8
1
10
35
4
Simba SC
18
8
8
2
17
32
5
Ruvu Shooting
17
6
7
4
3
25
6
Kagera Sugar
18
5
8
5
0
23
7
Coastal Union
18
4
10
4
3
22
8
Mtibwa Sugar
18
5
7
6
-1
22
9
JKT Ruvu
17
6
1
10
-8
19
10
Ashanti United
17
3
5
9
-14
14
11
JKT Oljoro
18
2
8
8
-14
14
11
Mgambo
18
3
5
10
-18
14
14
Prisons FC
15
2
7
6
-9
13
12
Rhino Rangers
18 3 6 9 -10 13

RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano Februari 19
Tanzania Prisons v JKT Ruvu
Jumamosi Februari 22
Ruvu Shooting v Yanga
Kagera Sugar v Rhino Rangers
Mtibwa Sugar v Ashanti United
Coastal Union v Mbeya City
JKT Oljoro v Mgambo JKT
Azam FC v Tanzania Prisons
Jumapili Februari 23
Simba v JKT Ruvu

FA CUP: LEO JUMAMOSI NI MAN CITY v CHELSEA!!

FA_CUP_2013-2014FA CUP
Raundi ya Tano
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumamosi Februari 15
15:45 Sunderland v Southampton
18:00 Cardiff v Wigan
18:00 Sheff Wed v Charlton
20:15 Man City v Chelsea
Jumapili Februari 16
16:30 Everton v Swansea
18:00 Sheff Utd v Nottm Forest
19:00 Arsenal v Liverpool
Jumatatu Februari 17
22:45 Brighton v Hull City

MANCHESTER CITY v CHELSEA
Kuelekea Mechi ya leo Tunakumbuka Wiki ziliyopita, kwenye Mechi ya Ligi iliyochezwa Etihad, Chelsea waliifunga Man City Bao 1-0 na kwenye FA CUP wameshakutana mara 4 na City kufungwa mara ya kwanza, Mwaka 1915, lakini wameshinda mara zote 3 zilizobakia ikiwemo mara ya mwisho Msimu uliopita walipoifunga Chelsea 2-1 kwenye Nusu Fainali.
Man City hawajashinda katika Mechi zao mbili zilizopita, wakifungwa moja na Sare moja, lakini Chelsea hawajafungwa katika Mechi zao 12 zilizopita wakishinda 9 na Sare 3.

ARSENAL VS LIVERPOOL KESHO FEB16
Hapa kazi ipo itakuwa  FA CUP yenye upinzani kutokana Arsenal watataka kulipa kisasi cha Jumamosi iliyopita kunyukwa Bao 5-1 huko Anfield kwenye Mechi ya Ligi.
Kwenye FA CUP, Timu hizi zimekuwa zikukutana kila Msimu katika Misimu 12 iliyopita na Arsenal kushinda mara 7, zikiwemo Fainali 2, na Liverpool  kushinda Fainali 1 na kusonga mara 4 mbele ya Arsenal.
Katika Mechi za FA CUP 8 zilizopita , Arsenal wamefungwa moja tu na Liverpool na hiyo ilikuwa kwenye Fainali ya 2001.
Katika Mechi 12 zilizopita wakicheza kwao Emirates, Arsenal hawajafungwa hata Bao moja kati Mechi 11.
Liverpool hawajafungwa katika Mechi 9 zilizopita wakishinda 7 na Sare 2.

JK: MTANDAO WA UJANGILI WAJULIKANA


Rais Jakaya Kikwete, amesema mtandao wa majangili unajulikana na jitihada za serikali zimefanikiwa kukamata vigogo 40 walio kwenye mtandao mkubwa wa biashara ya nyara hizo za serikali.
 
Akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya BBC , jana asubuhi alisema watuhumiwa hao wamebainika kuwa wanajihusisha na mtandao kwenye ukanda wa Kaskazini na kwamba tajiri mkuu wa biashara hiyo naye amefahamika na kwamba anapatikana mkoani Arusha .
Akizungumza katika kipindi cha Amka na BBC , alikozungumzia ujangili, alieleza kuwa mtandao umefahamika na kwamba unahusisha matajiri na miongoni mwa watu hao 40 yupo tajiri huyo wa Arusha ambaye hakutaka kumtaja jina redioni.

“Tumeutambua mtandao huo hadi wakubwa zao ni matajari pale Arusha kuna mmoja mkubwa ambaye sitaki kumtaja jina alikuwa akiendesha biashara hiyo naye yupo kwenye kundi hili la watu 40 kazi iliyokuwa ikifanyika ni kuutambua huo mtandao kwa upana,” alisema.

Awali alisema Tanzania ilikuwa na tembo wengi barani Afrika na hata duniani wakati huo baada ya Uhuru walikuwa 350,000 na ilipofikia mwaka 1987 walipungua hadi 55,000.
Alisema hapo ndipo serikali ilipofanya maamuzi ya kuingiza jeshi katika mapambano ya kupambana na ujangili jambo lililosaidia kwa kiasi kupunguza tatizo.

Hata hivyo, alisema ilipofikia mwaka 1989 shirika linaloshughulikia haki za wanyama walioko hatarini kutoweka (CITES) ilifanya maamuzi ya ku
piga marufuku biashara ya pembe za ndovu duniani.
Rais Kikwete alisema kwa mambo hayo mawili ikiwamo nguvu ya jeshi kuingilia kupambana na ujangili pamoja na biashara hiyo kupigwa marufuku duniani ilisaidia kupungua ujangili na tembo kuanza kuonekana.

Alisema ilipofika mwaka 2009 hesabu ilikuwa kubwa ambapo idadi ya tembo iliongezeka na kufikia 110,000.

Alipohojiwa juu ya gazeti moja la Uingereza la Daily Maili kumuandika kuwa hajafanya jitihada za kutosha kupambana na ujangili, alisema gazeti hilo limeandika uongo na kwamba serikali imejitahidi kufanya mikakati mbalimbali kuokoa maisha ya tembo na kupunguza ujangili.

Pembe hizo za ndovu wanaouliwa Afrika soko lake lipo katika nchi za Asia ikiwamo China.

Kikwete alisema jitihada mbalimbali zimefanywa ndiyo maana mtandao huo ambao unajihusisha na biashara ya meno ya tembo umegundulika.

Wakati Rais akiwa kwenye mkutano nchini Uingereza uliokuwa ukijadili ujangili na biashara haramu ya meno ya tembo na pembe za faru, polisi mkoani Singida wamemkamata George James na vipande 21 vya meno hayo.

Polisi ilisema meno hayo yenye thamani ya Sh. milio
ni 43 yana uzito wa kilo 49.

MAHOJIANO NA CNN
Wakati huo huo, ujangili umemfikisha Rais Kikwete, kwenye televisheni y
a CNN ya Marekani, alikohojiwa akitakiwa kueleza vita dhidi ya majangili inayofanyika nchini.
Akihojiwa na CNN jijini London juzi, alisema Tanzania imefanya operesheni nyingi dhidi ya majangili na kuhimiza haja ya mataifa makubwa kusaidia juhudi za kupambana na ujangili huo.
Akijibu maswali ya Christiane Amanpour wa CNN, Rais alitaka dunia kuungana kusimamisha biashara ya pembe za ndovu.

Alieleza kuwa hatua hiyo itaondoa kichocheo cha mtu kuwaua wanyama hao
Alieleza kuwa wakati wa uhuru walikuwepo tembo 350,000 kabla ya kuibuka wimbi la ujangili mkubwa ulioiachia nchi tembo 13,000 pekee.

AHADI YA MSAADA 
Akijibu swali kama kuna ahadi yoyote aliipata katika mkutano juu ya ulinzi wa wanyama pori uliofanyika London juzi, Rais Kikwete aliitaja Canada kuwa imeahidi kutoa Dola milioni mbili, wakati serikali ya Uingereza imeahidi kutoa msaada.

ALICHOTARAJIA
Alieleza kuwa kitu muhimu kwake na viongozi wa Afrika ni kufahamisha kuwa ili kuupiga vita ujangili kunahitajika rasilimali watu, kuwajengea uwezo askari wa wanyama pori wa kulinda wanyama.
Rais alisema alikuwa anategemea nchi zilizoendelea hasa Uingereza na Marekani kusaidia upande wa mafunzo ya askari wa wanyama pori na pia kuwapatia vifaa.

Alitaja silaha, magari na vyombo vyenye uwezo wa kufanya uchunguzi na kwamba ndicho alichotegemea kutoka kwenye mkutano huo na kwamba amepata ahadi za msaada.
AKIBA YA MENO
Rais Kikwete alisema Tanzania ina karibu tani 112 za pembe za ndovu ambazo haijajua itazifanya nini kwa sababu nchi ilizoea kuomba idhini ya kuziuza hatua ambayo inahitaji kuangaliwa upya.

UMASKINI
Akijibu swali kuhusu kukua kwa uchumi kwa kiasi kikubwa kulinganisha na nchi nyingine katika kipindi cha miaka michache iliyopita lakini nchi ikiwa na maskini wanaoishi kwenye ufukara, alisema “uchumi unakua kwa asilimia 70 lakini umasikini unapungua kwa asilimia 2.0” akiongeza kuwa mchango huo wa ukuaji wa asilimia 7.0 umetokana na sekta ya mawasiliano na usafiri.  
Chanzo: Nipashe