MAKOCHA wa timu za Taifa za Tanzania
(Taifa Stars) na Burundi (Intamba Mu Rugamba), Salum Mayanga na mwenzake
Niyungeko Alain Olivier wameahidi burudani ya nguvu kwenye mechi yao
itakayochezwa kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo ya kirafiki ambayo ni
sehemu ya maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar itachezeshwa na
refa Anthony Ogwayo kutoka Kenya na itaanza saa 10 kamili jioni.
Ogwayo atasaidiwa na Gilbert
Cheruiyot na Oliver Odhiambo wote pia kutoka Kenya.
Mwamuzi wa mezani atakuwa Israel
Mujuni wa Tanzania wakati Kamishna ni Charles Ndagala.