Wednesday, July 16, 2014

GARETH BALE LEO ATIMIZA MIAKA 25 AKIWA NDANI YA REAL MADRID


 
Gareth Bale
 


Kuhusu yeye binafsi
Full name

Gareth Frank Bale
Date of birth
16 July 1989 (age 25)
Place of birth
Cardiff, Wales
Height
1.83 m (6 ft 0 in)
Playing position
Timu ya sasa
Current team
Number
11
Timu za Vijana
2005–2006
Timu za ukubwa
Years
Team
  Mechi
(Goli)
2006–2007
40
(5)
2007–2013
146
(42)
2013–
27
(15)
Timu ya Taifa
2005–2006
7
(1)
2006
1
(1)
2006–2008
4
(2)
2006–
44
(12)

AFRIKA KUSINI YAWASILI KUIVAA SERENGETI BOYS


tff_LOGO1Afrika Kusini (Amajimbos) imewasili nchini kuikabili Tanzania (Serengeti Boys) katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 itakayochezwa keshokutwa (Julai 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.
Timu hiyo yenye msafara wa watu 37 ilitua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jana usiku (Julai 15 mwaka huu) na imefikia hoteli ya Sapphire. Amajimbos itafanya mazoezi leo saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Azam Complex.
Waamuzi watakaochezesha mechi hiyo kutoka Shelisheli wakiongozwa na Allister Barra tayari wamewasili nchini. Kamishna wa mechi hiyo ni Andriamiasasoa Doda Nirimboavonjy kutoka Madagascar.
Makocha wa timu za Seregenti Boys na Amajimbos pamoja na manahodha wao watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kesho (Julai 17 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Kiingilio katika mechi hiyo ni sh. 2,000. Tiketi zitauzwa uwanjani katika magari maalumu siku ya mechi.
SAMATA, ULIMWENGU WATUA, MWINYI KAZIMOTO KESHO
Washambuliaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wamewasili nchini leo asubuhi (Julai 16 mwaka huu) kutoka Tunisia kujiunga na Taifa Stars kwa ajili ya mechi dhidi ya Msumbiji itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Wachezaji hao wamefikia hoteli ya Courtyard, Seaview Upanga na leo (Julai 16 mwaka huu) watafanya mazoezi kwa programu maalumu waliyopewa na Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij wakati wakiwasubiri wenzao.
IMG_0750Naye kiungo Mwinyi Kazimoto anayecheza mpira wa miguu katika klabu ya Almarhiya ya Qatar atawasili nchini kesho (Julai 17 mwaka huu) saa 1.30 asubuhi kwa ndege ya Qatar Airways.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itawasili Dar es Salaam kesho (Julai 17 mwaka huu) saa 3.20 asubuhi kwa ndege ya Fastjet kutoka Mbeya tayari kwa maandalizi ya mwisho kabla ya kuivaa Msumbiji.

RAIS MALINZI KUZUNGUMZA NA WAANDISHI
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atakuwa na mkutano na waandishi wa habari Ijumaa (Julai 18 mwaka huu).

Thursday, July 10, 2014

SIMBA YAMNASA HUSSEIN SHARRIF KUTOKA MTIBWA

Simba Wekundu wa Msimbazi, Simba wamekamilisha usajili wa kipa namba moja wa Mtibwa Sugar, Hussein Sharrif `Iker Casillas` na kumsainisha mkataba wa miaka miwili.
Kwa muda mrefu Simba ilionesha nia ya kumsajili mlinda mlango huyo bora wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita, lakini ilimkosa mara kadhaa na sasa ndoto zimetimia.
Casillas aliyekuwa tegemeo katika klabu ya  Mtibwa Sugar ameungana na makipa Ivo Mapunda na Abuu Hashim katika kikosi cha Simba.


SERENGETI BOYZ VS AFRICA KUSINI AZAM COMPLEX

index
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boyz) inacheza mechi ya kujipima nguvu kesho (Julai 11 mwaka huu) dhidi ya Azam U-20 kwenyeUwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Mechi hiyo ambayo ni maalumu kwa benchi la ufundi la Serengeti Boyz likiongozwa na kocha Hababuu Ali Omari kuangalia kikosi chao itaanza saa 2 kamili asubuhi.
Serengeti Boyz itacheza mechi yake ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika dhidi ya Afrika Kusini (Amajimbos) siku ya Ijumaa, Julai 18 mwaka huu kwenye uwanja huo huo wa Azam Complex kuanzia saa 10 kamili jioni.
Wachezaji wanaounda kikosi cha Serengeti Boyz ni Abdallah Shimba, Abdulrasul Bitebo, Abutwalibu Mshery, Adolf Bitegeko, Ally Mabuyu, Ally Mnasi, Amin Noren, Athanas Mdamu, Badru Othman, Baraka Baraka, Hatibu Munishi na Issa Athuman.
Wengine ni Juma Yusuf, Kelvin Faru, Kelvin Kamalamo, Martin Luseke, Mashaka Ngajilo, Mechata Mnata, Mohamed Abdallah, Mussa Vicent, Nazir Barugire, Omary Omary, Omary Wayne, Prosper Mushi, Seif Seif na Yahya Hafidh.

Wednesday, July 9, 2014

STARS, MSUMBIJI KIINGILIO 7,000/=, TIKETI KWA M-PESA.

TFF-MPESA-MALIPOKiingilio cha chini cha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 7,000.
Tiketi zinapatikana kwa mfumo wa elektroniki kupitia M-PESA. Kiingilio hicho kwa ajili ya viti vya rangi ya rangi ya chungwa, kijani na bluu. Viingilio katika maeneo mengine vitatangazwa baadaye.
TFF-TANZANIA-MSUMBIJIMshabiki ili apate tiketi anatakiwa kutumia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha bonyeza 4, ingiza namba ya kampuni 173399 kisha weka 7000 kwenye namba ya kumbukumbu ya malipo, na weka
7000 kama kiasi cha bei ya tiketi na mwisho weka namba yao ya siri.
Baada ya hapo utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo kwa ajili ya kuchukulia tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.
TFF-MPESAVituo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illutions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).
Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na ofisi za TFF (PPF Tower).
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

VPL:LIGI KUU KUANZA SEPTEMBA 20


Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu wa 2014/2015 itaanza kutimua vumbi Septemba 20 mwaka huu.
VPL_2013-2014-FPAwali michuano hiyo ilikuwa ianze Agosti 24 mwaka huu, lakini Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limelazimika kuisogeza mbele kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupitisha michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame).
Michuano ya Kombe la Kagame inayoshirikisha mabingwa wa nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) itafanyika Agosti mwaka huu nchini Rwanda.
Timu 14 zitashiriki Ligi Kuu msimu huu. Timu hizo ni mabingwa watetezi Azam, Coastal Union, JKT Ruvu Stars, Kagera Sugar, Mbeya City, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Ndanda FC, Polisi Morogoro, Ruvu Shooting, Simba, Stand United, Tanzania Prisons na Yanga.
Ratiba ya ligi hiyo itatolewa mwezi mmoja kabla ya michuano hiyo kuanza kutimua vumbi.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Friday, July 4, 2014

ROBO FAINALI KOMBE LA DUNIA

FULECO_NA_BRAZUCA
RATIBA
ROBO FAINALI
IJUMAA, JULAI 4 ,2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
1900
France v Germany [57]
ROBO FAINALI
Estadio do Maracanã.
2300
Brazil v Colombia [58]
ROBO FAINALI
Estadio Castelão.
JUMAMOSI, JULAI 5, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
1900
Argentina v Belgium [59]
ROBO FAINALI
Nacional, Brasilia.
2300
Netherlands v Costa Rica [60]
ROBO FAINALI
Arena Fonte.
NUSU FAINALI
JUMANNE, JULAI 8, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
2300
Mshindi 57 v Mshindi 58 [61]
NUSU FAINALI
Estadio Mineirão
JUMATANO, JULAI 9, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
2300
Mshindi 59 Mshindi 60 [62]
NUSU FAINALI
Arena Corinthians.
MSHINDI WA TATU
JUMAMOSI, JULAI 12, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
2300
Aliefungwa 61 v Aliefungwa 62
MSHINDI WA 3
Nacional, Brasilia.
FAINALI
JUMAPILI, JULAI 13, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
2200
Mshindi Mechi 61 v Mshindi Mechi 62
FAINALI
Estadio do Maracanã.

BRAZIL-KIKOSI
Uso kwa Uso
Timu hizi zimekutana mara 25 na Brazil kushinda mara 15 Colombia 2 na Sare 8.
REFA: Carlos Ve
lasco [Spain]
KOMBE LA DUNIA
RATIBA
Saa za Bongo
VIKOSI VINATARAJIWA:
Brazil: Cesar, Marcelo, Silva, Alves, Luiz, Paulinho, Fernandinho, Hulk, Neymar, Fred, Willian.
Colombia: Ospina; Armero, Yepes, Zapata, Zunjiga; Guarin, Sanchez, Vargas, Martinez, Rodriguez; Teofilo.