Saturday, August 9, 2014

MTIBWA SUGAR 2-0 AZAM KIKOSI CHA PILI TAMASHA LA MATUMAINI

Timu ya Mtibwa Sugar imefanikiwa kukichalaza kikosi cha pili cha Azam fc mabao 2-0 dhidi ya katika mechi maalumu ya kirafiki ya Tamasha la Usiku wa Matumaini usiku huu uwanja wa Taifa, uliopo maeneo ya Chang’ombe, jijini Dar es salaam.
Kwa ushindi huo, wakata miwa wa mashamba ya Manungu Turiani Mkoani Morogoro wamefanikiwa kutwaa Ngao ya Matumaini.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa maalumu kwa kocha mkuu wa Mtibwa, Mecky Mexime kuonesha wachezaji wake jinsi walivyoiva, wachezaji wawili wakongwe, Musa Hassan Mgosi na Vicent Barnabas walionesha kandanda l
a kuvutia na kudhihirisha kuwa utu uzima dawa.
Baada ya mechi ya leo , kikosi hicho cha Azam kitasafiri muda wowote kuelekea mjini Kigali  nchini Rwanda kikifuata kikosi cha kwanza kinachoshiriki kombe la Kagame.

UJIO WA MAOFISA WA FIFA NCHINI.

imagesMaofisa wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wanawasili nchini kesho (Agosti 10 mwaka huu) kuangalia jinsi mchezo huo unavyoondeshwa nchini.
Ujumbe huo wa FIFA utakaokuwa na maofisa sita, baada ya ziara yake utashauri jinsi ya kuboresha uendeshaji huo katika kikao cha pamoja kati yake na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kitakachofanyika mwishoni mwa wiki ijayo.

Wednesday, August 6, 2014

SIMBA YA MNASA ABDI BANDA WA COASTAL UNION

CLUB ya Simba sc wazee wa Msimbazi wamefanikiwa kumsajili beki wa kushoto wa Coastal Union Abdi Banda baada ya kumuweka kwenye rada zake kwa muda mrefu.
Nyota huyo kinda mwenye uwezo wa kucheza nafasi zote za ulinzi, lakini beki ya kushoto ndio mahala pake haswaa , alisaini mkataba wa miaka mitatu jana na mara moja atajiunga na kikosi cha Simba kinachofanya mazoezi chini ya kocha mkuu, Mcroatia, Zdravko Logarusic.

Banda aliwahi kuripotiwa kuwindwa na Yanga katika dirisha dogo la usajili mwaka huu, lakini ilishindikana kwasababu alikuwa na mkataba na wagosi wa kaya na viongozi wa klabu hiyo walilalamika kitendo cha wanajangwani kumrubuni kijana huyo.

YANGA WAISHANGA CECAFA KUWEKA PEMBENI.

UONGOZI wa klabu ya Young Africans leo umefanya mkutano na waandishi wa habari juu na kusema kilichofanywa na waandaji wa michuano ya Kombe la Vilabu Bingwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuiondoa timu isishiriki ni cha kushangaza sana na kinadidimiza soka kwa ujumla.

Katibu Mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu amesema walipata barua ya mwaliko wa kushiriki mashindano tarehe 25/7/2014 na kudhibitisha kushiriki michuano hiyo kwa kuandika barua iliyokwenda TFF na kisha wao kuiwasilisha kwa CECAFA.

Tuesday, August 5, 2014

AZAM FC YACHUKUA NAFASI YA YANGA KAGAME CUP 2014 BAADA YA YANGA SC KUSUASUA.

BARAZA la vyama vya mpira wa miguu Afrika Mashariki na kati, CECAFA limeiengua rasmi klabu Yanga kushiri kombe la Kagame 2014 na nafasi yake imechukuliwa na mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc.
Tangu awali, CECAFA walitoa taarifa kuwa Azam watapewa nafasi ya upendeleo katika michuano hiyo inayoanza kushika kasi Agosti 8 mwaka huu, mjini Kigali nchini Rwanda, lakini mpaka jana wana Lambalamba walikuwa hawana taarifa rasmi.
azam-vs-yanga
Yanga sc ndio walitakiwa kushiriki michuano hiyo, lakini waliamua kupeleka kikosi B ambapo CECAFA ilikikataa na kuitaka timu hiyo ya makutano ya Twiga na Jangwani, Kariokoo jijini Dar es salaam ipeleke kikosi cha kwanza pamoja na kocha mkuu, Mbrazil Marcio Maximo.
Lakini Baada ya Yanga sc kuenguliwa kushiriki michuano ya klabu bingwa kwa ukanda wa Afrika mashariki na kati , maarufu kama Kombe la Kagame, kwa kugoma kupelekea kikosi cha kwanza kama walivyoagizwa, Shirikisho la soka Tanzania TFF, limesema klabu hiyo ina haki kutoshiriki mashindano kama inaona haijajiandaa.
Boniface Wambura Afisa habari na mawasiliano wa TFF, Mgoyo huu mchana huu ameumbia mtandao wa mkali dimba tz kuwa klabu inapokuwa bingwa, hakuna kanuni inayoibana kwamba lazima ishiriki mashindo fulani, bali kama wanaona hawapo tayari wanaweza kuwasiliana na TFF, halafu klabu nyingine inatafutwa.

MALINZI ATUMA RAMBIRAMBI MSIBA WA MAKAMU WA RAIS FIFA

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Shrikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Sepp Blatter kutokana na kifo cha makamu wake mwandamizi Julio Grondora.
julio1 Amesema yeye binafsi na jamii ya mpira wa miguu Tanzania kwa ujumla wanaomboleza msiba wa Grondora ambaye pia alikuwa Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Argentina (AFA).
 Ameongeza kuwa Grondora alikuwa mtumishi mwandamizi wa mpira wa miguu, kwani alijitoa katika kuutumikia mpira wa miguu, na mchango wake katika maendeleo ya mchezo huo utaendelea kukumbukwa wakati wote.
 Rais Malinzi amesema familia ya mpira wa miguu nchini Argentina imepata pigo, na ametoa pole kwa familia ya marehemu, AFA na familia nzima ya FIFA na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
 Bwana ametoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe. Amina.

Monday, August 4, 2014

WASIWASI MCHEZO UMEIGHARIMU TAIFA STARS- NOOIJ

KOCHA TAIFASTARSKocha wa Taifa Stars, Mart Nooij amesema moja ya sababu za kikosi chake kupoteza mechi dhidi ya Msumbiji (Mambas) ni wachezaji wake kucheza kwa wasiwasi katika kipindi cha kwanza.

Taifa Stars iliruhusu bao la kwanza sekunde chache kabla ya kumalizika kipindi cha kwanza katika mechi ya marudiano ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kutafuta tiketi ya kucheza hatua ya makundi iliyochezwa leo (Agosti 3 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa wa Zimpeto hapa Maputo.
KOCHA TAIFASTARS
Bao hilo katika mechi hiyo iliyomalizika kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-3 lilifungwa kwa kichwa na mshambuliaji Josemar Machaisse.

Nooij alisema wasiwasi katika kipindi cha kwanza ndio ulioipa Msumbiji fursa ya kutawala mechi hiyo katika kipindi hicho na kukimalizia ikiwa mbele kwa bao hilo la mshambuliaji huyo wa klabu ya Bravos de Maquis ya Angola.

Alisema timu yake ilitulia kipindi cha pili baada ya kumuingiza Amri Kiemba badala ya Khamis Mcha. Pia alilalamikia bao ambalo Taifa Stars ilifunga dakika ya 16 kupitia kwa John Bocco lakini likakataliwa na mwamuzi Dennis Bate kutoka Uganda.

Aliongeza kuwa mchezaji Elias Pelembe aliyeifungia Msumbiji bao la pili dakika ya 83 kwa mpira wa adhabu nje ya eneo la hatari ndiye aliyemaliza mchezo huo. Pia ni mchezaji huyo aliyebadili matokeo ya mchezo wa kwanza jijini Dar es Salaam ambapo Msumbiji ilisawazisha dakika tatu kabla ya filimbi ya mwisho.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, na ambayo ilicheza vizuri kipindi cha pili ilipata bao lake dakika ya 78 na Mbwana Samata kwa shuti la pembeni akiwa nje ya eneo la hatari na kumshinda kipa Ricardo Campos.
Matokeo hayo yameipeleka Msumbiji katika kundi C lenye timu za Cape Verde, Niger na Zambia. Mechi za hatua ya makundi kutafuta tiketi ya kucheza fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco zitaanza kuchezwa mwezi ujao.

Mechi hiyo ndiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya Tanzania na Msumbiji itakayoingia hatua ya makundi ya michuano ya Afrika kwa ajili ya kutafuta tiketi za Fainali itakayofanyika mwakani nchini Morocco.

Katika mechi ya kwanza iliyochezwa jijini Dar es Salaam wiki mbili zilizopita timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2. Timu itakayosonga mbele itaingia kwenye kundi lenye timu za Cape Verde, Niger na Zambia.

Taifa Stars inarejea Dar es Salaam kesho (Agosti 4 mwaka huu) saa 8 mchana kwa ndege ya Air Tanzania.

Kikosi cha Stars kilipangwa hivi; Deogratias Munishi, Said Moradi, Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Nadir Haroub, Erasto Nyoni, Mwinyi Kazimoto, Mcha Khamis/Amri Kiemba, John Bocco/Simon Msuva, Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu/Mrisho Ngasa