Wednesday, August 13, 2014

TFF YASEMA HAITAMBUI UONGOZI MPYA COASTAL UNION.

SHIRIKISHO la Soka wa nchini-TFF limedai kutotambua mabadiliko ya uongozi ndani ya Coastal Union yanayodaiwa kufanywa na mkutano wa wanachama wa klabu hiyo uliofanyika hivi karibuni. 

Katika taarifa ya shirikisho hilo iliyotumwa na Ofisa Habari wake
Boniface Wambura, TFF imesema wao wanatambua uongozi wa Coastal Union uliochaguliwa na mkutano wa uchaguzi wa klabu na ndio wataendelea kufanya nao kazi, na sio uongozi mwingine wowote ule. Shirikisho hilo limewakumbusha wanachama wakewakiwemo Coastal Union kuheshimu katiba ya TFF pamoja na katiba zao, kwani hazitambui mapinduzi ya uongozi wala kamati za muda za utendaji. TFF inafanya kazi za kamati za utendaji zilizopatikana kwa njia ya uchaguzi tu. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa tayari TFF imepokea barua kutoka kwa Kaimu Mwenyekiti wa Coastal Union, Steven Mnguto ikilalamikia kusimamishwa kwake na wanalifuatilia suala hilo kwa kina, na ikibainika kuwa kuna viongozi wamehusika katika mapinduzi hayo watafikishwa katika vyombo husika kwa hatua zaidi.

Saturday, August 9, 2014

MTIBWA SUGAR 2-0 AZAM KIKOSI CHA PILI TAMASHA LA MATUMAINI

Timu ya Mtibwa Sugar imefanikiwa kukichalaza kikosi cha pili cha Azam fc mabao 2-0 dhidi ya katika mechi maalumu ya kirafiki ya Tamasha la Usiku wa Matumaini usiku huu uwanja wa Taifa, uliopo maeneo ya Chang’ombe, jijini Dar es salaam.
Kwa ushindi huo, wakata miwa wa mashamba ya Manungu Turiani Mkoani Morogoro wamefanikiwa kutwaa Ngao ya Matumaini.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa maalumu kwa kocha mkuu wa Mtibwa, Mecky Mexime kuonesha wachezaji wake jinsi walivyoiva, wachezaji wawili wakongwe, Musa Hassan Mgosi na Vicent Barnabas walionesha kandanda l
a kuvutia na kudhihirisha kuwa utu uzima dawa.
Baada ya mechi ya leo , kikosi hicho cha Azam kitasafiri muda wowote kuelekea mjini Kigali  nchini Rwanda kikifuata kikosi cha kwanza kinachoshiriki kombe la Kagame.

UJIO WA MAOFISA WA FIFA NCHINI.

imagesMaofisa wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wanawasili nchini kesho (Agosti 10 mwaka huu) kuangalia jinsi mchezo huo unavyoondeshwa nchini.
Ujumbe huo wa FIFA utakaokuwa na maofisa sita, baada ya ziara yake utashauri jinsi ya kuboresha uendeshaji huo katika kikao cha pamoja kati yake na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kitakachofanyika mwishoni mwa wiki ijayo.

Wednesday, August 6, 2014

SIMBA YA MNASA ABDI BANDA WA COASTAL UNION

CLUB ya Simba sc wazee wa Msimbazi wamefanikiwa kumsajili beki wa kushoto wa Coastal Union Abdi Banda baada ya kumuweka kwenye rada zake kwa muda mrefu.
Nyota huyo kinda mwenye uwezo wa kucheza nafasi zote za ulinzi, lakini beki ya kushoto ndio mahala pake haswaa , alisaini mkataba wa miaka mitatu jana na mara moja atajiunga na kikosi cha Simba kinachofanya mazoezi chini ya kocha mkuu, Mcroatia, Zdravko Logarusic.

Banda aliwahi kuripotiwa kuwindwa na Yanga katika dirisha dogo la usajili mwaka huu, lakini ilishindikana kwasababu alikuwa na mkataba na wagosi wa kaya na viongozi wa klabu hiyo walilalamika kitendo cha wanajangwani kumrubuni kijana huyo.

YANGA WAISHANGA CECAFA KUWEKA PEMBENI.

UONGOZI wa klabu ya Young Africans leo umefanya mkutano na waandishi wa habari juu na kusema kilichofanywa na waandaji wa michuano ya Kombe la Vilabu Bingwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuiondoa timu isishiriki ni cha kushangaza sana na kinadidimiza soka kwa ujumla.

Katibu Mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu amesema walipata barua ya mwaliko wa kushiriki mashindano tarehe 25/7/2014 na kudhibitisha kushiriki michuano hiyo kwa kuandika barua iliyokwenda TFF na kisha wao kuiwasilisha kwa CECAFA.

Tuesday, August 5, 2014

AZAM FC YACHUKUA NAFASI YA YANGA KAGAME CUP 2014 BAADA YA YANGA SC KUSUASUA.

BARAZA la vyama vya mpira wa miguu Afrika Mashariki na kati, CECAFA limeiengua rasmi klabu Yanga kushiri kombe la Kagame 2014 na nafasi yake imechukuliwa na mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc.
Tangu awali, CECAFA walitoa taarifa kuwa Azam watapewa nafasi ya upendeleo katika michuano hiyo inayoanza kushika kasi Agosti 8 mwaka huu, mjini Kigali nchini Rwanda, lakini mpaka jana wana Lambalamba walikuwa hawana taarifa rasmi.
azam-vs-yanga
Yanga sc ndio walitakiwa kushiriki michuano hiyo, lakini waliamua kupeleka kikosi B ambapo CECAFA ilikikataa na kuitaka timu hiyo ya makutano ya Twiga na Jangwani, Kariokoo jijini Dar es salaam ipeleke kikosi cha kwanza pamoja na kocha mkuu, Mbrazil Marcio Maximo.
Lakini Baada ya Yanga sc kuenguliwa kushiriki michuano ya klabu bingwa kwa ukanda wa Afrika mashariki na kati , maarufu kama Kombe la Kagame, kwa kugoma kupelekea kikosi cha kwanza kama walivyoagizwa, Shirikisho la soka Tanzania TFF, limesema klabu hiyo ina haki kutoshiriki mashindano kama inaona haijajiandaa.
Boniface Wambura Afisa habari na mawasiliano wa TFF, Mgoyo huu mchana huu ameumbia mtandao wa mkali dimba tz kuwa klabu inapokuwa bingwa, hakuna kanuni inayoibana kwamba lazima ishiriki mashindo fulani, bali kama wanaona hawapo tayari wanaweza kuwasiliana na TFF, halafu klabu nyingine inatafutwa.

MALINZI ATUMA RAMBIRAMBI MSIBA WA MAKAMU WA RAIS FIFA

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Shrikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Sepp Blatter kutokana na kifo cha makamu wake mwandamizi Julio Grondora.
julio1 Amesema yeye binafsi na jamii ya mpira wa miguu Tanzania kwa ujumla wanaomboleza msiba wa Grondora ambaye pia alikuwa Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Argentina (AFA).
 Ameongeza kuwa Grondora alikuwa mtumishi mwandamizi wa mpira wa miguu, kwani alijitoa katika kuutumikia mpira wa miguu, na mchango wake katika maendeleo ya mchezo huo utaendelea kukumbukwa wakati wote.
 Rais Malinzi amesema familia ya mpira wa miguu nchini Argentina imepata pigo, na ametoa pole kwa familia ya marehemu, AFA na familia nzima ya FIFA na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
 Bwana ametoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe. Amina.