Tuesday, August 19, 2014

MAKOCHA WA COPA COCA-COLA KUPIGWA MSASA JIJINI DAR

Makocha wa kombaini za mikoa zitakazoshiriki Copa Coca-Cola mwaka 2014 pamoja na waamuzi vijana wa michuano hiyo watashiriki kozi ya ukocha na uamuzi itakayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Agosti 25 hadi 29 mwaka huu.
Kozi hiyo itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Agosti 25 hadi 29 mwaka huu ikiwa ni sehemu ya maandalizi michuano ya Copa Coca-Cola ngazi ya Taifa itakayochezwa Septemba mwaka huu.

Makocha watakaoshiriki kozi hiyo na mikoa yao kwenye mabano ni Ahmed Simba (Mwanza), Ally Kagire (Kagera), Aloyce Mayombo (Pwani), Andrew Zoma (Tabora), Anthony Mwamlima (Mbeya), Athuman Kairo (Morogoro), Bakari Ali (Kaskazini Pemba) na Charles Mayaya (Shinyanga).

Fidelis Kalinga (Iringa), Gabriel Gunda (Singida), Hafidh Muhidin Mcha (Kusini Pemba), Hamis Mabo (Kigoma), John William (Geita), Joseph Assey (Shinyanga), Joseph Haley (Manyara), Jumanne Ntambi (Kilimanjaro), Leonard Jima (Ruvuma), Madenge Omari (Mara), Mohamed Muya (Dodoma), Nicholas Kiondo (Ilala) na Nurdin Gogola (Temeke).
Osuri Kosuli (Simiyu), Peter Amas (Arusha), Ramadhan Abdulrahman Ramadhan (Mjini Magharibi), Renatus Mayunga (Kinondoni), Samwel Moja (Lindi), Seif Bakari (Katavi), Shaweji Nawanda (Mtwara), Sheha Khamis Rashid (Kaskazini Unguja), Tigana Lukinjo (Njombe), Yusuf Ramadhan Hamis (Kusini Unguja), Zahoro Mohamed (Tanga) na Zakaria Mgambwa (Rukwa).

Waamuzi vijana watakaoshiriki kozi hiyo chini ya Mkufunzi wa FIFA, Felix Tangawarima wa Zimbabwe ni 33. Kwa upande wa ukocha Mkufunzi ni Ulric Mathiott kutoka Shelisheli.

DR MSOLLA IONYA SIMBA NA YANGA KUELEKEA VPL

KOCHA wa zamani wa Taifa Stars ambaye sasa ni Daktari, Mshindo Msolla amesema timu za Simba na Yanga zisijidanganye kwa kucheza mechi za kirafiki na timu za Zanzibar kama sehemu ya kujipima kutokana na timu hizo kuwa na uwezo wa chini ukilinganisha na timu za Bara.
Simba ya Patrick Phiri iko kambini Unguja na Yanga ya Marcio Maximo jana Jumatatu imetua Pemba. Msolla amesema Azam imejiweka kwenye nafasi nzuri timu anazocheza nazo huko Rwanda ni za kiwango cha kimataifa timu hizo zitaweza kuwapima vizuri na kuwasaidia pia wakirejea watakuwa na muda wa kama wiki tatu kurekebisha makosa yao.
Simba na Yanga wao nimesikia wameweka kambi Zanzibar napata wasiwasi kama wataweza kupata mechi kubwa za kirafiki kutokana na muda kwenda wasijidanganye kucheza na timu za Zanzibar kwani timu za kule ziko chini, ligi yao si ya ushindani kama ya Bara.Wakishindwa kuwa na mechi kubwa za kirafiki watapata shinda mwanzo wa msimu kwani watakuwa hawajakomaa vizuri, pia katika mechi hizo lazima wazingatie ngazi waliyopo, kwa mfano Simba ilicheza na Zesco wakati ikiwa kwenye ngazi za awali, ile haikuwa kipimo tosha.

POLISI MORO WAJIGAMBA KUHUSU MRWANDA NA MACHAKU

POLISI Morogoro imeweka wazi kombinesheni ya washambuliaji wao wapya, Danny Mrwanda, Salum Machaku na Six Mwasekaga iko vizuri na wanachokifanya sasa ni kuwatengenezea mfumo wa kisasa utakaowaunganisha na viungo pamoja na mabeki wawatengenezee nafasi nyingi za mabao.
Benchi la ufundi la kikosi hicho chini ya kocha mkuu,Adolf Rishard na msaidizi wake, John Tamba wanawatengeneza mfumo ambao utawafanya mabeki na viungo kuwatengenezea washambuliaji hao nafasi nyingi za mabao.
Tamba amesema Kombinesheni ya Machaku, Mrwanda na Mwasekaga iko vizuri na ili kuwaongezea ubora, tunatengeneza mfumo mzuri wa kisasa utakaokuwa na muunganiko kunzia beki, kiungo ambao watawapa nafasi nzuri za kufunga washambuliaji.”

RUVU JKT WAMTWAA HARUMA SHAMTE MKATABA WA MWAKA1

MAAFANDE wa JKT Ruvu wamekamilisha usajili wa wachezaji watatu kati ya wengi waliokuwa wanafanya majaribio chini ya kocha mkuu, Fredy Felix Minziro.

Beki wa kulia aliyeichezea Simba sc msimu uliopita, Haruna Ramadhan Shamte amesajiliwa na maafane hao na kusaini mkataba mwa mwaka mmoja.

KOZI YA UKOCHA LESENI A KUFANYIKA SEPTEMBA 4

Waamuzi wanaotarajia kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu watafanya mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) mwezi ujao.
Mtihani huo utahusisha waamuzi wa daraja la kwanza (class one) wakiwemo pia wale wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Mbali ya mtihani huo unaotarajiwa kufanyika kabla ya Septemba 10 mwaka huu, pia kutakuwa na semina kwa makamishna ambao watasimamia mechi za VPL na FDL.
 Hivyo waamuzi wote wanatakiwa kutumia muda uliobaki kufanya maandalizi kwa ajili ya mtihani huo.
KOZI YA UKOCHA LESENI A KUFANYIKA SEPTEMBA 4
Kozi ya ukocha wa Leseni A inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) itafanyika mara ya kwanza nchini, jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 4 mwaka huu. 
Mkufunzi wa kozi hiyo itakayofanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume atatoka CAF, na itamalizika Septemba 8 mwaka huu wakati ada ya ushiriki ni sh. 300,000.
Washiriki wa kozi hiyo ni wale wenye leseni B ya ukocha ya CAF. Fomu kwa ajili ya ushiriki wa kozi hiyo zinapatikana kwenye ofisi za TFF na tovuti ya TFF.

POLISI MORO, MTIBWA KUCHEZA MECHI YA TIKETI ZA ELEKTRONIKI

Timu za Mtibwa Sugar na Polisi Morogoro zinazojiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitacheza Jumamosi (Agosti 23 mwaka huu) mechi ya majaribio ya mfumo wa tiketi za elektroniki.
Mechi hiyo itafanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro kuanzia saa 10 jioni wakati kiingilio kitakuwa sh. 1,000.