Benchi la ufundi la kikosi hicho chini ya kocha mkuu,Adolf Rishard na msaidizi wake, John Tamba wanawatengeneza mfumo ambao utawafanya mabeki na viungo kuwatengenezea washambuliaji hao nafasi nyingi za mabao.
Tamba amesema Kombinesheni ya Machaku, Mrwanda na Mwasekaga iko vizuri na ili kuwaongezea ubora, tunatengeneza mfumo mzuri wa kisasa utakaokuwa na muunganiko kunzia beki, kiungo ambao watawapa nafasi nzuri za kufunga washambuliaji.”