Tuesday, December 16, 2014

LIGI KUU VODACOM TZ BARA DIMBA DEC 26 TIMU KUUMANA DIMBANI

Timu zinazoshiriki ligi kuu vodacom tanzania bara kila moja tayari imekamilisha usajili ili kuimarisha vikiosi vyao kwa ajili ya Raundi ya nane ya ligi hiyo.
LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Ijumaa Desemba 26
Simba v Kagera Sugar
Jumamosi Desemba 27
Mtibwa Sugar v Stand United               
Prisons v Coastal Union             
JKT Ruvu v Ruvu Shootings
Jumapili Desemba 28
Mbeya City v Ndanda FC            
Polisi Moro v Mgambo JKT          
Yanga v Azam FC   
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Mtibwa Sugar
7
4
3
0
10
3
7
15
2
Yanga
7
4
1
2
9
4
4
13
3
Azam FC
7
4
1
2
8
4
4
13
4
Coastal Union
7
3
2
2
8
6
2
11
5
Kagera Sugar
7
2
4
1
5
3
1
10
6
JKT Ruvu
7
3
1
3
7
7
0
10
7
Simba
7
1
6
0
7
6
1
9
8
Polisi Moro
7
3
2
2
6
7
-1
9
9
Mgambo JKT
7
3
0
4
4
7
-3
9
10
Stand United
7
2
3
2
5
9
-4
9
11
Ruvu Shooting
7
2
1
4
4
7
-3
7
12
Tanzania Prisons
7
1
3
3
5
6
-1
6
13
Ndanda FC
7
2
0
5
8
12
-4
6
14
Mbeya City
7
1
2
4
3
5
-2
5

SIMBA YAFUNGA USAJILI KWA KUMNASA BEKI WA MTIBWA HASSAN KESSY RAMADHANI

Wekundu wa Msimbazi Simba imetua nanga baada ya kufunga usajili wake wa dirisha dogo kwa kumsaini beki kijana wa kulia wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Hassan Ramadhani Kessy.
Kessy amesaini usiku huu Mkataba wa miezi 18 baada ya mvutano wa muda mrefu na klabu hiyo juu ya dau.
Zaidi ya mara tatu, Kessy alikwishakutana mezani na uongozi wa Simba SC bila kufikia maafikiano na baada ya mvutano huo uliodumu kwa takriban mwezi mzima, leo mambo yameisha.
Kaburu amesema kwamba baada ya kumpata Kessi wanadhani sasa kikosi chao kimekamilika na wanaelekeza nguvu zao katika maandalizi kwa ajili ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kessy anakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Simba SC katika dirisha dogo, baada ya Waganda beki Juuko Murushid na washambuliaji Dan Sserunkuma na Simon Sserunkuma.
Murushid amesaini miaka mitatu, wakati akina Sserunkuma wamesaini miaka miwili kila moja.
Simba SC imewatema Warundi kiungo Pierre Kwizera na mshambuliaji Amisi Tambwe aliyehamia kwa mahasimu, Yanga SC baada ya kuwasajili Waganda hao.
Simba SC ililazimika kuwatema Warundi hao ili kukidhi matakwa ya kanuni ya Usajili ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ya wachezaji watano wa kigeni.
Murushid na akina Sserunkuma wanaungana na Waganda wenzao, beki Joseph Owino na mshambuliaji Emmanuel Okwi kukamilisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni.

YANGA WAKALI KWELI KWELI YAMTUPIA VIRAGO EMERSON NA KIIZA

Baada ya Mvutano wa hapa na pale nani aachwe kati ya Emerson kiiza na Coutinho Yanga sasa imeamua kuwaacha kuwatupia virago Mbrazil, Emerson de Oliviera Roque na Mganda Hamis Kiiza na kumsajili mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Mrundi Amisi Tambwe.
Tambwe amesaini Mkataba wa mwaka mmoja baada ya kuachwa na klabu yake, Simba SC aliyoichezea msimu mmoja uliopita akitokea Vital’O ya Burundi.
Yanga SC imeamua kumuacha Mbrazil Emerson baada ya kushindwa kupata Hati yake ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC).
Tambwe anaungana na Mliberia, Kpah Sherman, Wanyarwanda Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Mbrazil Andrey Coutinho kukamilisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni Yanga SC.
Wakati dirisha la usajili limefungwa jana Saa 6:00 usiku.
Yanga SC imesajili jumla ya wachezaji watatu wapya baada ya kumuacha Emerson, mwingine ni Danny Mrwanda. 
Katika kipindi cha msimu mmoja, Tambwe ameichezea Simba SC jumla ya mechi 43 na kuifungia mabao 26.
Maisha yake yalianza kuwa magumu Simba SC baada ya ujio wa kocha Mzambia, Patrick Phiri kuchukua mikoba ya Mcroatia, Zdravko Logarusic.