Wednesday, April 24, 2013

TAFAKARI YA LEO 
TOMATH MULLER 
Taarifa kamili
Jina kamili”
Thomas Müller
Kuzaliwa”
13 September 1989 (age 23)
Mahali”
Weilheim, West Germany
Urefu”
1.86 m (6 ft 1 in)
Nafasi anayocheza”
Timu ya sasa
Current club
Number
25
Timu za vijana*
1993–2000
TSV Pähl
2000–2008
Timu ya Ukubwa*
Years
Team
Mechi
(Goli)
2008–2009
35
(16)
2008–sasa
131
(44)
Timu ya Taifa
2004–2005
6
(4)
2007
1
(0)
2008
1
(1)
2009–2010
6
(1)
2010–
41
(13)
AJIWEKA PEMBENI KAMATI YA FIFA
MJUMBE wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Nicolas Leoz kutoka Paraguay amejiuzulu wadhifa wake huo kutokana na kile alichodai kuwa na matatizo ya kiafya ikiwa ni siku chache kabla ya shirikisho hilo halijatangaza uchunguzi wa bakshishi katika michuano ya Kombe la Dunia. FIFA ilithibitisha kupokea barua ya Leoz mwenye umri wa miaka 84 ambaye pia ataachia ngazi wadhifa wake wa urais wa Shirikisho la Soka la Amerika Kusini-CONMEBOL. Leoz ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo mara kadhaa amekuwa mjumbe katika bodi ya FIFA kuanzia mwaka 1998 na amekuwa rais wa CONMEBOL kuanzia mwaka 1986. Katika barua yake Leoz amesisitiza kuwa uamuzi aliochukua ni binafsi kutokana na matatizo ya kiafya aliyonayo kwani hawezi kusafiri mara tano kwa mwaka kama ilivyokuwa zamani.


Ijapo kuwa matajiri wa london Man city wameonekana kuvutiwa na kiwango chake KLABU ya Paris Saint-Germain-PSG ya Ufaransa imemtengea mkataba mnono wa euro milioni 8.5 kwa msimu mshambuliaji nyota wa Napoli ya Italia Edinson Cavani. Imeripotiwa na vyombo vua habari nchini humo kuwa mkurugenzi wa michezo wa klabu ya PSG, Leonardo ameshafanya vikao kadhaa na wakala wa nyota huyo kuzungumzia uhamisho wake kutoka Napoli ambao unakaribia kufikia kiasi cha euro milioni 63. Mbali na PSG vilabu vingine vikubwa barani Ulaya ambavyo vimeonyesha nia ya kuhitaji sahihi ya nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay ni pamoja na Real Madrid, Manchester City na Chelsea. Cavani mwenye umri wa miaka 26 ana mkataba na Napoli mpaka 2015 ambao unamuwezesha kulipwa kiasi cha euro milioni 1.4 kwa msimu.
MKALI RONALDINHO APEWA UNAHODHA VS CHILE:;
RONALDINHO anatarajiwa kupewa unahodha wa timu ya taifa ya Brazil katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Chile hatua ambayo itamuweka katika nafasi nzuri ya kujumuishwa katika kikosi kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Shirikisho.
Kocha wa Brazil Luis Felipe Scolari ameonyesha matumaini yake kwa Ronaldinho ambaye amaewahi kunyakuwa tuzo ya mchzaji bora wa dunia mara mbili kwa kumpa unahodha kwenye mechi ya mwisho kabla hajatangaza kikosi cha michuano ya Kombe la Shirikisho.
Scolari tayari amebainisha kuwa kuna uwezekano akamchukua kati ya Ronaldinho au Kaka kwa ajili ya michuano hiyo itakayofanyika June mwaka huu. Kaka atakosa mchezo dhidi ya Chile kwasababu ni wachezaji wanaocheza katika vilabu vya Brazil peke ndio waliochaguliwa kwa ajili ya mchezo huo kirafiki kitendo ambacho kinampa nafasi kubwa kama akionyesha kiwango kizuri.
MUNICH YAITANDIKA BARCA 4-MTUNGI ANGALI MAMBO YA JANA
MABINGWA wa Ujerumani maarufu BUNDASLIGA, Bayern Munich wamejiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya fainali ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya baada ya kuitandika Barcelona 4-0 katika mchezo wa kwanzawa nusu fainali nchini Ujerumani. Mabao mawili ya Thomas Müller, na yale ya Mario Gomez na Arjen Robben yaliizamisha Barcelona ambayo ilikuwa na nyota wake wote wakutegemewa, akiwemo Messi ambaye alikosa michezo kadhaa kabla ya kuanzishwa usiku huu. Hii imekuwa mara ya kwanza kwa Barcelona kufungwa mabao 4-0 tangu mwaka 1997 walipofungwa na Dynamo Kiev ya Urusi mwaka 1997 kwenye hatua ya robo fainali ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya. Bayern Munich wametoka kutawazwa kuwa mabingwa wa Ujerumani wiki chache zilizopita na iwapo watafanikiwa kuiondosha Barcelona na kutinga hatua ya fainali ya michuano ya klabu bingwa, itakuwa fainali yao ya tatu kushiriki ndani ya miaka minne. Michuano hiyo itaendelea tena leo usiku ambapo mahasimu wa Barcelona, Real Madrid watakuwa na kibarua kizito pale itakapokaribishwa katika Uwanja wa Signal-Iduna-Park kukwaana na wenyeji Borussia Dortmund kwenye mchezo unaotaajiwa kuwa mgumu na wa kusisimua.
TAIFA STARS KUCHEZA MICHUANO YA COSAFA

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itashiriki michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayofanyika Julai mwaka huu nchini Zambia. Taifa Stars inashiriki michuano hiyo ya timu za Taifa za nchi wanachama wa COSAFA ikiwa timu mwalikwa. Nchi wanachama wa COSAFA ni Afrika Kusini, Angola, Botswana, Comoro, Lesotho, Madagascar, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Shelisheli, Swaziland, Zambia na Zimbabwe. Michuano hiyo itafanyika kuanzia Julai 6 hadi 21 mwaka huu katika miji ya Lusaka, Ndola na Kabwe. Ratiba ya makundi ya michuano hiyo itapangwa Mei 3 mwaka huu jijini Lusaka. Mara ya mwisho michuano hiyo ilifanyika miaka mitatu iliyopita. Hii itakuwa mara ya pili kwa Tanzania kushiriki michuano hiyo baada ya kucheza ya kwanza iliyofanyika mwaka 1996 nchini Zimbabwe. Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inatarajia kuingia kambini mwishoni mwa mwezi ujao kujiandaa kwa mechi ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech. Juni 16 mwaka huu Taifa Stars itacheza na Ivory Coast jijini Dar es Salaam katika mechi nyingine ya mchujo ya Kombe la Dunia wakati Juni mwishoni na Julai mwanzoni itacheza mechi ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) dhidi ya Uganda. Wakati huo huo, waandishi wa habari wanaotaka kuripoti michuano hiyo wanatakiwa kuwasilisha majina yao TFF kabla ya Aprili 27 mwaka huu ili maombi yao yatumwe COSAFA kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho (Accreditation).

Tuesday, April 23, 2013

KOCHA KIM ATANGAZA YOUNG TAIFA STARS
Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza timu ya pili ya Taifa (Young Taifa Stars) atakayoitumia kuangalia wachezaji ambao baadaye anaweza kuwajumuisha kwenye timu ya wakubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo (Aprili 23 mwaka huu) kabla ya kutaja kikosi hicho, Kim amesema timu hiyo ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliozinduliwa Aprili 4 mwaka huu ukilenga kuendeleza wachezaji.

Amesema timu hiyo inajumuisha wachezaji ambao wamepita umri wa kuchezea timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) na wakubwa ambao hawajapata fursa ya kuingia Taifa Stars, lakini atatumia Young Taifa Stars kuangalia uwezo wao.

“Timu hii ni kiungo kati ya vijana na wakubwa. Wengi wa wachezaji watakuwa vijana, lakini wakubwa wachache watapata fursa ya kuwemo ili kuangalia uwezo wao hata kama uko nyuma waliwahi kuchezea Taifa Stars. Lakini timu hii vilevile ni changamoto wa wachezaji wa Taifa Stars kuwa wapo wanaosubiri wazembee ili wachukue nafasi zao,” amesema.

Young Taifa Stars yenye wachezaji 30 itakuwa na kambi ya siku tano jijini Dar es Salaam kuanzia Mei 2 hadi 6 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa ni Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Ali Mustapha (Yanga) ambao ni makipa. Mabeki ni Kessy Hassan (Mtibwa Sugar), Kennan Ngoma (Barnsley FC, Uingereza), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), David Mwantika (Azam), Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Kagera Sugar), Waziri Salum (Azam), Samih Nuhu (Azam) na Emily Mgeta (Simba).

Viungo ni Haruna Chanongo (Simba), Edward Christopher (Simba), Mudathiri Yahya (Azam), William Lucian (Simba), Jonas Mkude (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Jimmy Shoji (JKT Ruvu), Abdallah Seseme (Simba), Ramadhan Singano (Simba), Farid Mussa (Azam) na Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Jerome Lambele (Ashanti United), Zahoro Pazi (JKT Ruvu), Twaha Hussein (Coastal Union), Abdallah Karihe (Azam) na Juma Luizio (Mtibwa Sugar).

AFRICAN LYON, JKT RUVU KUUMANA CHAMAZI
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho (Aprili 24 mwaka huu) kwa mechi moja kati ya wenyeji African Lyon na JKT Ruvu.

Mechi hiyo namba 165 itachezwa Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam chini ya usimamizi wa Kamishna Hamisi Kisiwa wa Dar es Salaam. Waamuzi wa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni ni Hashim Abdallah, Omari Kambangwa, Abdallah Selega na Said Ndege wote wa Dar es Salaam.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
VAN MAGOLI JEZI 20 APIGA TATU NA KUILETEA UBINGWA WA 20 MAN U:
Katika mechi ya jana Robin van Persie, amefanya kile ambacho wadau na mashabiki wa man u ambao waliondoa imani naye kuwa haufumanii nyavu lakini aliweza kudhihilisha kuwa yeye ni bora zaidi baada ya kutupia Bao Dakika za 2, 13 na 33 na, kufuatia kazi nzuri ya Nguli Ryan Giggs na Wayne Rooney, na kuwatwanga Aston Villa Bao 3-0 Uwanjani Old Trafford na kuipatia Manchester United Ubingwa wa BPL, Barclays Premier League huku wakiwa na Mechi 4 mkononi.
HISTORIA:
.Hii ni mara ya 4 kwa Man United kutwaa Ubingwa Uwanjani kwao Old Trafford
.Mara nyingine walizotwaa Ubingwa Old Trafford ni Mwaka 1999, 2002 na 2009
.Mwaka 2001 walitwaa Ubingwa wakiwa na Mechi 5 mkononi
.Msimu wa 1999/2000 walitwaa Ubingwa kwa pengo la Pointi 18
kwa sasa Van Persie  anaongoza Ufungaji Bora BPL akiwa na Bao 24 kwa mtukutu Luis suarez akiwa na mabao 23.
Huu ni Ubngwa wa 13, chini ya Sir Alex Ferguson, katika Miaka 21 ya Historia ya Ligi Kuu England.
MSIMAMO==BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE
NA
TIMU
P
GD
PTS
1
Man Utd
34
40
84
2
Man City
33
29
68
3
Arsenal
34
30
63
4
Chelsea
33
31
62
5
Tottenham
33
17
61
6
Everton
34
13
56
7
Liverpool
34
19
51
8
West Brom
33
-1
45
9
Swansea
33
1
42
10
West Ham
34
-7
42
11
Fulham
34
-8
40
12
Southampton
34
-7
39
13
Norwich
34
-20
38
14
Sunderland
34
-7
37
15
Stoke
34
-11
37
16
Newcastle
34
-17
37
17
Aston Villa
34
-27
34
18
Wigan
33
-23
31
19
QPR
34
-27
24
20
Reading
34
-28

24