Tuesday, August 19, 2014
KOZI YA UKOCHA LESENI A KUFANYIKA SEPTEMBA 4
Mbali ya mtihani huo unaotarajiwa kufanyika kabla ya Septemba 10 mwaka huu, pia kutakuwa na semina kwa makamishna ambao watasimamia mechi za VPL na FDL.
Hivyo waamuzi wote wanatakiwa kutumia muda uliobaki kufanya maandalizi kwa ajili ya mtihani huo.
KOZI YA UKOCHA LESENI A KUFANYIKA SEPTEMBA 4
Mkufunzi wa kozi hiyo itakayofanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume atatoka CAF, na itamalizika Septemba 8 mwaka huu wakati ada ya ushiriki ni sh. 300,000.
Washiriki wa kozi hiyo ni wale wenye leseni B ya ukocha ya CAF. Fomu kwa ajili ya ushiriki wa kozi hiyo zinapatikana kwenye ofisi za TFF na tovuti ya TFF.
Monday, August 18, 2014
SIMBA YAENDELEA NA TIZI ZANZIBAR
Simba wameweka kambi visiwani
Zanzibar (Unguja) chini ya kocha mkuu mpya, Mzambia, Patrick Phiri
akisaidiwa na kocha msaidizi, kiungo wa zamani wa klabu hiyo na timu ya
taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’, Suleiman Abdallah Matola ‘Veron’ na
kocha wa makipa, Idd Pazzi ‘Father’.
FIFA KUBORESHA MAKAO MAKUU YA TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) yaliyoko kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala ili
yawe katika kiwango cha kisasa ikiwa ni pamoja na kuwa na vitendea kazi
na miundombinu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa ofisi.
Hatua hiyo itaiwezesha TFF kuwa na
mazingira bora ya kufanya shughuli zake kwa ufanisi. Vilevile kupitia
programu zake mbalimbali ikiwemo ile ya Goal, FIFA imeahidi kushirikiana
na TFF katika kuendeleza mradi wa kiuchumi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu
ya Karume.
YANGA YATUA PEMBA KUWEKA CHIMBO LA VPL SEPT 20,2014
Msafara wa watu 35 ukiwa na wachezaji 27 na benchi la Ufundi 8 wa timu ya Young Africans
tayari umeshawasili Kisiwani Pemba kwa ajili ya maandalizi ya mwisho
kujiandaa na mikikimikiki ya Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2014/2015.
Kocha mkuuu Marcio Maximo na kikosi chake wamefikia katika hoteli ya
kitalii ya Pemba Misali iliyopo eneo la Wesha na watakua wakijifua kwa
muda wa takribani siku 10 kabla ya kurejea jijini Dar es salaam mwisho wa mwezi huu.

Kikosi
cha Young Africans kitakua kikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Gombani
mjini Chake Chake na siku ya alhamis wanataraji kucheza wa kwanza wa
kirafiki dhidi ya timu ya Chipukizi ya kisiwani Pemba.
Kulingana na program ya bench
la Ufundi kisiwani Pemba, Young Africans inatarajia kucheza michezo
mitatu ya kirafiki na timu za kutoka Visiwa vya Pemba na Unguja na
baadae kurejea Dar es salaam kwa michezo mwili ya kimataifa kabla ya
kucheza mchezo wa Ngao ya Hisani septemba 13, 2014.
Wachezaji waliondoka kuelekea Pemba ni:
Walinda Mlango:
Juma Kaseja, Ally Musatfa "Barthez" na Deogratias Munish "Dida"
Walinzi wa Pembeni:
Juma Abdul, Salum Telea, Oscar Joshua, Edwad Charles na Amos Abel
Walinzi wa Kati:
Kelvin Yondani, Nadir Haroub "Cannavaro", Rajab Zahir na Pato Ngonyani.
Viungo:
Mbuyu Twite, Said Juma "Makapu", Omega Seme, Hassan Dilunga, Haruna Niyonzima na Hamis Thabit.
Viungo wa Pembeni:
Saimon Msuva, Mrisho Ngasa, Nizar Khalfani na Andrey Coutinho.
Washambuliaji:
Geilson Santos "Jaja", Said Bahanuzi, Jerson Tegete, Hamis Kizza na Hussein Javu
Benchi la Ufundi walioko Kisiwani Pemba ni:
Kocha Mkuu : Marcio Maximo
Kocha wasaidizi Leonado Neiva, Salvatory Edward
Kocha wa Makipa: Juma Pondamali
Daktari wa timu: Dr Suphian Juma
Meneja wa timu: Hafidh Saleh
Mchua Misuli: Jaco Onyango
Mtunza Vifaa: Mahmod Omar "Mpogolo"
Saturday, August 16, 2014
MAN UNITED YAPOLEA KIPONDO NYUMBANI 2-1 SWANSEA CITY
MENEJA mpya wa klabu ya
Manchester United ameanza vibaya kampeni zake za Ligi Kuu baada ya
kushuhudia kikosi chake kikitandikwa mabao 2-1 dhidi ya Swansea city katika mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Old Trafford
mchana wa leo.
Wageni Swansea ndio waliokuwa wa kwanza kuchukuliwa wavu
wa United kwa bao lililofungwa na Ki Sung-yueng katika dakika ya 28
lakini bao hilo lilisawazishwa muda mfupi baada ya kuanza kipindi cha
pili kupitia kwa nahodha wake Wayne Rooney.
Swansea
walifunga bao lao la ushindi katika dakika ya 72 kupitia kwa Gyfi
Sigurdsson hivyo kuifanya timu hiyo kupoteza mchezo wake wa ufunguzi
nyumbani kwa mara ya kwanza toka mwaka 1972.
United walionekana
kushindwa kabisa kutengeneza mipango ya kusawazisha bao hilo hatua
ambayo mashabiki wake walionnekana kukata tamaa na kuanza kuondoka
mapema uwanjani kabla ya mchezo kumalizika.
Mashabiki wa United duniani
kote kabla ya mchezo walionekana kuwa na imani kubwa na kikosi chao toka
alipotua Van Gaal akichukua mikoba ya David Moyes ambaye alifanikiwa
kushinda mechi zake zote za kirafiki alizocheza.
Subscribe to:
Posts (Atom)


