Tuesday, August 19, 2014

RUVU JKT WAMTWAA HARUMA SHAMTE MKATABA WA MWAKA1

MAAFANDE wa JKT Ruvu wamekamilisha usajili wa wachezaji watatu kati ya wengi waliokuwa wanafanya majaribio chini ya kocha mkuu, Fredy Felix Minziro.

Beki wa kulia aliyeichezea Simba sc msimu uliopita, Haruna Ramadhan Shamte amesajiliwa na maafane hao na kusaini mkataba mwa mwaka mmoja.

KOZI YA UKOCHA LESENI A KUFANYIKA SEPTEMBA 4

Waamuzi wanaotarajia kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu watafanya mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) mwezi ujao.
Mtihani huo utahusisha waamuzi wa daraja la kwanza (class one) wakiwemo pia wale wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Mbali ya mtihani huo unaotarajiwa kufanyika kabla ya Septemba 10 mwaka huu, pia kutakuwa na semina kwa makamishna ambao watasimamia mechi za VPL na FDL.
 Hivyo waamuzi wote wanatakiwa kutumia muda uliobaki kufanya maandalizi kwa ajili ya mtihani huo.
KOZI YA UKOCHA LESENI A KUFANYIKA SEPTEMBA 4
Kozi ya ukocha wa Leseni A inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) itafanyika mara ya kwanza nchini, jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 4 mwaka huu. 
Mkufunzi wa kozi hiyo itakayofanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume atatoka CAF, na itamalizika Septemba 8 mwaka huu wakati ada ya ushiriki ni sh. 300,000.
Washiriki wa kozi hiyo ni wale wenye leseni B ya ukocha ya CAF. Fomu kwa ajili ya ushiriki wa kozi hiyo zinapatikana kwenye ofisi za TFF na tovuti ya TFF.

POLISI MORO, MTIBWA KUCHEZA MECHI YA TIKETI ZA ELEKTRONIKI

Timu za Mtibwa Sugar na Polisi Morogoro zinazojiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitacheza Jumamosi (Agosti 23 mwaka huu) mechi ya majaribio ya mfumo wa tiketi za elektroniki.
Mechi hiyo itafanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro kuanzia saa 10 jioni wakati kiingilio kitakuwa sh. 1,000.

Monday, August 18, 2014

SIMBA YAENDELEA NA TIZI ZANZIBAR

Simba wekundu wa Msimbazi Simba wanaendelea vyema na maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza kushika kasi septemba 30 mwaka huu.
Simba wameweka kambi visiwani Zanzibar (Unguja) chini ya kocha mkuu mpya, Mzambia, Patrick Phiri akisaidiwa na kocha msaidizi, kiungo wa zamani wa klabu hiyo na timu ya taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’, Suleiman Abdallah Matola ‘Veron’ na kocha wa makipa, Idd Pazzi ‘Father’.

FIFA KUBORESHA MAKAO MAKUU YA TFF

ofisi-za-TFFSHIRIKISHO la Mpira wa Miguu duniani (FIFA) limeahidi kuboresha makao makuu ya
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) yaliyoko kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala ili yawe katika kiwango cha kisasa ikiwa ni pamoja na kuwa na vitendea kazi na miundombinu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa ofisi.
Hatua hiyo itaiwezesha TFF kuwa na mazingira bora ya kufanya shughuli zake kwa ufanisi. Vilevile kupitia programu zake mbalimbali ikiwemo ile ya Goal, FIFA imeahidi kushirikiana na TFF katika kuendeleza mradi wa kiuchumi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

YANGA YATUA PEMBA KUWEKA CHIMBO LA VPL SEPT 20,2014

Msafara wa watu 35 ukiwa na wachezaji 27 na benchi la Ufundi 8 wa timu ya Young Africans tayari umeshawasili Kisiwani Pemba kwa ajili ya maandalizi ya mwisho kujiandaa na mikikimikiki ya Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2014/2015.
Kocha mkuuu Marcio Maximo na kikosi chake wamefikia katika hoteli ya kitalii ya Pemba Misali iliyopo eneo la Wesha na watakua wakijifua kwa muda wa takribani siku 10 kabla ya kurejea jijini Dar es salaam mwisho wa mwezi huu.
Kikosi cha Young Africans kitakua kikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Gombani mjini Chake Chake na siku ya alhamis wanataraji kucheza wa kwanza wa kirafiki dhidi ya timu ya Chipukizi ya kisiwani Pemba.
Kulingana na program ya bench la Ufundi kisiwani Pemba, Young Africans inatarajia kucheza michezo mitatu ya kirafiki na timu za kutoka Visiwa vya Pemba na Unguja na baadae kurejea Dar es salaam kwa michezo mwili ya kimataifa kabla ya kucheza mchezo wa Ngao ya Hisani septemba 13, 2014.
Wachezaji waliondoka kuelekea Pemba ni:
Walinda Mlango:
Juma Kaseja, Ally Musatfa "Barthez" na Deogratias Munish "Dida"
Walinzi wa Pembeni:
Juma Abdul, Salum Telea, Oscar Joshua, Edwad Charles na Amos Abel
Walinzi wa Kati:
Kelvin Yondani, Nadir Haroub "Cannavaro", Rajab Zahir na Pato Ngonyani.
Viungo:
Mbuyu Twite, Said Juma "Makapu", Omega Seme, Hassan Dilunga, Haruna Niyonzima na Hamis Thabit.
Viungo wa Pembeni:
Saimon Msuva, Mrisho Ngasa, Nizar Khalfani na Andrey Coutinho.
Washambuliaji:
Geilson Santos "Jaja", Said Bahanuzi, Jerson Tegete, Hamis Kizza na Hussein Javu 
Benchi la Ufundi walioko Kisiwani Pemba ni:
Kocha Mkuu : Marcio Maximo
Kocha wasaidizi Leonado Neiva, Salvatory Edward
Kocha wa Makipa:  Juma Pondamali
Daktari wa timu: Dr Suphian Juma
Meneja wa timu:  Hafidh Saleh
Mchua Misuli: Jaco Onyango
Mtunza Vifaa: Mahmod Omar "Mpogolo"

Saturday, August 16, 2014

MAN UNITED YAPOLEA KIPONDO NYUMBANI 2-1 SWANSEA CITY

MENEJA mpya wa klabu ya Manchester United ameanza vibaya kampeni zake za Ligi Kuu baada ya kushuhudia kikosi chake kikitandikwa mabao 2-1 dhidi ya Swansea city katika mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Old Trafford mchana wa leo.
Wageni Swansea ndio waliokuwa wa kwanza kuchukuliwa wavu wa United kwa bao lililofungwa na Ki Sung-yueng katika dakika ya 28 lakini bao hilo lilisawazishwa muda mfupi baada ya kuanza kipindi cha pili kupitia kwa nahodha wake Wayne Rooney.
Swansea walifunga bao lao la ushindi katika dakika ya 72 kupitia kwa Gyfi Sigurdsson hivyo kuifanya timu hiyo kupoteza mchezo wake wa ufunguzi nyumbani kwa mara ya kwanza toka mwaka 1972.
United walionekana kushindwa kabisa kutengeneza mipango ya kusawazisha bao hilo hatua ambayo mashabiki wake walionnekana kukata tamaa na kuanza kuondoka mapema uwanjani kabla ya mchezo kumalizika.
 Mashabiki wa United duniani kote kabla ya mchezo walionekana kuwa na imani kubwa na kikosi chao toka alipotua Van Gaal akichukua mikoba ya David Moyes ambaye alifanikiwa kushinda mechi zake zote za kirafiki alizocheza.