Monday, April 22, 2013

DROGBA VS ETOO KUWANIA TUZO GUU LA DHAHABU
WASHAMBULIAJI bora  barani Afrika, Didier Drogba na Samuel Eto’o
wameingizwa kwenye orodha ya kuwania tuzo ya Guu la Dhahabu mwaka 2013, kufuata nyayo za mshambuliaji wa Paris Saint Germain ya Ufaransa, Zlatan Ibrahimovic, aliyeshinda mwaka jana.
Manahodha hao wa Ivory Coast na Cameroon ni Waafrika pekee katika orodha ya wachezaji tisa walioingizwa kwenye kinyang’anyiro cha tuzi hiyo, inayotolewa kwa wachezaji wenye mafanikio makubwa na mwonekano mzuri.
Wawania tuzo hiyo wengine ni Mfaransa David Trezeguet, Mjerumani Miroslav Klose, Mtaliano Andrea Pirlo, Waspanyola Andres Iniesta na Iker Casillas na Waingereza Franck Lampard na David Beckham.
Tuzo huyo Guu la Dhahabu inatolewa kwa mchezaji aliye uwanjani ambaye angalau ana umri usiopungua miaka 29 na hawezi kushinda zaidi ya mara moja
Washindi wa awali wa tuzo hiyo ni; 2003: Roberto Baggio (Italia, Brescia) 2004: Pavel Nedved (Jamhuri ya Czech, Juventus) 2005: Andryi Shevchenko (Ukraine, AC Milan) 2006: Ronaldo (Brazil, Real Madrid) 2007: Alessandro Del Piero (Italia, Juventus) 2008: Roberto Carlos da Silva (Brazil, Fenerbahçe) 2009: Ronaldinho (Brazil, AC Milan) 2010: Francesco Totti (Italia, Roma) 2011: Ryan Giggs (Wales, Manchester United) na 2012: Zlatan Ibrahimovic (Sweden, Paris SG).

TAZAMA MECHI WALIZO CHEZA NA MAGOLI WALIOFUNGA
 Didier Drogba Games/Goals
2009/10 Chelsea 21/17
2008/09 Chelsea 24/5
2007/08 Chelsea 19/8
2006/07 Chelsea 36/20
2005/06 Chelsea 29/12
2004/05 Chelsea 26/10
2003/04 Marseille 35/19
2002/03 Guingamp 34/17
2001/02 Guingamp 10/3
2001/02 Le Mans 21/5
2000/01 Le Mans 11/0
1999/00 Le Mans 30/7
1998/99 Le Mans 2/0
TOTAL: 298/123

Samuel Eto
'o Games/Goals
2009/10 Inter 19/8
2008/09 Barcelona 36/30
2007/08 Barcelona 18/16
2006/07 Barcelona 17/11
2005/06 Barcelona 34/27
2004/05 Barcelona 37/25
2003/04 Mallorca 32/17
2002/03 Mallorca 29/14
2001/02 Mallorca 29/6
2000/01 Mallorca 25/11
1999/00 Mallorca 9/6
1999/00 R Madrid 2/0
1998/99 R Madrid 1/0
1997/98 Leganes 28/3
TOTAL: 316/174
  

BONDIA wa uzito wa juu wa Uingereza, Dereck Chisora amefanikiwa kumchakaza Hector Alfredo Avila katika raundi ya tisa likiwa ni pambano lake la kwanza toka alipopata kipigo kutoka kwa David Haye Julai mwaka jana. Chisora mwenye umri wa miaka 29 alikuwa akipigana pambano lake la kwanza toka aliporejeshewa leseni yake Machi mwaka huu baada ya leseni hiyo kuzuiwa kufuatia vurugu za nje ya ulingo alizofanya na Haye mapema mwaka huu. Akihojiwa mara baada ya kumpiga Avila ambaye ni raia wa Argentina Chisora amesema lilikuwa pambano gumu kwasababu mpinzani wake alikuwa amempania lakini anashukuru amemaliza kwa ushindi na anasubiri mpinzani mwingine. Chisora anasubiri pambano linguine dhidi ya bondia mwingine wa uzito wa juu wa Uingereza David Price ambaye kabla ya kupambana na Chisora atapigana na Tony Thompson katika pambano la marudiano Julai mwaka huu.

NUSU FAINALI UEFA CHAMPION LIGI KESHO WANAUME DIMBANI
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]
Jumanne Aprili 23
Bayern Munich v Barcelona
Jumatano Aprili 24
Borussia Dortmund v Real Madrid
MARUDIANO
Jumanne Aprili 30
Real Madrid v Borussia Dortmund
Jumatano Mei 1
Barcelona v Bayern Munich
FAINALI
25 Mei 2013
UWANJA wa WEMBLEY, Londo