Monday, April 22, 2013

FA USO KWA USO SUAREZ HUKU CLUB YAKE PIA IKIMTWANGA FAINI

 Chama cha Soka cha England "FA" kimetangaza kumfungulia Mashitaka Straika wa Liverpool Luis Suarez, kwa Kosa la kuleta vurugu Uwanjani kwa kumng’ata meno Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic.


Tukio hilo lilitokea Uwanjani Anfield Liverpool ilipotoka sare ya 2-2 na Chelsea katika Mechi ya BPL, Barclays Premier League lakini Refa Kevin Friend hakuliona kama ilivyothibitishwa na FA kufuatia Ripoti ya Refa na hivyo wao kupata fursa kumfungulia mashitaka kwa kutumia ushahidi wa Mikanda ya Video.
Mara baada ya tukio hapo Uwanjani Ivanovic alionekana akimuonyesha Refa Friend alama za meno mkononi mwake.
SUAREZ_KIDOLEFA pia imetamka kuwa kawaida makosa kama hayo ni Kifungo cha Mechi 3 lakini kwa tukio hilo Adhabu hiyo haitoshi.
Suarez amepewa had Aprili 23 Saa 2 Usiku mwaka huu awe amejibu Mashitaka hayo na
 Jumatano Aprili 24, Jopo Huru la FA litaketi kusikiliza Kesi hiyo.
Tayari Suarez ameshaomba radhi kwa kumuuma meno Ivanovic na kuongea na Beki huyo wa Chelsea.
Liverpool pia imetangaza kumpiga Faini lakini imesisitiza ataendelea kubakia kuwa Mchezaji wao.

OLIVIER GIROUD: ARSENAL KUPAMBANA KADI NYEKUNDU

Washika bunduki wa jiji la london  Arsenal chini ya meneja wenger" wamewasilisha Rufaa yao kupinga Kadi Nyekundu aliyopewa Straika wao mahili  Olivier Giroud Juzi Jumamosi Arsenal walipoifunga Fulham Bao 1-0 Uwanjani Craven Cottage kwenye Mechi ya Ligi.
Giroud alitolewa kwa kumchezea Rafu Stanislav Manolev.
Akielezea tukio hilo baada ya Mechi, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, alisema: “Giroud aliniambia aliteleza wakati akifuata Mpira na hilo limethibitishwa na Mikanda ya Video.”
Jopo Huru la FA litatoa uamuzi wake Siku ya Jumanne.
Ushindi huo wa Arsenal dhidi ya Fulham ulikuwa ushindi wao wa 5 katika Mechi 6 za Ligi na umezidi kuwaimarisha katika azma yao ya kumaliza kwenye 4 Bora.
Arsenal sasa wapo nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 63.
Tangu ajiunge na Arsenal kutoka Montpellier mapema mwanzoni mwa Msimu huu, Giroud amepachika Bao 17 katika Mechi zake 46 na Arsenal.
ARUDI TENA NDANI YA STAMFORD BRIDGE"
CLATTENBURG1
REFA Mark Clattenburg anatajiwa kurudi katika dimba la Stamford Bridge kuichezesha Chelsea kwa mara ya kwanza tangu asafishwe suala la Ubaguzi dhidi ya John Obi Mikel na huko Emirates, Arsenal i
CLATTENBURG NA CHELSEA
JUMAPILI, Refa Mark Clattenburg atarudi Uwanja wa Stamford Bridgekuichezesha Chelsea kwa mara ya kwanza baada ya Miezi 6 baada ya kusafishwa kutumia Ubaguzi dhidi ya Kiungo wa Chelsea John Obi Mikel.
Chelsea walilalamika kuwa Clattenburg alitumia lugha isiyofaa dhidi ya Mikel wakati wanachapwa Bao 3-2 na Manchester United Mwezi Oktoba Mwaka jana Uwanjani Stamford Bridge.
Baada ya uchunguzi wa FA, Refa huyo, ambae alitamka jambo hilo limemtisha, Clattenburg alisafishwa kuhusu tuhuma zote.
Baadae Klabu ya Chelsea ilitoa tamko la kusikitika kuhusu walivyochukulia suala hilo na kutaka radhi na sasa, Miezi 6 baadae, Clattenburg ataichezesha Chelsea watakapocheza na Swansea City