Monday, April 29, 2013

MAKAMU M/KITI SIMBA AIPONGEZA YANGA KUTWAA UBINGWA


KLABU ya Simba imewapongeza watani zao Yanga kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara huku wakiapa kuwatibulia furaha kwa kuwafunga katika mechi ya kufunga pazia la ligi hiyo itakayochezwa Mei 18 kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Joseph Itang’ale ikiwa ni siku chache tangu Yanga itwae ubingwa wa ligi hiyo baada ya Azam kutoka sare ya bao 1-1 na Coastal Union ya Tanga, hivyo kutokewepo timu yenye ubavu wa kuzifikia pointi 56 ilizonazo hadi sasa.
Kinesi amesema pamoja na pongezi hizo, wajiandae kwani wamejipanga kutibua furaha hiyo kwa kuwafunga na kamwe hawawezi kukubali kuvuliwa ubingwa na kufungwa na mtani wao.
Kinesi ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo anayekaimu nafasi ya Makamu Mwenyekiti baada ya kujiuzulu kwa Geofrey Nyange  amesema japo watani zao wametwa ubingwa, wasitarajie ushindi Mei 18.
 ambapo wekundu hao ndio mabingwa wa msimu uliopita baada ya kuwachalaza watani hao bao 5-0 toka ligi kuu ianzishwe simba imetwaa taji hilo mara 18 huku yanga ikitwaa mara 24
Mwaka 1965, 1966 (as Sunderland)
1972, 1973, 1976, 1977, 1978, 1979, 1980, 1993, 1994, 1995, 2001/02, 2002/03, 2004/05, 2007/08, 2009/10, 2011/12 
Mwaka1968, 1969, 1970, 1971, 1972, 1974, 1981, 1983, 1985, 1987, 1989, 1991, 1992, 1993, 1996, 1997, 1998, 2002, 2005, 2006, 2008, 2009, 2011,2013