Ligi kuu ya Zanzibar Grand Malt msimu wa 2012/2013 imemalizika
rasmi mwishoni mwa wiki ambapo timu ya KMKM imefanikiwa kuwa bingwa mpya huku
timu ya Chuoni ikitwaa nafasi ya pili.
mabingwa watetezi wa ligi hiyo Super Falcon imepatwa
na balaa na kushindwa kuhimili mikikimikiki na hatimaye kushuka daraja.
kutokana na kufanikiwa kutwaa ubingwa KMKM ndiyo itaiwakilisha
Zanzibar katika Ligi ya Mabingwa Afrika, wakati Chuoni watajitupa katika michuano
ya Kombe la Shirikisho.
Kmkm imefanikiwa kutwaa kombe, medali ya dhahabu kwa timu nzima pamoja na fedha taslimu Sh milioni 10, huku mshindi wa pili Chuoni akipata Sh milioni 5 pamoja na medali ya fedha kwa kila mchezaji.
Golikipa bora bora alikuwa ni Khamis Uzidi wa Zimamoto ambaye alikabidhiwa kikombe pamoja na fedha taslimu Sh 500,000 huku mfungaji bora wa ligi hiyo, Juma Mohd Juma wa Chuoni akijipatia Sh milioni 1 na kikombe.
Kmkm imefanikiwa kutwaa kombe, medali ya dhahabu kwa timu nzima pamoja na fedha taslimu Sh milioni 10, huku mshindi wa pili Chuoni akipata Sh milioni 5 pamoja na medali ya fedha kwa kila mchezaji.
Golikipa bora bora alikuwa ni Khamis Uzidi wa Zimamoto ambaye alikabidhiwa kikombe pamoja na fedha taslimu Sh 500,000 huku mfungaji bora wa ligi hiyo, Juma Mohd Juma wa Chuoni akijipatia Sh milioni 1 na kikombe.
Mchezaji bora wa Grand Malt premier League ni Abdullah Juma wa
Jamhuri ya Pemba aliyekabidhiwa Sh milioni 1 taslimu pamoja na kikombe.
Mbali na hilo wadhamini wa ligi hiyo ilitoa zawadi
kwa timu za madaraja mengine ambayo mshindi wa kwanza na wa pili katika Ligi
Daraja la Kwanza ambazo ni Miembeni na Polisi zilikabidhiwa seti ya jezi na
vikombe.
Zawadi hizo zilitolewa kwa mshindi wa kwanza na wapili wa Ligi Daraja la Pili ambazo ni Kimbunga na Bweleo fc.
Zawadi hizo zilitolewa kwa mshindi wa kwanza na wapili wa Ligi Daraja la Pili ambazo ni Kimbunga na Bweleo fc.