Monday, May 6, 2013

RCL MCHAKATO WA UPANGAJI KUCHUKUA NAFASI KESHO"

MCHAKATO wa  upangaji wa ratiba ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) uliokuwa ufanyike juzi (Mei 3 mwaka huu), sasa utafanyika kesho Jumanne (Mei 7 mwaka huu) na ligi hiyo itaanza Mei 12 mwaka huu kama ilivyopangwa.
Uamuzi huo umefanya na Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliyokutana jana (Mei 5 mwaka huu) kujadili maandalizi ya ligi hiyo, yakiwemo maombi ya baadhi ya mikoa ambayo haijamaliza yao kutaka RCL isogezwe mbele.
Kamati ya Mashindano chini ya Uenyekiti wa Blassy Kiondo ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF ilipitia maombi hayo na kuangalia athari ambazo zinaweza kujitokeza huko mbele iwapo RCL itasogezwa mbele.
Baadhi ya athari iwapo RCL itasogezwa mbele ni timu zitakazopanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kutopata muda wa kufanya usajili wa wachezaji kwa msimu mpya.

Hivyo draw hiyo itakayofanyika saa 6 mchana itahusisha mikoa ambayo tayari imemaliza ligi na kuwasilisha majina ya mabingwa wao. 
ni Abajalo SC (Dar es Salaam 2), Biharamulo FC (Kagera), Flamingo SC (Arusha), Friends Rangers (Dar es Salaam 3), Katavi Warriors (Katavi), Kiluvya United (Pwani), Kimondo FC (Mbeya) na Machava FC (Kilimanjaro).
Mingine ni Magic Pressure FC (Singida), Mbinga United (Ruvuma), Mji Njombe (Njombe), Polisi Jamii Bunda FC (Mara), Red Coast FC (Dar es Salaam 1), Rukwa United (Rukwa), Saigon FC (Kigoma), TECKFOLT FC ya Kilombero ambayo ni Shule ya Sekondari (Morogoro) na UDC FC ya Ukerewe (Mwanza).
Ada ya ushiriki ni sh. 100,000 wakati usajili wa wachezaji wa timu hizo ni uleule uliofanyika katika Ligi ya Mkoa na unatakiwa kuwasilishwa TFF kwa ajili ya uthibitisho.

TFF inapenda kusisitiza kuwa hakuna usajili mpya wa wachezaji kwa ajili ya ligi hiyo. Mikoa ambayo bado haijawasilisha mabingwa wake ni Dodoma, Geita, Iringa, Lindi, Manyara, Mtwara, Shinyanga, Simiyu, Tabora na Tanga.

KAGAME SASA NI WAKATI WA DARFUR NA KORDOFAN YA KUSINI.

KATIBU Mkuu wa Baraza la Michezo kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati-CECAFA, Nicholas Musonye amesema wameteua miji Darfur na Kordofan ya Kusini nchini Sudan kuwa wenyeji wa michuano ya vilabu inayoandaliwa na baraza hilo. Musonye amesema michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kati ya June 18 na Julai 2 mwaka huu. Aliendelea kusema kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya kufanya ziara ya kukagua miundo mbinu pamoja na usalama katika miji hiyo ambayo imekabiliwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa kipindi kirefu sasa. Amesema viwanja walivyochagua ni Uwanja wa El Fasher uliopo jijini Darfur na uwanja mwingine mdogo wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 20,000 uliopo Kordofan ya Kusini. Vilabu 13 vimeshathibitisha kushiriki michuano hiyo wakiwemo Yanga ya Tanzania ambao ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo.